Monday, 7 July 2025

RAIS WA ZANZIBAR AVUTIWA NA UONGOZI WA TANTRADE

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti  wa Baraza la Wawakirishi Zanzibar Dr Hoseni Mwinyi amewapongeza viongozi wa TANTRADE chini ya Mkurugenzi Mkuu Mtendaji  Ratifa Ali Muhammed kwa kutafasiri kwa vitendo farsafa ya Dr Samia  na maono yake ya kukuza biashara ya mtu mmoja mmoja   au makundi mbalimbali kwa kuweza kufanya ubunifu kwenye  maonyesho ya Sabasaba  kwa kuweka mifumo ya kujisajili kwaajili ya kupata mabanda na ukataji tiketi kwa njia ya mtandao ambako inasaidia fedha ya serikali kuingia moja kwa moja bila kupitia mikononi mwa watu.

Pia wameweza kukamilisha mpango wa ujenzi wa kiwanja cha kisasa cha maonyesho ya sabasaba .

Uwepo wa ubunifu wa maonyesho wa bidhaa za nchi za kigeni mfano siku China ,Japani huku ni kukuza dipromasia  ya Kiuchumi. Rais wa Zanzibar ameiakikishia TANTRADE yeye na rais Samia wataendelea kuwapa ushirikiano wa Ali na mali na serikali ina mikakati mikubwa juu ya TANTRADE. 

Rais amezindua Nembo ya Bidhaa za Tanzania  ambako hii ni alama ya kutamburisha bidhaa zetu kitaifa na kimataifa amesema haya tarehe 7 mwezi wa 7 2025 ndani ya viwanja vya Sabasaba wilayani temeke jijini dar es salaam  wakati alipofungua maonyesho ya sabasaba  ya 49.

Habari na Ally Thabit Mbungo. 

No comments:

Post a Comment