Sunday, 13 July 2025

TANFOAM YAJA KIVINGINE KWEMBE MAONYESHO YA SABASABA YA 49

 

Daniel Philipo Marko Afisa Mauzo wa Kampuni ya Tonfoam amesema kwenye maonyesho  ya Sabasaba  ya 49  kampuni yao imeleta bidhaa zenye ubora na zenye gharama nafuu kwa wateja wa jumla na lejaleja . Miongoni mwa bidhaa ambazo wamezileta kampuni ya  Tanfoam Magodoro,Vitanda,Taulo, Mito na Mashuka .

Afisa Mauzo amesema kulingana na msimu huu wa Sabasaba  kuna punguzo la bidhaa zao kwa asilimia 10  kuanzia tarehe 1 mwezi wa 7 2025 mpaka tarehè 31 mwezi wa 7 mwaka 2025.Kampuni hii ya Tanfoam ina miaka 55 tangu kuanzishwa ,Pia ina maduka yao binausi mfano Masaki,Vingunguti,Tegeta na ina mawakqla tanzania nzima  kanda ya Magharibi ,Nyanda za juu kusini,Kanda ya kaskazini,Kanda ya kati ,Kanda ya kati  na kanda ya Mashariki.

Licha Tanfoam  kufanya biashara vilevile inatoa fursa kwa watu kwa kuwaajili ama kujiajili wenyewe kwa kuwapa bidhaa zao kwa makubaliano ivyo ametoa rai kwa vijana na watu wengineo kutumia kampuni ya Tanfoam  ili wajikwamuwe kiuchumi na amewataka kutembelea viwanja vya Sabasaba kwenye  banda la Karume watakutana na watoa huduma wa kampuni ya  TANFOAM  ambako watawahudumia kwa uraisi.

Ametoa wito kwa watu kutumia bidhaa za  Tanfoam  kwani zina ubora amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 ndani ya viwanja vya Sabasaba  wilayani  temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo. 

No comments:

Post a Comment