Wednesday, 9 July 2025

TANTRADE MPYA NA YENYE UBUNIFU YANG'ARA KITAIFA NA KIMATAIFA


 Mkurugenzi Mkuu Mtendaji  wa TANTRADE  Latifa Muhamed amesma ubunifu alioufanya na maboresho alioyafanya ndani ya TANTRADE yamepelekea TANTRADE  kuwa mpya na ya kisasa ndio maana inang'ara kitaifa na kimataifa na kupelekea wafabiashara na wawekezaji kuchangamkia fursa mbalimbali.

Mkurugenzi  ZLatifa Muhamed amesema ameamuwa kuweka mifumo ya Tehama  kwa watu wanaoitaji huduma za TANTRADE  na ukataji wa tiketi kwa njia ya Kieletronik Lengo fedha ya serikali iingie moja kwa moja serikalini  hili kusiwe na ubadhirifu na zisipotee na hili TANTRADE imefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Vilevile TANTRADE imefungua matawi Mwanza ,Arusha,Mbeya,Dodoma na Zanzibar  Lengo kuwafikia wateja kwa uraisi. TANTRADE ndani ya viwanja vya Sabasaba kutajengwa majengo ya kisasa ambako magari yatakuwa na sehemu ya kupaki,Sehemu ya watoto kucheza na biashara zitakuwa zinafanyika wakati wote.

Latifa Muhamed anatekeleza kwa vitendo farsafa na maono ya rais Dr Samia  na huku akimpongeza rais Dr Samia  kwa kuiwezesha TANTRADE kufanya mabadiriko amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam .

Habari picha na Victoria Stanslaus 


No comments:

Post a Comment