Kama inavyoonekana Pichani Jiko linalotumia mkaa mbadala pamoja na mkaa wennyewe mbadala kwenye viwanja vya sabasaba maonyesho jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
TIRDO imetoa mafunzo kwenye mikoa 12 juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia pia kwa upande mwingine TIRDO inatoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu wa aina zote na kuwafanyia hatamizi amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yaliofanyika jijini dar es salaam .
Habari picha na Victoria Stanslaus
Majaliwa Kasimu Majaliwa Waziri Mkuu wa Tanzania amesema maonyesho ya Sabasaba ya 49 ambayo yamefanyika wilayani temeke jijini dar es salaam yamekuwa yenye tija kwa Wajasiliamali,Wafanya biashara wadogo ,Wakati na Wakubwa kwani wameweza kutangaza bidhaa zao kitaifa na kimataifa pia wamepata masoko ndani ya nchi na nje ya nchi.
Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema sekta ya utalii imetangazwa vyema kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 na yamepelekea kuvutia walii kuja kutaliina kuwekeza ,vile vile ameupongeza uongozi wa TANTRADE chini ya Mkurugenzi Mkuu Bi Latifa kwa ubunifu wake kwa kuyafanya maonyesho ya Sabasaba ya 49 kwa njia ya kidigitali .
Bi Latifa Muhamed amepongezwa na Waziri Mkuu Majaliwa kasimu Majaliwa Waziri Mkuu wa tanzania kwa kuweka mifumo imala ya kiteknolojia kwa waombaji maeneo ya kufanyia biashara zao na kununua tiketi kwa njia ya mtandao amesema haya wakati akifunga maonyesho ya Sabasaba ya 49 yaliofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam kuanzia tarehe 28 mwezi6 2025 na hatimae yamefungwa na Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa tarehe 13 mwezi 7 mwaka 2025.
Habari na Ally Thabit Mbungo
TBA inajenga nyumba rafiki na wezeshi kwa makundi yote kwa watumishi wa serikali wanapangishwa nyumba kwa kiasi cha shiringi milioni moja nawasio wa serikali milioni moja na laki tano . TBA wameweka vutasa janja kwenye milango lengo ni kukabiliana na kuwadhibiti wapangaji ambao awalipi kodi.
Amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es.
Habari picha na Victoria Stanslaus.
Kama Inavyoonekana Kitanda .Mito, Taulo ,Mito ya duara na Vishikizia miguu vyote vinapatikana kwenye TANFOAM LIMITED vilevile TANFOAM wana vitanda pamoja na magodoro ambayo ni rafiki kwa watu wenye changamoto ya uti wa mgongo .
Hivi vyote vinapatikana ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye banda la Karume kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam. Pia wanapatikana kwa mawakala wao waliopo nchi nzima tanzania na kwenye maduka yao yote.
Habari picha na Ally Thabit
Daniel Philipo Marko Afisa Mauzo wa Kampuni ya Tonfoam amesema kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 kampuni yao imeleta bidhaa zenye ubora na zenye gharama nafuu kwa wateja wa jumla na lejaleja . Miongoni mwa bidhaa ambazo wamezileta kampuni ya Tanfoam Magodoro,Vitanda,Taulo, Mito na Mashuka .
Afisa Mauzo amesema kulingana na msimu huu wa Sabasaba kuna punguzo la bidhaa zao kwa asilimia 10 kuanzia tarehe 1 mwezi wa 7 2025 mpaka tarehè 31 mwezi wa 7 mwaka 2025.Kampuni hii ya Tanfoam ina miaka 55 tangu kuanzishwa ,Pia ina maduka yao binausi mfano Masaki,Vingunguti,Tegeta na ina mawakqla tanzania nzima kanda ya Magharibi ,Nyanda za juu kusini,Kanda ya kaskazini,Kanda ya kati ,Kanda ya kati na kanda ya Mashariki.
Licha Tanfoam kufanya biashara vilevile inatoa fursa kwa watu kwa kuwaajili ama kujiajili wenyewe kwa kuwapa bidhaa zao kwa makubaliano ivyo ametoa rai kwa vijana na watu wengineo kutumia kampuni ya Tanfoam ili wajikwamuwe kiuchumi na amewataka kutembelea viwanja vya Sabasaba kwenye banda la Karume watakutana na watoa huduma wa kampuni ya TANFOAM ambako watawahudumia kwa uraisi.
Ametoa wito kwa watu kutumia bidhaa za Tanfoam kwani zina ubora amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 ndani ya viwanja vya Sabasaba wilayani temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Ivyoamesema bei zao ni rafiki na nafuu kwa wateja wao na pia kahawa inawawezesha watu kupata ajira amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Kahawa yao aina ya Arabika ina ubora ivyo wanawataka watanzania na wasio watanzania kutumia kahawa yao aina ya Arabika . Chama kikuu cha Wakulima Mkoani MARA WAMACU LIMITED itafanya ka'i ya kufungua masoko jijini dar es salaam na mikoa mingine kwaajili ya kuwafikia wateja wao amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 kwenye banda la Wizara ya Kilimo .
Habari picha na Ally Thabit
Ndege hii imekuwa mkombozi kwa wakulima ambao mazao yao yalikuwa yanaaribiwa na vivamizi hata ivyo serikali itaepukana na gharama ya kukodi ndege nchi za nje kwaajili ya kudhibiti kwelea Kwelea,Viwa vijashi , Nzige na Panya .
Dr Mujuni amesema Mamlaka yao inatoa vibali vya kuingiza na kupeleka nje ya nchi mazao vilevile Mamlaka hii inatoa vibali vya kuingiza viwatilifu na kusambaza teknolojia kwa wakulima na wanatoa elimu kupitia Almashauri kwa wakulima namna ya kutumia viwatilifu kwenye mazao yao .
Pia wanatumia redio,TV,Vipeperushi na Mafunzo mbalimbali kwa wakulima anawataka watu wote kufika kwenye banda la Wizara ya Kilimo na kutembelea Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viwatilifu Tanzania ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye maonyesho ya 49 yanayofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit
Moja ya majukumu ya TARI kufanya utafiti wa Afya ya Udongo,Utafiti wa mazao na Ugunduzi wa mbegu bora,Kulinda mazao yasishambuliwe na wadudu pamoja na magonjwa mbalimbali, Namna ya kuongeza thamani kwenye mazao na kutunza pia wanawafundisha na kufanya utafiti wa za kuifadhi na kusindika mazao pamoja na kuwapelekea teknolojia mbalimbali.
Amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 wilayani temeke jijini dar es salaam kwenye banda la TARI.
Habari picha na Ally Thabit
Maombi ya watu kutaka kuwepo kwa Tembo na Twiga watafanyia kazi kutokana na mazingira ya Ikolojia hata ivyo amewataka watu kufika eneo la Pande lililopo Bunju ambako kuna hifadhi ya wanyamapori ambako kiingilio elfu 11800 .
Habari picha na Victoria Stanslaus
Kama inavyoonekana pichani mazao ya Mpunga na Korosho amesema haya ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye banda la CBE kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit
Petro amewaakikishia watu kuwa mfumo huu ni salama huku akitoa wito watu wajiunge na Chuo Kikuu cha CBE amesema haya ndani ya banda la CBE lililopo kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 wilaya ya temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit
Kozi hizi zinatolewa Asubuhi mpaka jioha nawengine wanaingia joini mpaka usiku Pia Chuokikuu cha CBE wanatoa kozi za muda mfupi mfano . Wanashirikiana na Latra kwaajili ya kutoa mafunzo kwa watoa huduma kwenye mabasi na madereva wa bodaboda .
Bi jakrene E Kaaya anawataka watu kutembelea banda la CBE ili waweze kujisajili kwaajili ya kupata elimu Chuokikuu cha CBE ambako chuo hiki kina miaka 60 amesma haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 wilaya ya temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Victoria Stanslaus
Mkurugenzi ZLatifa Muhamed amesema ameamuwa kuweka mifumo ya Tehama kwa watu wanaoitaji huduma za TANTRADE na ukataji wa tiketi kwa njia ya Kieletronik Lengo fedha ya serikali iingie moja kwa moja serikalini hili kusiwe na ubadhirifu na zisipotee na hili TANTRADE imefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Vilevile TANTRADE imefungua matawi Mwanza ,Arusha,Mbeya,Dodoma na Zanzibar Lengo kuwafikia wateja kwa uraisi. TANTRADE ndani ya viwanja vya Sabasaba kutajengwa majengo ya kisasa ambako magari yatakuwa na sehemu ya kupaki,Sehemu ya watoto kucheza na biashara zitakuwa zinafanyika wakati wote.
Latifa Muhamed anatekeleza kwa vitendo farsafa na maono ya rais Dr Samia na huku akimpongeza rais Dr Samia kwa kuiwezesha TANTRADE kufanya mabadiriko amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam .
Habari picha na Victoria Stanslaus
Meneja Mahusiano na Mawasiliano Tume ya Madini Greyson amesema tume ya madini nchini tanzania imewafikia na itaendelea kuwafikia watu wenye ulemavu wa aina zote pia tume ya madini imefungua masoko 43 na vituo vya ununuzi wa madini kwa tanzania 109 Lengo la serikali kufanya hivi ni kutoa usumbufu kwa wauzaji na wanunuzi wa madini.
Leseni mbalimbali tume ya madini inatoa miongoni mwao ni Leseni ya Utafiti wa Madini,Leseni ya uchimbaji wa madini , Uchenjuaji madini, Usafishaji wa madini na zinginezo ambako tume ya madini inatoa Leseni kupitia mifumo ya Tehama Lengo kuondoa urasimu na kuarakisha kupatikana kwa muda mfupi ambako ndani ya mwezi mmoja unapata Leseni.
Egera Doto amewataka watu kufika kwenye banda la tume ya madini ndani ya viwanja vya maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Wawakirishi Zanzibar Dr Hoseni Mwinyi amewapongeza viongozi wa TANTRADE chini ya Mkurugenzi Mkuu Mtendaji Ratifa Ali Muhammed kwa kutafasiri kwa vitendo farsafa ya Dr Samia na maono yake ya kukuza biashara ya mtu mmoja mmoja au makundi mbalimbali kwa kuweza kufanya ubunifu kwenye maonyesho ya Sabasaba kwa kuweka mifumo ya kujisajili kwaajili ya kupata mabanda na ukataji tiketi kwa njia ya mtandao ambako inasaidia fedha ya serikali kuingia moja kwa moja bila kupitia mikononi mwa watu.
Pia wameweza kukamilisha mpango wa ujenzi wa kiwanja cha kisasa cha maonyesho ya sabasaba .
Uwepo wa ubunifu wa maonyesho wa bidhaa za nchi za kigeni mfano siku China ,Japani huku ni kukuza dipromasia ya Kiuchumi. Rais wa Zanzibar ameiakikishia TANTRADE yeye na rais Samia wataendelea kuwapa ushirikiano wa Ali na mali na serikali ina mikakati mikubwa juu ya TANTRADE.
Rais amezindua Nembo ya Bidhaa za Tanzania ambako hii ni alama ya kutamburisha bidhaa zetu kitaifa na kimataifa amesema haya tarehe 7 mwezi wa 7 2025 ndani ya viwanja vya Sabasaba wilayani temeke jijini dar es salaam wakati alipofungua maonyesho ya sabasaba ya 49.
Habari na Ally Thabit Mbungo.
Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani nchini tanzania amesema matokeo ya Mitihani ya Taifa ya Kidato cha sita yamekuwa yenyekuleta faida na faraja kwa kiasi kikubwa kwa ufahuru kuongezeka ukilinganisha na miaka ya nyuma .Uongozi wa rais Dr Samia awamu hii ya sita ya uongozi wake ameweza kufanya maboresho na mabadiriko kwa kiasi kikubwa kwenye sekta ya elimu kwenye ujenzi wa madarasa ,mabweni ,nyumba za walimu ,kidato cha tano na cha sita awalipi ada haya yote yamepelekea wanafunzi waliofanya mitihani ya taifa ya kidato cha sita ufahuru wao kuongezeka na kuwa mzuri.
Ufahuru wa somo la Hisabati umeongezeka ambako asilimia 73 ukilinganisha na miaka ya nyuma , Walio futiwa matokeo ya kidato cha sita ni wanafunzi 70 kwa sababu za udanganyifu na sababu zinginezo na mmoja kafutiwa matokeo kwa mitihani ya Ualimu na kupelekea jumla ya waliofufiwa matokeo kuwa 71 ambako 70 kidato cha sita na mmoja ni mitihani ya Ualimu.
Haya ametangaza Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani Dr Mohamedi Ally akiwa Zanzibar.
Habari na Ally Thabit
Kijana Mwenye Changamoto ya Kuto Ona Ally Thabit Mbungo ameupongeza Uongozi wa Latra Ccc kwa kuweza kuwajali na kuwazingatia watu wenye ulemavu wa aina zote kwa kuandika majarida kwa kutumia maandishi ya nukta nundu kwaajili ya wasio Ona kama inavyoonekana pichani .Ambako sisi tusio ona tunapata elimu na kujifunza maswala ya Latra Ccc kwa njia raisi na nyepesi bila utegemezi .
Pia Latra Ccc wameweka maandishi makubwa kwenye watu wenye Uoni hafifu vilevile watu wenye Uziwi wanapata elimu kutoka Latra Ccc kupitia Lugha ya Alama.
Ni vyema watu wafike kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Victoria Stanslaus
Huku akiwataka abiria kuakikisha kwenye tiketi zao wanaandikiwa taarifa sahihi mwanzo wa safari yake na mwisho wa safari na jina la mmiliki wa basi liandikwe kwa kilefu ili kuepuka kushushwa eneo ambalo ujakusudiwa na ukipata matatizo iweraisi kupata haki zako kupitia kampuni za bima .
Amesema haya kwenye maonyesho ya 49 ndani ya viwanja vya Sabasaba yanayofanyika wilaya ya temeke jijini Dar es salaam. Habari picha na Victoria Stanslaus.
Ametoa wito kwa wamiliki wa mabasi kutekeleza kwa vitendo kanuni ya kutumia tiketi mtandao na kwa abiria wazingatie matumizi ya tiketi mtandao kwani itaepusha kupandishiwa nauli kiolela olela amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit
Mwalimu Kintu anaefundisha Watu wenye Ulemavu Chuo cha Veta amesema katika kutoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu ya fani mbalimbali Veta Dar es salaam ndio wa kwanza kutoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu.
Na yeye mwenyewe ameweza kijitegemea katika maisha yake anaishukuru Veta Songea kwa kumlejeshea tumaini lake la maisha licha yakuwa mlemavu anawataka wazazi na walezi kutowafungia ndani watu wenye ulemavu hivyo wawapeleke shuleni ama kwenye Vyuo vya Veta huku akiwataka watu wenye ulemavu kutokata tamaa .Wafike kwenye Vyuo vya Veta ili wapate mafunzo ya fani mbalimbali kwani Veta ndio kimbilio la watu wenye ulemavu.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Huku akiwataka watu kutembelea banda la Veta kwenye maonyesho ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit
Lengo wajifunze namna ya watu wenye ulemavu wanavyofanya kazi zao na Veta walivyoludisha tumaini la watu wenye ulemavu katika maisha yao .
Habari picha na Victoria Stanslaus
Ameishukuru Veta kwakuweza kuibua matumaini yake ya maisha yake na kukamilika kwa ndoto zake.
Ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwapeleka watu wenye Ulemavu Veta amesema haya kwenye banda la Veta ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye maonyesho ya 49 Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam.
Habari picha na Victoria Stanslaus
Habari picha na Victoria Stanslaus
Habari picha na Victoria Stanslaus.
Pia Sido imewaandaa wataalam wa kutengeneza majiko ambayo yanatumia mkaa mbadala vilevile Sido wanatengeneza mashine na vipuri vya majiko yote Mali ghafi zake zinatoka hapa nchini tanzania .
Sido wameweza kuwafikia Mama Lishe na Baba Lishe kwa kuwapa elimu na mafunzo namna ya kutumia nishati safi ya kupikia ,Taasisi , kampuni,mashuleni,kwenye kambi za jeshi ,polisi na magerezani Sido imeweza kupeleka majiko yanayotumia nishati safi ya kupikia huku akiwataka watu kutembelea kwenye banda la Sido ili wanunue majiko yanayotumia nishati safi ya kupikia kwenye viwanja vya Sabasaba Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam katika maonyesho ya 49.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo.
Pia PPRA imeandaa majarida yenye maandishi ya nukta nundu kwaajili ya walemavu wasio Ona na vifaa vya kurekodia sauti zana hizi zimewezesha watu wenye ulemavu kupata elimu na uwelewa kuhusu zabuni na tenda zinazotolewa na PPRA vilevile PPRA inatoa elimu kwa watu wote kupitia redio,tv,magazeti,na makongamano pamoja na semina kupitia taasisi za watu wenye ulemavu.
Josefu Muozi amewataka watu kutembelea banda la PPRA viwanja vya sabasaba maonyesho Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam kwenye maonyesho ya 49 habari picha na Victoria Stanslaus.
Denisi Simba amesema PPRA wameweka mazingira rafiki na wezeshi kwa makundi yote ikiwemo wanawake ,vijana,wazee na Watu wenye ulemavu Pia amewataka watu watembelee banda la PPRA kwenye maonyesho ya 49 ya sabasaba yanayofanyika jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Ashim Rungwe Mwenyekiti wa Chama cha Chauma Maarufu Mzee wa Ubwabwa yupo Maututi Mkoani Kilimanjaro Mjini Moshi na kupelekea kulazwa kwenye hospitali ya Kisms hali hii ya ugonjwa imemtokea kwenye zoezi la kukieneza na kukitangaza chama cha Chauma haya yamesemwa na mkuu wa Idara ya chama cha Chauma John Mrema .
Ambae amesema plesha na sukari vimepanda kwa Ashim Rungwe maarufu Mzee wa Ubwabwa.
Habari na Ally Thabit Mbungo
Dr Mustafa amewasilisha Mada ya Namna ya ubunifu utakavyo wasaidia wakulima kulima kilimo chenye tija .
Habari na Ally Thabit Mbungo.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Dr Ana Makakala Kamishina Mkuu wa Uhamiaji nchini tanzania amesema katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu jeshi la Uhamiaji la tanzania limeweka nguvu kubwa mipakani kote kwenye nchi zinazozunguka tanzania kwaajili ya kudhibiti wahamihaji ambao awana vibali vya kuingia tanzania hili kuimarisha ulinzi na usalama wa tanzania kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi.
Dr Ana Makakala amesisitiza kuwa tanzania itaendelea kufanya mikutano yake na nchi za Rwanda, Burundi,Uganda na nchi zinginezo.
Mfano Mkutano wa Drc Kongo na Tanzania ni mwanzo tu wa mikutano mingiyo Dr Ana Makakala ametoa wito kwa watu wanaotaka kuja tanzania wafuate kanuni,miongozo,taratibu na sheria kabla awajaingia tanzania .
Amesema haya jijini dar es salaam
Habari picha na Ally Thabit Mbungo.
Waziri wa Fedha Dr Mwigulu Mchemba amesema bajeti alioiwasirisha bungeni jijini dodoma kiasi cha tilioni56.49 bajeti hii itamalizia miradi mbalimbali ya kimkakati na ile itakayoanzishwa . Bajeti hii fedha nyingi za ndani zitaendesha uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 bila kutegemea mataifa ya nje .
Habari na Ally Thabit Mbungo
Ndg Israel K. Ilunde Mwenyekiti wa Policy Forum(PF) na Mkurugenzi mtendaji wa YPC kutoka Kibaha mkoa wa pwani amesema mifumo ya kodi iliyopo nchini tanzania si rafiki kwa wajasilia Mali na wafanyabiashara wadogo ndio maana watu awatoi ushirikiano pindi TRA wanapowahitaji wafike kwenye ofisi zao na kwenye mamlaka zingine za kikodi.
Na pindi mtu au taasisi ukihitaji uwe mlipa kodi unapofika kwenye ofisi zao unakutana na mambo mengi ya kukukatisha tamaa .
Mwenyekiti na Mkurugenzi ametoa wito kwa serikali na mamlaka za kikodi nchini tanzania zifanye marekebisho kwenye mifumo ya kodi na waweke mazingira rafiki na wezeshi kwa wanaohitaji kulipa kodi ambao ni wapya na wale wanaoendelea kulipa kodi hii itasaidia nchi yetu kukusanya kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa walipa kodi na kuachana na bajeti yetu ya tanzania . Kutegemea fedha za misahada na za waisani kutoka nje ya nchi.
Amesema haya makao makuu ya TGNP eneo la mabibo jijini dar es salaam.
Habari na Ally Thabit Mbungo
Mwanaharakati na Mjumbe wa TGNP Ana amesema serikali ya tanzania iakikishe bajeti wanazozipanga zizingatie usawa wa kijinsia .Kwani bajeti iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha na Dr Mwigulu Mchemba yenye kiasi cha shilingi za kitanzania tilioni 56.49 ,kwa kiasi kikubwa aijazingatia misamaha ya kikodi kwenye taulo za kike,visaidizi vya watu wenye ulemavu na mengineyo.
Ametoa wito kwa Wanaharakati wa tanzania kuendelea kupaza sauti kwa serikali amesema haya makao makuu ya TGNP eneo la mabibo jijini dar es salaam.
Habari na Ally Thabit Mbungo
Mwanaharakati Mkongwe wa TGNP BI Subira ameitaka serikali ya tanzania kabla ya kupanga bajeti ni vyema kuwashirikisha wananchi wote kuanzia ngazi ya kaya ,kitongoji au Mtaa ,Kijiji,Kata,Tarafa,Wilaya,Mkoa na ngazi ya Kitaifa lengo kuwa na bajeti shirikishi .
Hamesema haya Makao Makuu TGNP eneo la mabibo jijini dar es salaam.
Habari na Ally Thabit
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Mulilo Jumanne Mulilo amethibitisha kuwa watu waliompiga na kumjeruhi Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Dkt Charese Kitima wamekatwa na utaratibu wa kufikishwa Mahakamani unafanyika .
Ambako hivi karibuni eneo la Kurasini Makao Makuu ya Baraza la Maaskofu nchini Tanzania majira ya saa nne ya usiku watu hawa walifika eneo hili na kumshambulia Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania.
Habari na Ally Thabit
Anesema haya kwenye mkutano mkuu wa chama cha NLD ambako chama hiki wanachama wake walipomchagua na kumpitisha Doyo Hassan Doyo kuwa ndiye atakayepeperusha bendera ya urais ifikako mwezi wa kumi mwaka huu 1025 kwenye uchaguzi mkuu.
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Kitu ambacho kinamfanya awe na uhakika wa kuwa Raisi kutokana na dira ya chama chake cha NLD ambako kusimamia Kilimo kwa kuwapa wakulima mbegu bora na za kisasa pamoja na kuwatafutia masoko ya kitaifa na kimataifa. Ugawaji wa mbolea na pembeje bule kwa wakulima . Kilimo cha kisasa kupitia umwagiliaji,Usimamizi bora kwenye sekta ya madini ambako atahakikisha kila mchimbaji anapata vifaa vya kisasa vya kuchimbia madini na kuweka bei elekezi, Utoaji wa resen kwa wazawa bila mashariti magumu.
Sekta ya Ajira .
Doyo Hassan Doyo Mgombea kiti cha urais kupitia chama cha NLD atahakikisha kila mtanzania anapata ajira ya kudumu,hatakuza sekta ya viwanda na upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na kuimarisha sekta ya Afya na upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa gharama nafuu.
Vile vile atakuza sekta ya Usafirishaji na Uchukuzi kwenye miundombinu ya majini ,nchikavu na Angani amesema haya baada ya kupewa nafasi ya kupeperusha bendera ya uraisi kupitia chama cha NLD . Hivyo amewataka watanzania wamchague Doyo Hassan Doyo awe rais wa tanzania kupitia chama cha NLD. Kwani ccm walio ahixi hawajatekeleza hata moja .
Habari picha na Ally Thabit Mbungo
Pia miundombinu ya kiafya imezidi kujengwa na kuimarishwa kwa Unguja na Pemba na Madaktali bingwa wapo wa kutosha .
Waziri wa Afya wa Zanzibar anawataka wazanzibar wakate bima za Afya.vilevile ameongeza kwa kusema katika mwaswala ya watu wenye ulemavu zanzibar yanazingatiwa kwa kiasi kikubwa .Mfano Mashuleni kuna miundombinu rafiki na wezeshi kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa aina zote.
Kwa upande wa wanafunzi wasioona kuna maandishi ya nukta nundu pia kwa watu wenye ulemavu wakienda kupata huduma kwenye vituo vya Afya ,Zahanati, Mahospitalini na maeneo mengine wanapewa kipaumbele.
Habari picha na Victoria Stanslaus.
Ndugu Wanahabari Mitihani ya Kidato cha sita ( ACSEE) na Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada imeanza tarehe 05 mei 2025 Tanzania Bara na Zanzibar. Mtihani wa Ualimu utakamilika tarehe 19 Mei,2025 na Kidato cha Sita tarehe 26 Mei,2025. Mtihani wa kidato cha sita utafanyika katika jumla ya shule za secondari 982 na vituo vya watahiniwa wa kujitegemea 245. Aidha , Mtihani wa Ualimu utafanyika katika Vyuo vya Ualimu 68.
USAJILI WA WATAHINIWA
(a) Watahiniwa wa Kidato cha Sita
Jumla ya watahiniwa 134,390 wamesajiliwa kufanya mtihani wa Kidato cha Sita 2025 ambapo watahiniwa wa shule ni 126,957 na Watahiniwa wa Kujitegemea ni 7,433.
Kati ya Watahiniwa wa Shule 126,957 waliosajiliwa, wavulana ni64,581 sawa na asilimia 50.87 na Wasichana ni 62,376 sawa na asilimia 49.13. Aidha watahiniwa wenye mahitaji maalum ni 453 ambapo kati yao weenye Uoni hafifu ni 300, wasioona ni 16, wenye Uziwi 58, wenye ulemavu wa akili ni 04 na wenye ulemavu wa viungo vya mwili ni 75.
Kati ya Watahiniwa wa Kujitegemea 7,433 waliosajiliwa,wavulana 4,782 sawa na asilimia 64.33 na wasichana ni 2,651 sawa na asilimia 35.67. Aidha Watahiniwa wa Kujitegemea wenye mahitaji maalum wako 151 ambapo kati yao wenye uoni hafifu ni142 na wasioona ni 9.
Mwaka 2024 idadi ya watahiniwa wa Shule na Kujitegemea waliosajiliwa walikuwa 113,536. Hivyo, kuna ongezeko la jumla ya watahiniwa 20,854 (18.37) kwa mwaka 2025 ukilinganisha na mwaka 2014.
(b) Mtihani wa Ualimu
Jumla ya watahiniwa 10,895 wamesajiliwa kufanya mtihani wa Ualimu Mei 2025.
Kati ya watahiniwa hawa 3,100 ni wa ngazi ya Stashahada na 7,795 ni wa ngazi ya Cheti.kwa ngazi ya Stashahada, wanaume ni1,751 sawa na asilimia 56.48 na wanawake ni 1,349 sawa na asilimia 43.52. Aidha kwa ngazi ya Cheti watahiniwa 3,987 sawa na asilimia 51.15 ni wanawake .
Watahiniwa wenye Mahitaji Maalum waliosajiliwa kufanya mtihani wa Ualimu 24.Kati yao 2 ni wenye Uoni hafifu kwa ngazi ya Stashahada; na 16 wenye uoni hafifu ,3 wasioona ,1uziwi,1Ulemavu wa viungo ni wa ngazi ya Cheti.
Mwaka 2024 idadi ya Watahiniwa wa Ualimu waliosajiliwa walikuwa 11,435. Hivyo, kuna upungufu wa jumla ya watahiniwa 540 (4.72) kwa mwaka 2025 ukulinganisha na mwaka 2024.
MAANDALIZI YAMEKAMILIKA PAMOJA NA KUSAMBAZWA KWENYE VITUO USIKA PAMOJA NA VITABU VYA KUJIBIA NA NYARAKA ZOTE MUHIMU KWENYE MIKOA YOTE KWA TANZANIA BARA NA ZANZIBAR.
Mitihani wa kidato cha sita ni muhimu kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla kwani upima maarifa .stadi na umahiri wa wanafunzi katika maeneo yote waliojifunza kwa kipindi cha miaka miwili ya elimu ya secondari ya juu. Matokeo ya mtihani huu hutumika katika uchaguzi wa wanafunzi wanaojiunga na Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati katika fani mbalimbali za Utaalaam wa kazi kama vile Afya ,Kilimo,Ualimu,Ufundi na nyinginezo. Hivyo Mtihani huu ni muhimu sana kwa wanafunzi ,Wazazi na Taifa kwa ujumla.kwa upande wa mtihani wa Ualimu,mtihani hufanyika kwa lengo la kupata walimu makini ambao watafundisha katika ngazi ya Elimu ya Msingi na Secondari.
WITO KWA KAMATI ZA MITIHANI,WASIMAMIZI,WAMILIKI WA SHULE NA JAMII
Wito kwa Kamati za Mitihani
Pamoja na Maandalizi yote muhimu yaliyofanyika Kamati za Miitihani za Mikoa na Almashauri ziakikishe kuwa usalama wa Vituo vya Mitihani vinaimarishwa na kwamba Vituo hivyo vinatumika kwa mujibu wa Mwongozo uliotolewa na Baraza la Mitihani la Tanzania .Aidha , Wahaakikishe wasimamizi wote waliopangwa kusimamaia uendeshaji wa mtihani katika kituo husika wanafika kwa wakati katika vituo husika.
WITO KWA WASIMAMIZI
Baraza linatoa wito kwa wasimamizi wote walioteuliwa kusimamia mitihani kufanya kazi yao kwa weledi na uadilifu wa hali ya juu.Wasimamizi wahakikishe kuwa wanazingatia kanuni za mitihani, Tarabu na Miongozo ya Baraza la mitihani waliyopewa ili kila mtahiniwa apate haki yake.
Aidha ,wasimamizi wahakikishe watahiniwa wote wenye mahitajiamaalum wanafanya mitihani yao ipasavyo ili wapate haki zao za msingi.Haki hizo ni pamoja na kuwapa mitihani yenye maandishi ya nukta nundu kwa watahiniwa wasio ona na Maandishi ya kukuza kwa watahiniwa wenye uoni hafifu. Watahiniwa wote wenye mahitaji maalum waongezewe muda wa dakika 20 kwa kila saa kwa somo la Hisabatina dakika 10 kwa kila saa kwa masomo mengine,kama kanuni za mitihanizinavyoelekeza .Wasimamizi wahakikishe watahiniwa wote wanafanya mitihani kwa muda ulio pangwa na katika hali ya utulivu.
WITO KWA WATAHINIWA
Baraza linaamini kuwa walimu na wanafunzi wamewaandaa vizuri katika kipindi cha miaka miwili ya secondari ya juu na kozu ya mafunzo ya Ualimu. Hivyo ni matarajio ya Baraza la mitihani kuwa kila mtahiniwa atafanya mtihani wake kwa kuzingatia kanuni za mitihani.Aida,Baraza halitarajii kuona mtahiniwa yeyote atakayebainika kufanya udanganyifu. Mtahiniwa yeyote atakayebainiwa kufanya udanganyifu kwa Mitihani matokeo yake yatafutwa kwa mujibu wa kanuni za Mitihani.
WITO KWA WAKUU WA SHULE MA WAMILIKI WA SHULE NA VYUO
Baraza linawaasa Wakuu wa Shule na Wakuu wa Vyuo kutekeleza majukumu yao ya usimamizi kwa kuzingatia mwongozo wa usimamizi uliotolewa na Baraza la Mitihani na kuepuka kuingilia usimamizi wa watahiniwa ndani ya vyumba vya mitihani.
Aidha, Baraza linawaasa Wamiliki wa Shule na Vyuo kutambua kuwa shule zao ni vituo maalum vya mitihani na hivyo hawatakiwi kwa namna yoyote kuingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani katika kipindi chote cha ufanyikaji wa mitihani hii. Baraza halitasita kukifuta kituo chochote cha mitihani endapo litajiridhisha pasipo shaka kuwa uwepo wake unahatqrisha usalama wa Mitihani.
WITO KWA JAMII
Baraza linatoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano unaotakiwa katika kuhakikisha Mitihani ya Kidato cha Sita na Ualimu mwaka 2015 inafanyika kwa amani na utulivu. Wananchi wanaombwa kuhakikisha kuwa hakuna mtu yeyote asiyehusika na mitihani anaingia kwenye maeneo ya shule na vyuo katika kipindi chote chamitihani. Kwa kufanya hivyo,tutawawezesha wanafunzi waliosajiliwa kufanya mitihani ya Kidato cha Sita na Ualimu Mei 2025 kwa amani na utulivu.
Haya yanesemwa na Katibu Mtendaji Dkt .Said A. Mohamed.
Habari na Ally Thabit Mbungo
Mkurugenzi Mtendaji Tgnp Liliani Liundi amesema tarehe 19 ya mwezi 3 mwaka 2025 rais Dr Samia ametimiza miaka minne ya uongozi wake kitendo hiki wanaharakati wanaopigania haki za binadamu kwao ni mafanikio makubwa kwani watu wengi waliamini kuwa mwanamke awezi kuiongoza nchi . Kupitia rais Dr Samia zana hii mbaya na potofu dhidi ya mwanamke imeweza kufutwa na kunjwa.
Ndani ya miaka 30 ya Beijing wanawake wamejikomboa kiungozi, ardhi na wameweza kujiamini amesema haya viwanja vya tgnp mabibo katika siku ya mwanamke duniani na uzinduzi wa ripoti ya Beijing.
Habari picha na Victoria Stanslaus
Ujenzi wa viwanda vya sukari na upanuzi wa viwanda vya zamani vya sukari. Prof Keneth Bengesi amesema rais Dr Samia kwa kipindi cha uongozi wake wa miaka minne amekamilisha miradi yote ilioachwa na mtangulizi wake.mfano ujenzi wa bwawa la mwalimu nyerere, daraja la Kigongo busisi mwanza, ujenzi wa SGR, uwanja wa msarato jijini dodoma , amekuza demokrasia kwa kuwa nafasi viongozi wa vyama vya siasa kufanya mikutano yao kwa uhuru, maridhiano kwa kupitia farsafa yake ya R nne na kuwarejesha watu wote waliokimbia nje ya nchi.
Na mengineyo mengi ameyafanya rais Dr Samia ikiwemo kufunguwa fursa kwa wafabiashara, wasanii kwa kusafiri nao nje ya nchi kwaajili ya kuwatafutia masoko ya kitaifa na kimataifa , ameweka mazingira rafiki na wezeshi kwa wawekezaji kuwekeza kwenye sekta ya sukari na maeneo mengineyo.
Ametoa wito kwa watanzania waendelee kumuunga mkono na mwaka huu kwenye uchaguzi wampe kura za kutosha rais Dr Samia ili aendekee kuwa rais wa Tanzania hakika rais Dr Samia mitano tena.
Habari picha na Victoria Stanslaus
Habari picha na Ally Thabit
Mwenyekiti wa Jumuhiya ya Wanawake wa Kiislamu Taifa na Mwana harakati mkongwe amewapongeza TGNP kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kupiga vita ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake , wasichana na makundi mengineyo na kupelekea idadi ya wanawake ya kuwa viongozi nchini tanzania imeongezeka. Mfano wabunge wanawake wa ku haguliwa wapo 26 ukilinganisha na miaka ya nyuma haya ndio walio yapigania kwenye mkutano wa Beijing nchini China mwaka 1995 amesema haya kwenye siku ya mwanamke duniani kwenye viwanja vya TGNP Mabibo jijini dar es salaam.
Habari picha na Ally ThabitPia rais Dr Samia ameanzisha miradi mipya na kukamisha miradi ilioachwa na mtangulizi wake. kupitia sekta ya elimu amejenga madarasa mapya, mabweni, ameajili waalimu, ujenzi wa nyumba za walimu na mabadiliko ya sera ya elimu ambako inamuwezesha mwanafunzi akimaliza elimu yake anaweza kujiajili ama kuajiliŵa.
Vilevile Wakiri Msomi na Mkurugenzi wa Shule za St. Matthew's Dr Peter Tadeo Mtembei amewataka wa'azi na walezi kuwaandikisha watoto wao kwenye shule zote nane za St Matthew's kwani shule zao zinatoa elimu bora nidhamu na usalama ni vitu vya msingi na wanavizingatia na ufahuru wa uhakika na wakiwango cha juu.
Ametoa rai kwa wahitimu 97 wa kidato cha sita kwenye shule ya St. Matthew's iliyopo mkoa wa wa pwani wilaya ya mkuranga kata ya mwandege katika maafari haya ya 20 kwa mwaka 2025 pindi wa wakimaliza mitihani ya taifa wakawe mabalozi wema , waendeleze maadili mema kwa jamii, tabia njema na watumie elimu walioipata kutatuwa changamoto za kijamii.
Pia amewasisitiza wazazi na walezi kwa elimu bora, nidhamu na usalama kwa wanafunzi na gharama nafuu za ada ni vyema wachague shule za St Matthew's kwani kupitia Maendeleo Bank wazazi na walezi watakopeshwa ada kwa riba nafuu ya asilimia moja .
Habari picha na Victoria Stanslaus
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Dr Tito Magoti anawataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kwenye shule za St. Matthew's kwani zinafundisha vizuri mpaka kupelekea mwanafunzi kuweza kujiajili kupitia mafunzo ya ujasilia Mali na kuondokana kuwa tegemezi katika jamii .
Shule za St. Matthew's zinaunga mkono na kutekeleza maono ya rais Dr Samia kwa kuwapa wanafunzi elimu bora na viwango vikubwa hivyo ni vyema wazazi na walezi wasiache kuwapeleka watoto wao kwenye shule za St. Matthew's.
Amesema haya kwenye maafari ya 20 ya kidato cha sita ambako wahitimu 97 wanamaliza elimu yao kwenye shule ya St. Matthew's wilaya ya Mkuranga kata ya mwandege mkoani pwani.
Habari na Ally Thabit
Makamu Mwenyekiti wa Bodi Shule ya St. Matthew's Dr Mwisiga amesema siri kubwa ya mafanikio kwa shule za St Matthew's katika wanafunzi kufahuru kwa kiwango kikubwa ni mazingira ni rafiki na wezeshi ya kufundishia na kujifunza wanafunzi.
Kuwepo kwa mahabara za kutosha na matumizi ya kiteknolojia ya kufundishia na kujisomea .swala la nidhamu, usalama na malezi ni misingi inayosimamiwa na kuzingatiwa kwenye shule zote za St. Matthew's.
Makamu Mwenyekiti wa Shule za St. Matthew's anawataka wazazi na walezi wawpeleke watoto wao kwenye shule za St Matthew's kwani watapata elimu bora na gharama ni nafuu na inalipika kwa hawamu nne lakini pia kupitia Maendeleo Bank watapata mkopo wa ada wenye riba ya asili moja .Makamu Mwenyekiti wa bodi Dr Mwisiga amesema swala la maadili, mafundisho ya dini , tabia njema ni vitu. Vinavyosimamiwa na kuzingatiwa kwa wanafunzi ndio maana ufahuru unaongezeka mwaka hadi mwaka amesema haya kwenye maafari ya 20 ya kidato cha sita kwa wanafunzi wapatao 97 wa shule ya St. Matthew's.
Habari na Ally Thabit
Mkuu wa Shule ya St. Matthew's Josefu Malahila. amewataka Wazazi na walezi kuwahandikisha watoto wao kwenye shule zote nane za St. Matthew's kuanzia elimu ya Awali , msingi kwa Secondary kuanzia kidato cha kwanza mpaka kidato cha sita. Ambako mzazi analipa hada kwa awamu nne.
Shule za St. Matthew's zina malengo ya kutoa elimu inayozingatia nidhamu, usalama kwa wanafunzi na malezi bora kwa wanafunzi wote shule ya St Matthew's inamuwezesha mwanafunzi kujiajili ama kuajiliwa amesema haya kwenye maafari ya kidato cha sita ya wanafunzi wapatao 97 wa shule ya St.Matthew's.
Mkuu wa Shule ya St. Matthew's Josefu Malahila ametoa wito kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita elimu na ujuzi walioupata wakatumie katika kutatuwa changamoto za kijamii.
Habari na Ally Thabit
Balozi Mulamula amewataka Wanawake Kuchangamkia fursa mbalimbali miongoni mwao zikiwemo fursa za kiuchumu ambako wakifanya biashara au ujasilia Mali watafanikiwa kiuchumi .
Pia amewataka wanawake wote wawe na elimu ya fedha amesema haya wakati wa kuwajengea uwezo wanawake na wasichana walipo kutana na Women Shaping the future (SRS) jijini dar es salaam.
Habari na Ally Thabit
Samia 4×4 itagawa vifaa vya kujifungulia wamama wajawazito ambako vifaaa hivyo ni zaidi ya elfu moja ivyo wanawake wote wanatakiwa kujitokeza kwa wingi .
Pia msafara huu utapokelewa na waziri wa maji Awesu Juma Awesu .katika msafara huu kutakuwa na uzinduzi wa miradi mbalimbali iliyotekelezwa na rais Dr samia na kilele cha msafara huu wa Samia 4×4 utafikia tamati tarehe 8 mwezi wa 4 mwaka 2025.
Habari picha na Ally Thabit
Mwenyekiti wa Bodi ya Maendeleo Bank Plc Prof Ulingeta Mbamba Azindua Huduma ya CLICK BANK SMILE amesema uzinduzi wa Internet Banking .
Amechukua fursa ya kuwapongeza kwa dhati Menejimenti na wafanyakazi wa Maendeleo bank kwa juhudi kubwa walizofanya kuhakikisha huduma hii mpya ya inakamilika na kuzinduliwa kwa mafanikio.jitohada,maarifa,na kujituma kwao kumeifanya Maendeleo bank kuwa kinara wa ubunifu katika sekta ya kifedha amewaponeza sana .
Katika Ulimwenngu wa sasa wa kidigitali,benkiinayoendelea ni ile inayokwenda sambamba na teknolojia- Click Bank Smile ni jibu sahihi kwa mahitaji yawateja wa leo wanaotaka huduma za haraka ,salama na zinazoweza kupatikana mahali popote na muda wowote .
Hivyo Matarajio ya huduma hii itaongeza ufanisi wa biashara, hasa kwa wafannyabiashaara wadogo na wa kati na kuokoa muda na gharama za wateja kwa kila kitu kinapatikana kwa mfuso wa kidole kwenye simu au kompyuta.
Huu ni ushahidi kwa Maendeleo Bank Plc inatekeleza kwa vitendo mkakati wake wa ukuaji wa kidigitali na kufanikisha azma ya kuwa benki ya kisasa inayoendana na mabadiliko ya kiteknolojia.
Kwa Mujibu wa Fin-Scope Survey ya Mwaka 2023 kiwango cha upatikanaji na matumizi ya huduma rasmi za kifedha kiliongezeka hadi 89% na 76% mwaka 2023 kutoka 86% na 65% mwaka 2017". Hii ilichangiwa sana na uimarikaji wa huduma za kifedha kwa njia ya kidigitali na hasa huduma za kifedha kwa njia ya simu.
Hivyo ni Imani kuwa huduma hii ya Internet banking si tu kwamba itawanufaisha wateja wa Maendeleo Bank tu bali pia itasaidia ukuaji wa uchumi wa wananchi kwa kuongeza ujumuishi wa kifedha nchini. Kwa namna hii, Maendeleo Bank inachangia moja kwa moja katika malengo ya serikali , katika kuimarisha uchumi wa kidigitali na kuhakikisha wananchi wengi wanapata huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.
Pia ametoa wito kwa watanzania wote kutumia huduma hii ya CLICK BANK SMILE ili kujionea urahisi wake na manufaa yake .Hii ni huduma iliyoandaliwa kwa ajili yenu hivyo ni jukumu letu kuitumia kwa tija .
Kwa heshima na taadhima ,sasa ameitangaza rasmi kuwa huduma ya Internet banking ya Maendeleo Bank Plc -CLICK BANK SMILE- imezinduliwa rasmi, leo tarehe 18 mwezi wa tatu mwaka 2025 .PONGEZI KWA MAENDELEO BANK PLC!.
Habari na Ally Thabit
Habari picha na Victoria Stanslaus
Habari picha na Victoria Stanslaus
Amoll Abudi Juma Mjumbe wa Almashauri Kuu ya ccm taifa mkoa wa dar es salaam amempongeza bi Aisha Sururu kwa kuendesha mashindano ya quran kwa miaka ishilini na tano pamoja na kuwahifazisha maneno ya mungu watoto yatima,wajane,wasiojiweza,watu wa makundi maalum kwani kufanya hivi kunasaidia kupata watu wenye maadili,wenye ofu ya mungu na hatimae nchi ya tanzania inapata amani ,upendo na utulivu.
Sheikh Issa Ponda amewataka Waislamu wote wale ambao awana matatizo ya kiafya waweze kutekeleza nguzo ya nne ya kiislam kati ya tano wafunge ramadhani ndani ya mwezi huu wa ramadhani kwani watakuwa waja wema pia wasome Quran mara kwa mara.
Habari na Victoria StanslausKatibu Mkuu wa Baraza Kuu la Ulamaa Bakwata amewataka waislamu nchini tanzania wafunge ramadhani kwenye mwezi huu mtukufu wa ramadhani kwani miongoni mwa faida watakazozipata ni kuimarika kwa afya zao .Pia mungu atawasamehe makosa yao na zambi zao pia anawasisitiza watanzania wote bila jujali dini,kabila,rangi na jinsia wazidi kumuombea afya njema rais Dr Samia kwani amekalisha miradi yote na anatenda haki kwa kila mmoja hivyo ni vyema kumchagua kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu hakika mama samia mitano tena.
Habari picha na Ally Thabit.