Friday, 11 July 2025

MAMLAKA YA AFYA YA MIMEA NA VIWATILIFU TANZANIA YAMPONGEZA RAIS SAMIA


 Dr Mujuni Kabululu Kaimu Mkuu Kitengo cha Kuifadhi Nasaba za Mimea Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viwatilifu Tanzania  amempongeza rais Dr Samia  kwa kuweza kununua ndege kwaajili ya kupambana na kuwadhibiti Viwavijeshi,Kweleakwelea na Nzige .

Ndege hii imekuwa mkombozi kwa wakulima ambao mazao yao yalikuwa yanaaribiwa na  vivamizi  hata ivyo serikali itaepukana na gharama ya kukodi ndege nchi za nje kwaajili ya kudhibiti kwelea Kwelea,Viwa vijashi , Nzige na Panya .

Dr Mujuni amesema Mamlaka yao inatoa vibali vya kuingiza na kupeleka nje ya nchi mazao vilevile Mamlaka  hii inatoa vibali vya kuingiza viwatilifu na kusambaza teknolojia  kwa wakulima na wanatoa elimu kupitia Almashauri  kwa wakulima namna ya kutumia viwatilifu kwenye mazao yao .

Pia wanatumia redio,TV,Vipeperushi  na Mafunzo mbalimbali kwa wakulima anawataka watu wote kufika  kwenye banda la Wizara ya Kilimo na kutembelea Mamlaka  ya Afya ya Mimea na Viwatilifu Tanzania  ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye maonyesho ya 49 yanayofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 

No comments:

Post a Comment