Saturday, 5 July 2025

PPRA YAWAFIKIA WATU WENYE ULEMAVU


 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PPRA  Josefu Muozi amesema watu wenye ulemavu katika  kupata fursa za tenda za PPRA  wamefikiwa kwa kiwango kikubwa huu ni mpango maalum ulioandaliwa na serikali tangu mwaka 2011 na sheria ya PPRA  ikafanyiwa maboresho mwaka 2023  ambako maboresho haya yamesaidia kwa kiasi kikubwa watu wenye ulemavu wa aina zote kupata zabuni za tenda za PPRA. 

Pia PPRA  imeandaa majarida yenye maandishi ya nukta nundu kwaajili ya walemavu wasio Ona na vifaa vya kurekodia sauti zana hizi zimewezesha watu wenye ulemavu kupata elimu na uwelewa kuhusu  zabuni na tenda zinazotolewa na PPRA  vilevile PPRA  inatoa elimu kwa watu wote kupitia redio,tv,magazeti,na makongamano pamoja na semina  kupitia taasisi za watu wenye ulemavu. 

Josefu Muozi amewataka watu kutembelea banda la PPRA  viwanja vya sabasaba maonyesho Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam kwenye maonyesho ya 49 habari picha na Victoria Stanslaus. 


No comments:

Post a Comment