Monday, 7 July 2025

MWALIMU KINTU AELEZA MAGUMU VETA WALIOPITIA KWA WATU WENYE ULEMAVU

 

Mwalimu Kintu  anaefundisha Watu wenye Ulemavu  Chuo cha Veta amesema katika kutoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu  ya fani mbalimbali Veta Dar es salaam  ndio wa kwanza kutoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu. 

Mwalimu Kintu amesema iliwachukuwa miaka saba kufanya ushawishi kwa Vyuo  vya Veta  mikoa ya tanzania kuwapokea na kuwafundisha watu wenye ulemavu  ambako kwa sasa amejawa na furaha kwa kuona mafunzo ya fani mbali mbali yanatolewa kwenye Vyuo vya Veta  vyote nchini kwa watu wenye ulemavu wa aina zote.

Mwalimu Kintu amesema kuwepo kwa sera inayowatambua watu wenye ulemavu  kuwa na wao wana haki ya kupata mafunzo kupitia Veta ni jambo zuri. 
Habari picha na Ally Thabit. 

No comments:

Post a Comment