Sunday, 13 July 2025

WAZIRI MKUU ASIFU NA KUPONGEZA MAONYESHO YA SABASABA YA 49

 Majaliwa Kasimu Majaliwa  Waziri Mkuu wa Tanzania amesema maonyesho ya Sabasaba ya 49 ambayo yamefanyika  wilayani temeke jijini dar es salaam  yamekuwa yenye tija kwa Wajasiliamali,Wafanya biashara wadogo ,Wakati na Wakubwa kwani wameweza kutangaza bidhaa zao kitaifa na kimataifa pia wamepata masoko ndani ya nchi na nje ya nchi.

Waziri  Mkuu  Kasimu Majaliwa  amesema sekta ya utalii imetangazwa vyema kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 na yamepelekea kuvutia walii kuja kutaliina kuwekeza ,vile vile ameupongeza uongozi wa TANTRADE  chini ya Mkurugenzi Mkuu  Bi Latifa kwa ubunifu wake kwa kuyafanya maonyesho ya Sabasaba ya 49 kwa njia ya kidigitali .

Bi Latifa Muhamed  amepongezwa na Waziri  Mkuu  Majaliwa kasimu Majaliwa  Waziri Mkuu  wa tanzania kwa kuweka mifumo imala ya kiteknolojia kwa waombaji maeneo ya kufanyia biashara zao na kununua tiketi kwa njia ya mtandao  amesema haya wakati akifunga maonyesho ya Sabasaba ya 49 yaliofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam  kuanzia tarehe 28 mwezi6 2025 na hatimae yamefungwa na Waziri Mkuu  Kasimu Majaliwa  tarehe 13 mwezi 7 mwaka 2025. 

Habari na Ally Thabit Mbungo 

No comments:

Post a Comment