Sunday, 13 July 2025

PICHANI BIDHAA ZA NISHATI SAFI YA KUPIKIA


 Kama inavyoonekana Pichani Jiko linalotumia mkaa mbadala  pamoja na mkaa wennyewe mbadala kwenye viwanja vya sabasaba  maonyesho  jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

TIRDO YAJA NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA


 Devid Langa Afisa Uhusiano  na Mawasiliano TIRDO  amesema wanatebgeneza na kupima majiko yanayotumia nishati mbadala vile vile TIRDO  inatoa mafunzo ya namna ya kutengeneza mkaa mbadala .,Mkaa huu auchafui mazingira kwani nishati yake ya kupikia ni safi na salama .

TIRDO imetoa mafunzo kwenye mikoa 12 juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia pia  kwa upande mwingine TIRDO  inatoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu wa aina zote  na kuwafanyia hatamizi amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yaliofanyika jijini dar es salaam .

Habari picha na Victoria Stanslaus 

WAZIRI MKUU ASIFU NA KUPONGEZA MAONYESHO YA SABASABA YA 49

 Majaliwa Kasimu Majaliwa  Waziri Mkuu wa Tanzania amesema maonyesho ya Sabasaba ya 49 ambayo yamefanyika  wilayani temeke jijini dar es salaam  yamekuwa yenye tija kwa Wajasiliamali,Wafanya biashara wadogo ,Wakati na Wakubwa kwani wameweza kutangaza bidhaa zao kitaifa na kimataifa pia wamepata masoko ndani ya nchi na nje ya nchi.

Waziri  Mkuu  Kasimu Majaliwa  amesema sekta ya utalii imetangazwa vyema kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 na yamepelekea kuvutia walii kuja kutaliina kuwekeza ,vile vile ameupongeza uongozi wa TANTRADE  chini ya Mkurugenzi Mkuu  Bi Latifa kwa ubunifu wake kwa kuyafanya maonyesho ya Sabasaba ya 49 kwa njia ya kidigitali .

Bi Latifa Muhamed  amepongezwa na Waziri  Mkuu  Majaliwa kasimu Majaliwa  Waziri Mkuu  wa tanzania kwa kuweka mifumo imala ya kiteknolojia kwa waombaji maeneo ya kufanyia biashara zao na kununua tiketi kwa njia ya mtandao  amesema haya wakati akifunga maonyesho ya Sabasaba ya 49 yaliofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam  kuanzia tarehe 28 mwezi6 2025 na hatimae yamefungwa na Waziri Mkuu  Kasimu Majaliwa  tarehe 13 mwezi 7 mwaka 2025. 

Habari na Ally Thabit Mbungo 

TBA YAJA NA MIKAKATI MIZITO


  Martin Sayeli Afisa Mipango Idara ya Milki Wakala wa Majengo Nchini Tanzania (TBA) wanatekeleza kwa vitendo miradi yote ya ujenzi wa nyumba za serikali ambako nyumba hizi wanauziwa na kupangishiwa watumishi wa serikali na watu binausi .

TBA inajenga nyumba rafiki na wezeshi kwa makundi yote kwa watumishi wa serikali wanapangishwa nyumba kwa kiasi cha shiringi milioni moja  nawasio wa serikali milioni moja na laki tano . TBA  wameweka vutasa janja kwenye milango lengo ni kukabiliana na kuwadhibiti wapangaji ambao awalipi kodi.

Amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es. 

Habari picha na Victoria Stanslaus. 

PICHANI BIDHAA ZA KAMPUNI YA TANFOAM

 

Kama Inavyoonekana Kitanda .Mito, Taulo ,Mito ya duara na Vishikizia miguu vyote vinapatikana kwenye TANFOAM  LIMITED  vilevile TANFOAM wana vitanda pamoja na magodoro ambayo ni rafiki kwa watu wenye changamoto ya uti wa mgongo .

Hivi vyote vinapatikana ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye banda la Karume kwenye maonyesho ya  Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam. Pia wanapatikana kwa mawakala wao waliopo nchi nzima tanzania na kwenye maduka yao yote.

Habari picha na Ally Thabit 

TANFOAM YAJA KIVINGINE KWEMBE MAONYESHO YA SABASABA YA 49

 

Daniel Philipo Marko Afisa Mauzo wa Kampuni ya Tonfoam amesema kwenye maonyesho  ya Sabasaba  ya 49  kampuni yao imeleta bidhaa zenye ubora na zenye gharama nafuu kwa wateja wa jumla na lejaleja . Miongoni mwa bidhaa ambazo wamezileta kampuni ya  Tanfoam Magodoro,Vitanda,Taulo, Mito na Mashuka .

Afisa Mauzo amesema kulingana na msimu huu wa Sabasaba  kuna punguzo la bidhaa zao kwa asilimia 10  kuanzia tarehe 1 mwezi wa 7 2025 mpaka tarehè 31 mwezi wa 7 mwaka 2025.Kampuni hii ya Tanfoam ina miaka 55 tangu kuanzishwa ,Pia ina maduka yao binausi mfano Masaki,Vingunguti,Tegeta na ina mawakqla tanzania nzima  kanda ya Magharibi ,Nyanda za juu kusini,Kanda ya kaskazini,Kanda ya kati ,Kanda ya kati  na kanda ya Mashariki.

Licha Tanfoam  kufanya biashara vilevile inatoa fursa kwa watu kwa kuwaajili ama kujiajili wenyewe kwa kuwapa bidhaa zao kwa makubaliano ivyo ametoa rai kwa vijana na watu wengineo kutumia kampuni ya Tanfoam  ili wajikwamuwe kiuchumi na amewataka kutembelea viwanja vya Sabasaba kwenye  banda la Karume watakutana na watoa huduma wa kampuni ya  TANFOAM  ambako watawahudumia kwa uraisi.

Ametoa wito kwa watu kutumia bidhaa za  Tanfoam  kwani zina ubora amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 ndani ya viwanja vya Sabasaba  wilayani  temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo. 

Saturday, 12 July 2025

PICHANI NI KAHAWA AINA YA ARABICA INAYOPATIKANA KWENYE CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHA MKOANI MARA WAMACU LIMITED


 Chama Kikuu cha Ushirika kutoka Mkoani MARA WAMACU COOPERATIVE UNION  LMT kama inavyoonekana pichani hii ni kahawa aina ya Arabica inayouzwa kwa bei rafiki kwa kila mtu. Hivyo ni vyema watu wafike ndani ya viwanja vya Sabasaba  kwenye maonyesho ya 49 kwenye banda la Wizara ya Kilimo wanunue kahawa hii aina ya Arabica kutoka mkoani mara .

Habari picha na Ally Thabit Mbungo