Sunday, 13 July 2025

PICHANI BIDHAA ZA NISHATI SAFI YA KUPIKIA


 Kama inavyoonekana Pichani Jiko linalotumia mkaa mbadala  pamoja na mkaa wennyewe mbadala kwenye viwanja vya sabasaba  maonyesho  jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

TIRDO YAJA NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA


 Devid Langa Afisa Uhusiano  na Mawasiliano TIRDO  amesema wanatebgeneza na kupima majiko yanayotumia nishati mbadala vile vile TIRDO  inatoa mafunzo ya namna ya kutengeneza mkaa mbadala .,Mkaa huu auchafui mazingira kwani nishati yake ya kupikia ni safi na salama .

TIRDO imetoa mafunzo kwenye mikoa 12 juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia pia  kwa upande mwingine TIRDO  inatoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu wa aina zote  na kuwafanyia hatamizi amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yaliofanyika jijini dar es salaam .

Habari picha na Victoria Stanslaus 

WAZIRI MKUU ASIFU NA KUPONGEZA MAONYESHO YA SABASABA YA 49

 Majaliwa Kasimu Majaliwa  Waziri Mkuu wa Tanzania amesema maonyesho ya Sabasaba ya 49 ambayo yamefanyika  wilayani temeke jijini dar es salaam  yamekuwa yenye tija kwa Wajasiliamali,Wafanya biashara wadogo ,Wakati na Wakubwa kwani wameweza kutangaza bidhaa zao kitaifa na kimataifa pia wamepata masoko ndani ya nchi na nje ya nchi.

Waziri  Mkuu  Kasimu Majaliwa  amesema sekta ya utalii imetangazwa vyema kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 na yamepelekea kuvutia walii kuja kutaliina kuwekeza ,vile vile ameupongeza uongozi wa TANTRADE  chini ya Mkurugenzi Mkuu  Bi Latifa kwa ubunifu wake kwa kuyafanya maonyesho ya Sabasaba ya 49 kwa njia ya kidigitali .

Bi Latifa Muhamed  amepongezwa na Waziri  Mkuu  Majaliwa kasimu Majaliwa  Waziri Mkuu  wa tanzania kwa kuweka mifumo imala ya kiteknolojia kwa waombaji maeneo ya kufanyia biashara zao na kununua tiketi kwa njia ya mtandao  amesema haya wakati akifunga maonyesho ya Sabasaba ya 49 yaliofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam  kuanzia tarehe 28 mwezi6 2025 na hatimae yamefungwa na Waziri Mkuu  Kasimu Majaliwa  tarehe 13 mwezi 7 mwaka 2025. 

Habari na Ally Thabit Mbungo 

TBA YAJA NA MIKAKATI MIZITO


  Martin Sayeli Afisa Mipango Idara ya Milki Wakala wa Majengo Nchini Tanzania (TBA) wanatekeleza kwa vitendo miradi yote ya ujenzi wa nyumba za serikali ambako nyumba hizi wanauziwa na kupangishiwa watumishi wa serikali na watu binausi .

TBA inajenga nyumba rafiki na wezeshi kwa makundi yote kwa watumishi wa serikali wanapangishwa nyumba kwa kiasi cha shiringi milioni moja  nawasio wa serikali milioni moja na laki tano . TBA  wameweka vutasa janja kwenye milango lengo ni kukabiliana na kuwadhibiti wapangaji ambao awalipi kodi.

Amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es. 

Habari picha na Victoria Stanslaus. 

PICHANI BIDHAA ZA KAMPUNI YA TANFOAM

 

Kama Inavyoonekana Kitanda .Mito, Taulo ,Mito ya duara na Vishikizia miguu vyote vinapatikana kwenye TANFOAM  LIMITED  vilevile TANFOAM wana vitanda pamoja na magodoro ambayo ni rafiki kwa watu wenye changamoto ya uti wa mgongo .

Hivi vyote vinapatikana ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye banda la Karume kwenye maonyesho ya  Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam. Pia wanapatikana kwa mawakala wao waliopo nchi nzima tanzania na kwenye maduka yao yote.

Habari picha na Ally Thabit 

TANFOAM YAJA KIVINGINE KWEMBE MAONYESHO YA SABASABA YA 49

 

Daniel Philipo Marko Afisa Mauzo wa Kampuni ya Tonfoam amesema kwenye maonyesho  ya Sabasaba  ya 49  kampuni yao imeleta bidhaa zenye ubora na zenye gharama nafuu kwa wateja wa jumla na lejaleja . Miongoni mwa bidhaa ambazo wamezileta kampuni ya  Tanfoam Magodoro,Vitanda,Taulo, Mito na Mashuka .

Afisa Mauzo amesema kulingana na msimu huu wa Sabasaba  kuna punguzo la bidhaa zao kwa asilimia 10  kuanzia tarehe 1 mwezi wa 7 2025 mpaka tarehè 31 mwezi wa 7 mwaka 2025.Kampuni hii ya Tanfoam ina miaka 55 tangu kuanzishwa ,Pia ina maduka yao binausi mfano Masaki,Vingunguti,Tegeta na ina mawakqla tanzania nzima  kanda ya Magharibi ,Nyanda za juu kusini,Kanda ya kaskazini,Kanda ya kati ,Kanda ya kati  na kanda ya Mashariki.

Licha Tanfoam  kufanya biashara vilevile inatoa fursa kwa watu kwa kuwaajili ama kujiajili wenyewe kwa kuwapa bidhaa zao kwa makubaliano ivyo ametoa rai kwa vijana na watu wengineo kutumia kampuni ya Tanfoam  ili wajikwamuwe kiuchumi na amewataka kutembelea viwanja vya Sabasaba kwenye  banda la Karume watakutana na watoa huduma wa kampuni ya  TANFOAM  ambako watawahudumia kwa uraisi.

Ametoa wito kwa watu kutumia bidhaa za  Tanfoam  kwani zina ubora amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 ndani ya viwanja vya Sabasaba  wilayani  temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo. 

Saturday, 12 July 2025

PICHANI NI KAHAWA AINA YA ARABICA INAYOPATIKANA KWENYE CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHA MKOANI MARA WAMACU LIMITED


 Chama Kikuu cha Ushirika kutoka Mkoani MARA WAMACU COOPERATIVE UNION  LMT kama inavyoonekana pichani hii ni kahawa aina ya Arabica inayouzwa kwa bei rafiki kwa kila mtu. Hivyo ni vyema watu wafike ndani ya viwanja vya Sabasaba  kwenye maonyesho ya 49 kwenye banda la Wizara ya Kilimo wanunue kahawa hii aina ya Arabica kutoka mkoani mara .

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA KUTOKA MKOANI MARA WAMACU LIMITED CHAFICHUA SIRI NZITO KWENYE MAONYESHO YA SABASABA YA 49


 Olais Piniel Meneja Shughuri wa Chama Kikuu cha Ushirika kutoka Mkoani MARA WAMACU LIMITED   amesema ni muhimu watu kutumia kahawa aina ya Arabica  kwani miongoni mwa siri zilizojificha kuasaidia mtu kutopata kisukari steji ya pili ,kansa steji ya oili,kulinda maungio ya mguu,kibofu cha mkojo kutopata matatizo , kulinda Figo kutopata na magonjwa, na  inapunguza unene uliokithiri.

Ivyoamesema bei zao ni rafiki na nafuu kwa wateja wao na pia kahawa inawawezesha watu kupata ajira amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

CHAMA CHA USHIRIKA CHA MARA COOPERATIVE UNION WAMACU LIMITED YAJITANGAZA KWENYE MAONYESHO YA SABASABA YA 49 JIJINI DAR ES SALAAM


 Alfred Msajigwa Afisa Tehama Chama Kikuu cha Ushirika kutoka Mkoani MARA WAMACU LIMITED  amesema wao ni mara  ya kwanza kushiriki kwenye maonyesho ya Sabasaba  yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam  licha ya ugeni wao wamepata faida ya kujitangaza na kupata masoko ya kitaifa na kimataifa  ambako nchi ya Bulgaria,Ukraine  na Rashia. 

Kahawa yao aina ya Arabika ina ubora ivyo wanawataka watanzania na wasio watanzania kutumia kahawa yao aina ya Arabika . Chama kikuu cha Wakulima Mkoani MARA WAMACU LIMITED  itafanya ka'i ya kufungua masoko jijini dar es salaam  na mikoa mingine kwaajili ya kuwafikia wateja wao amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 kwenye banda la Wizara ya Kilimo .

Habari picha na Ally Thabit 

Friday, 11 July 2025

MAMLAKA YA AFYA YA MIMEA NA VIWATILIFU TANZANIA YAMPONGEZA RAIS SAMIA


 Dr Mujuni Kabululu Kaimu Mkuu Kitengo cha Kuifadhi Nasaba za Mimea Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viwatilifu Tanzania  amempongeza rais Dr Samia  kwa kuweza kununua ndege kwaajili ya kupambana na kuwadhibiti Viwavijeshi,Kweleakwelea na Nzige .

Ndege hii imekuwa mkombozi kwa wakulima ambao mazao yao yalikuwa yanaaribiwa na  vivamizi  hata ivyo serikali itaepukana na gharama ya kukodi ndege nchi za nje kwaajili ya kudhibiti kwelea Kwelea,Viwa vijashi , Nzige na Panya .

Dr Mujuni amesema Mamlaka yao inatoa vibali vya kuingiza na kupeleka nje ya nchi mazao vilevile Mamlaka  hii inatoa vibali vya kuingiza viwatilifu na kusambaza teknolojia  kwa wakulima na wanatoa elimu kupitia Almashauri  kwa wakulima namna ya kutumia viwatilifu kwenye mazao yao .

Pia wanatumia redio,TV,Vipeperushi  na Mafunzo mbalimbali kwa wakulima anawataka watu wote kufika  kwenye banda la Wizara ya Kilimo na kutembelea Mamlaka  ya Afya ya Mimea na Viwatilifu Tanzania  ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye maonyesho ya 49 yanayofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 

TARI YAJA NA MUAROBAINI KWA WAKULIMA


 Dr Filson Kagimbo Mkurugenzi Mkuu wa TARI  Kigoma amesema wakulima wengi walikuwa wanakumbwa na changamoto za kulima bila tija ivyo Taasisi ya Kilimo Tanzania TARI  imeamuwa kufanya tafiti na kuwapelekea teknolojia wakulima.

Moja ya majukumu ya TARI  kufanya utafiti wa Afya ya Udongo,Utafiti wa mazao na Ugunduzi wa mbegu bora,Kulinda mazao yasishambuliwe na wadudu pamoja na magonjwa mbalimbali, Namna ya kuongeza thamani kwenye mazao na kutunza pia wanawafundisha na kufanya utafiti wa za kuifadhi na kusindika mazao pamoja na kuwapelekea teknolojia mbalimbali.

Amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 wilayani temeke jijini dar es salaam  kwenye  banda la TARI. 

Habari picha na Ally Thabit 

TAWA YAVUTIWA NA MWITIKIO WA WATU VIWANJA VYA SABASABA


 Zuwena Kikoti Muifadhi  Mkuu wa TAWA amesema kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika jijini dar es salaam  wilayani temeke Tawa wamevutiwa kwa kiasi kikubwa kwa watu kujitokeza kwa wingi kuona wanyama .

Maombi ya watu kutaka kuwepo kwa Tembo na Twiga watafanyia kazi kutokana na mazingira ya Ikolojia  hata ivyo amewataka watu kufika eneo la Pande lililopo Bunju ambako kuna hifadhi ya wanyamapori ambako kiingilio elfu 11800 .

Habari picha na Victoria Stanslaus 

CHUO KIKUU CHA CBE CHAWAFIKIA WAKULIMA KIDIGITALI


 Martin Alfred Lwafu ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha CBE kwa ngazi ya Diploma ICT amesema wakulima nchini tanzania wanapata changamoto nyingi sana katika kuuza mazao yao kwa njia ya MNADA ivyo ameamua kuja na mfumo wa Tehama ambao utamuwezesha mkulima kuuza mazao yake kupitia njia ya kidigitali  ambako mkulima anaweza kutumia simu janja au kompyuta mpakato .

Kama inavyoonekana pichani mazao ya Mpunga na Korosho amesema haya ndani ya viwanja vya Sabasaba  kwenye  banda  la CBE kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA CBE KUTATUA SIDA YA MAEGESHO YA MAGARI


 Petero ni Mwanafunzi wa Ngazi ya Diploma Mwaka wa pili Chuo Kikuu cha CBE  ICT amebuni mfumo ambao utatumika kutatua matatizo ya maegesho ya magari Mfumo huu utamwezesha mtu kutambua maegesho ya magari kama yamejaa ama ayajajaa kupitia simu janja au kompyuta mpakato  miongoni mwa faida zitakazo patikana kupitia mfumo huu serikali itakusanya pesa yake kwa wepesi , kuepuka usumbufu  kwa wenye magari na kunusuru upoteaji wa mafuta .

Petro  amewaakikishia watu kuwa mfumo huu ni salama huku akitoa wito watu wajiunge na Chuo Kikuu cha CBE  amesema haya ndani ya banda la CBE lililopo kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 wilaya ya temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 


CHUO KIKUU CHA CBE CHAWATAKA WATU KUCHANGAMKIA FURSA


 Afisa wa Chuo Kikuu cha CBE Jakrene E Kaaya anawataka watu kujiunga na Chuo cha CBE ambako chuo Kikuu hichi kina matawi Dodoma,Mbeya,Arusha na Dar es salaam ambako mtu anaweza kujisajili na kujiunga na matawi ya chuo Kikuu cha  CBE  kwenye maeneo yalio tajwa , Viwango mbalimbali vya elimu vinatolewa kwa ngazi ya Cheti, Diploma ,Digree,Master na PHD vilevile Kozi ya ICT inatolewa kwa ngazi zote Ambako inawezesha watu kuendana na teknolojia za kisasa.

Kozi hizi zinatolewa Asubuhi mpaka jioha  nawengine  wanaingia joini mpaka usiku  Pia Chuokikuu  cha CBE wanatoa kozi za muda mfupi mfano . Wanashirikiana na Latra kwaajili ya kutoa mafunzo kwa watoa huduma kwenye mabasi na madereva  wa bodaboda .

Bi jakrene E Kaaya   anawataka watu kutembelea  banda la CBE ili waweze kujisajili kwaajili ya kupata elimu  Chuokikuu  cha CBE ambako chuo hiki kina miaka 60 amesma haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 wilaya ya temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

Wednesday, 9 July 2025

TANTRADE MPYA NA YENYE UBUNIFU YANG'ARA KITAIFA NA KIMATAIFA


 Mkurugenzi Mkuu Mtendaji  wa TANTRADE  Latifa Muhamed amesma ubunifu alioufanya na maboresho alioyafanya ndani ya TANTRADE yamepelekea TANTRADE  kuwa mpya na ya kisasa ndio maana inang'ara kitaifa na kimataifa na kupelekea wafabiashara na wawekezaji kuchangamkia fursa mbalimbali.

Mkurugenzi  ZLatifa Muhamed amesema ameamuwa kuweka mifumo ya Tehama  kwa watu wanaoitaji huduma za TANTRADE  na ukataji wa tiketi kwa njia ya Kieletronik Lengo fedha ya serikali iingie moja kwa moja serikalini  hili kusiwe na ubadhirifu na zisipotee na hili TANTRADE imefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Vilevile TANTRADE imefungua matawi Mwanza ,Arusha,Mbeya,Dodoma na Zanzibar  Lengo kuwafikia wateja kwa uraisi. TANTRADE ndani ya viwanja vya Sabasaba kutajengwa majengo ya kisasa ambako magari yatakuwa na sehemu ya kupaki,Sehemu ya watoto kucheza na biashara zitakuwa zinafanyika wakati wote.

Latifa Muhamed anatekeleza kwa vitendo farsafa na maono ya rais Dr Samia  na huku akimpongeza rais Dr Samia  kwa kuiwezesha TANTRADE kufanya mabadiriko amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam .

Habari picha na Victoria Stanslaus 


Tuesday, 8 July 2025

TUME YA MADINI YAWAFIKIA WATU WENYE ULEMAVU

 

Meneja Mahusiano na Mawasiliano Tume ya Madini Greyson amesema tume ya madini nchini tanzania imewafikia na itaendelea kuwafikia watu wenye ulemavu wa aina zote pia tume ya madini imefungua masoko 43 na vituo vya  ununuzi wa madini kwa  tanzania  109 Lengo la serikali kufanya hivi ni kutoa usumbufu kwa wauzaji na wanunuzi wa madini.

Vilevile tume ya madini  inapanga na kusimamia bei elekezi za madini ambako kauli mbiu inasema Madini ni Maisha na Utajiri amesema haya kwenye maonyesho ya Sabasaba  ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam .
Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

TUME YA MADINI YAWAITA WATU KUWEKEZA


 Afisa wa Leseni Tume ya Madini  Egera Doto amewataka  Watu  ususani watanzania kuchangamkia fursa za kuwekeza kwenye sekta ya madini , Ambako tume ya madini imeweka mazingira rafiki na wezeshi kwa mtu ama kikundi cha watu anaehitaji kuwekeza kwenye sekta hii.

Leseni mbalimbali tume ya madini  inatoa miongoni mwao ni Leseni ya Utafiti wa Madini,Leseni ya uchimbaji wa madini , Uchenjuaji madini, Usafishaji wa madini na zinginezo ambako tume ya madini inatoa Leseni  kupitia mifumo ya Tehama Lengo kuondoa urasimu na kuarakisha kupatikana kwa muda mfupi ambako ndani ya mwezi mmoja unapata Leseni. 

Egera Doto amewataka watu kufika kwenye banda la tume ya madini ndani ya viwanja vya maonyesho  ya Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

Monday, 7 July 2025

RAIS WA ZANZIBAR AVUTIWA NA UONGOZI WA TANTRADE

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti  wa Baraza la Wawakirishi Zanzibar Dr Hoseni Mwinyi amewapongeza viongozi wa TANTRADE chini ya Mkurugenzi Mkuu Mtendaji  Ratifa Ali Muhammed kwa kutafasiri kwa vitendo farsafa ya Dr Samia  na maono yake ya kukuza biashara ya mtu mmoja mmoja   au makundi mbalimbali kwa kuweza kufanya ubunifu kwenye  maonyesho ya Sabasaba  kwa kuweka mifumo ya kujisajili kwaajili ya kupata mabanda na ukataji tiketi kwa njia ya mtandao ambako inasaidia fedha ya serikali kuingia moja kwa moja bila kupitia mikononi mwa watu.

Pia wameweza kukamilisha mpango wa ujenzi wa kiwanja cha kisasa cha maonyesho ya sabasaba .

Uwepo wa ubunifu wa maonyesho wa bidhaa za nchi za kigeni mfano siku China ,Japani huku ni kukuza dipromasia  ya Kiuchumi. Rais wa Zanzibar ameiakikishia TANTRADE yeye na rais Samia wataendelea kuwapa ushirikiano wa Ali na mali na serikali ina mikakati mikubwa juu ya TANTRADE. 

Rais amezindua Nembo ya Bidhaa za Tanzania  ambako hii ni alama ya kutamburisha bidhaa zetu kitaifa na kimataifa amesema haya tarehe 7 mwezi wa 7 2025 ndani ya viwanja vya Sabasaba wilayani temeke jijini dar es salaam  wakati alipofungua maonyesho ya sabasaba  ya 49.

Habari na Ally Thabit Mbungo. 

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA AWAMU YA SITA YAVUNJA REKODI NA KUTIA FOLA

 Katibu Mkuu wa  Baraza  la Mitihani  nchini tanzania amesema matokeo ya Mitihani ya Taifa ya Kidato cha sita yamekuwa yenyekuleta faida na faraja kwa kiasi kikubwa kwa ufahuru kuongezeka ukilinganisha na miaka ya nyuma  .Uongozi wa rais Dr Samia awamu hii ya sita ya uongozi wake ameweza kufanya maboresho na mabadiriko kwa kiasi kikubwa kwenye sekta ya elimu kwenye ujenzi wa madarasa ,mabweni ,nyumba za walimu ,kidato cha tano na cha sita awalipi ada haya yote yamepelekea wanafunzi waliofanya mitihani ya taifa ya kidato cha sita ufahuru wao kuongezeka na kuwa mzuri.

Ufahuru wa somo la Hisabati umeongezeka ambako asilimia 73 ukilinganisha na miaka ya nyuma , Walio futiwa matokeo ya kidato cha sita ni wanafunzi 70 kwa sababu za udanganyifu na sababu zinginezo na mmoja kafutiwa matokeo kwa mitihani ya Ualimu na kupelekea jumla ya waliofufiwa matokeo  kuwa 71 ambako 70 kidato cha sita na  mmoja ni mitihani ya Ualimu.

Haya ametangaza Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani Dr Mohamedi Ally akiwa Zanzibar. 

Habari na Ally Thabit 

WATU WENYE ULEMAVU YAWAPA TANO LATRA CCC

 

Kijana Mwenye Changamoto ya Kuto Ona Ally Thabit Mbungo  ameupongeza Uongozi wa Latra Ccc kwa kuweza kuwajali na kuwazingatia watu wenye ulemavu  wa aina zote kwa kuandika majarida kwa kutumia maandishi ya nukta nundu kwaajili ya wasio Ona kama inavyoonekana pichani .Ambako sisi tusio ona tunapata elimu na kujifunza maswala ya Latra Ccc kwa njia raisi na nyepesi bila utegemezi .

Pia Latra Ccc wameweka maandishi makubwa kwenye watu wenye Uoni hafifu vilevile  watu wenye Uziwi wanapata elimu kutoka Latra Ccc kupitia Lugha ya Alama.

Ni vyema watu wafike kwenye maonyesho  ya Sabasaba  ya 49 yanayofanyika wilayani temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

LATRA CCC YAWAFIKIA WATU WENYE MAHITAJI MAALUM


 Kama inavyoonekana Pichani Katibu Mkuu Mtendaji wa Latra Ccc  Daud Daud akimkabidhi kijana mwenyechangamoto ya kuto Ona kitabu cha maandishi ya nukta nundu ambacho wanatumia watu wasio ona kwaajili ya kupata taarifa za huduma zinazotolewa na Latra ccc  ambako Katibu Mkuu Mtendaji  amesema Latra ccc inatoa elimu kwa makundi yote .

Huku akiwataka abiria kuakikisha kwenye tiketi zao wanaandikiwa taarifa sahihi mwanzo wa safari yake na mwisho wa safari na jina la mmiliki wa basi liandikwe kwa kilefu ili kuepuka kushushwa eneo ambalo ujakusudiwa na ukipata matatizo iweraisi kupata haki zako kupitia kampuni za bima .

Amesema haya kwenye  maonyesho ya 49 ndani ya  viwanja vya Sabasaba yanayofanyika wilaya ya temeke jijini Dar es salaam. Habari picha na Victoria Stanslaus. 

LATRA CCC YATOA SIRI NZITO TIKETI MTANDAO


 Katibu Mkuu Mtendaji wa Latra Ccc Daud Daud ameeleza faida za kutumia Tiketi Mtandao ambako kwa wamiliki wa mabasi inawasaidia kwa kiasi kikubwa kupata taarifa sahihi za watu waliopanda kwenye mabasi yao  Pia pesa wanakusanya kwa wakati kwa upande wa abiria  wanaepukana na usumbufu wa kuuziwa tiketi mala mbili mbili.

Ametoa wito kwa wamiliki wa mabasi kutekeleza kwa vitendo kanuni ya kutumia tiketi mtandao na kwa abiria wazingatie matumizi ya tiketi mtandao kwani itaepusha kupandishiwa nauli kiolela olela amesema haya kwenye maonyesho ya  Sabasaba ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 

MWALIMU KINTU AELEZA MAGUMU VETA WALIOPITIA KWA WATU WENYE ULEMAVU

 

Mwalimu Kintu  anaefundisha Watu wenye Ulemavu  Chuo cha Veta amesema katika kutoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu  ya fani mbalimbali Veta Dar es salaam  ndio wa kwanza kutoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu. 

Mwalimu Kintu amesema iliwachukuwa miaka saba kufanya ushawishi kwa Vyuo  vya Veta  mikoa ya tanzania kuwapokea na kuwafundisha watu wenye ulemavu  ambako kwa sasa amejawa na furaha kwa kuona mafunzo ya fani mbali mbali yanatolewa kwenye Vyuo vya Veta  vyote nchini kwa watu wenye ulemavu wa aina zote.

Mwalimu Kintu amesema kuwepo kwa sera inayowatambua watu wenye ulemavu  kuwa na wao wana haki ya kupata mafunzo kupitia Veta ni jambo zuri. 
Habari picha na Ally Thabit. 

VETA YAJA KIVINGINE KWA WATU WENYE UREMAVU


 Gonsalva Lungu ni Msichana Mwenye Ulemavu wa viungo ambae amehitimu mafunzo ya Ushonaji Chuo cha Veta Songea ndani ya miaka miwili ambako amefungua ofisi ya ushonaji songea mjini eneo la mshangano Licha ya kuwa mlemavu kwenye ofisi yake ameweza kuajili watu wawili ambao awana ulemavu na kuwalipa posho kila mwezi.

Na yeye mwenyewe ameweza kijitegemea katika maisha yake anaishukuru Veta Songea kwa kumlejeshea tumaini lake la maisha licha yakuwa mlemavu anawataka wazazi na walezi kutowafungia ndani watu  wenye ulemavu  hivyo wawapeleke shuleni ama kwenye Vyuo vya Veta huku akiwataka watu wenye ulemavu  kutokata tamaa  .Wafike kwenye Vyuo vya Veta ili wapate mafunzo ya fani mbalimbali kwani Veta ndio kimbilio la watu wenye ulemavu. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 


VETA SONGEA YAMUIBUA MTU MWENYE ULEMAVU


Riziki Stefano Ndumba ni Kijana mwenye ulemavu wa viungo ameipongeza na kuishukuru Veta Songea kwakuweza kumpa mafunzo ya kushona nguo ambako 2020 aliweza kupata mafunzo haya na kuweza kuhitimu kwa miaka miwili  ambako mafunzo haya yamemuwezesha kuingiza pesa . Hivyo anawataka watu wenye ulemavu kufika kwenye Vyuo vya Veta popote walipo hapa tanzania hili waweze kupata fani ambako itawasaidia kutokuwa wategemezi katika maisha yao .

Huku akiwataka watu kutembelea  banda la Veta kwenye maonyesho ya 49 yanayofanyika wilaya ya temeke jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 

PICHANI NAMNA YA JOSEPH JOACHIM MTEI


Kama inavyoonekana  Pichani Kijana  Joseph Joachim  Mtei hii ndio njia ambayo anatumia kuchora ramani za majengo ambako chuo cha Veta  Dodoma  ilivyoweza kumpa mbinu ya kuchora ramani kupitia miguu yake, Joseph Joachim Mtei anawataka watu watembelee kwenye banda la Veta ndani ya viwanja  vya Sabasaba kwenye maonyesho  ya 49 jijini dar es salaam. 

Lengo wajifunze namna  ya watu wenye ulemavu  wanavyofanya kazi zao na Veta walivyoludisha tumaini la watu wenye ulemavu  katika maisha yao .

Habari picha na Victoria Stanslaus 

VETA YAIBUA VIPAJI VYA WATU WENYE ULEMAVU


Joseph Johachim Mtei  ni Kijana  Mwenye  Ulemavu  wa Viungo ambae Veta imempa  Mafunzo ya Uchoraji wa Ramani mafunzo haya anapata mkoani Dodoma, Joseph amesema lengo lake anataka awe Mwandisi wa kucora ramani za majengo Licha yakuwa na changamoto ya mikono Joseph  ndoto zake na ndoto zake zimeweza kuibuliwa na Chuo cha Veta Dodoma ambako anachora ramani za majengo kupitia Miguu.

Ameishukuru Veta kwakuweza kuibua matumaini yake ya maisha yake na kukamilika kwa ndoto zake. 

Ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwapeleka watu wenye Ulemavu Veta amesema haya kwenye  banda la Veta  ndani ya viwanja  vya Sabasaba kwenye maonyesho ya 49 Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

Saturday, 5 July 2025

SIDO YAPONGEZWA KWA MKAA MBADALQ


Bi Fatma ameipongeza Sido na Kuishukuru kwa kuweza kumpa mafunzo ya kutengeneza Mkaa Mbadala ambao auchafui mazingira na gharama yake nafuu .Bi Fatma anawataka watu wote nchini tanzania watumie mkaa mbadala kwani ni nishati safi na salama kwa kupikia na ambayo aichafui mazingira Pia aina madhara kwenye mwili wa binadamu, Bi Fatma ametoa wito kwa watu wote kufika kwenye banda la Sido kununua mkaa mbadala kwani ni nishati safi ya kupikia na inapatikana ndani ya viwanja vya Sabasaba kwenye maonyesho  ya 49 yanayofanyika jijini Dar es salaam. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

PICHANI NI MAJIKO YA NISHATI MBADALA YANAYOPATIKANA KWENYE BANDA LA SIDO VIWANJA VYA SABASABA


Hama hakika  haya ni majiko yenye ubora na imara yanayotengenezwa na Sido ambayo yanatumia nishati safi ya kupikia  hivyo ni vyema watu wote kufika kwenye banda la Sido kwenye  viwanja vya Maonyesho ya sabasaba  ambako maonyesho haya ni ya 49 yanayofanyika Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam. 

Habari picha na Victoria Stanslaus. 

SIDO YAUNGA MKONO MATUMIZI YA NISHATI SAFI


 Afisa Masoko Mwandamizi Sido Makao Makuu Christopha Eduwadi Mwakyusa amesema katika kuunga mkono juhudi na jitihada za Dr Samia  ifikapo mwaka 2030 watu wote nchini tanzania watumie nishati safi ya kupikia  ambako upande wao Sido wanatoa mafunzo ya kutengeneza mkaa mbadala Mkaa huu auchafuhi mazingira . 

Pia Sido imewaandaa wataalam wa kutengeneza majiko ambayo yanatumia mkaa mbadala vilevile Sido wanatengeneza mashine na vipuri vya majiko yote Mali ghafi zake zinatoka hapa nchini tanzania .

Sido wameweza kuwafikia Mama Lishe na Baba Lishe kwa kuwapa elimu na mafunzo namna ya kutumia nishati safi ya kupikia ,Taasisi , kampuni,mashuleni,kwenye kambi za jeshi ,polisi na magerezani Sido imeweza kupeleka majiko yanayotumia nishati safi ya kupikia huku akiwataka watu kutembelea kwenye banda la Sido  ili wanunue majiko yanayotumia nishati safi ya kupikia  kwenye viwanja vya Sabasaba Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam  katika maonyesho ya 49. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo. 

PPRA YAWAFIKIA WATU WENYE ULEMAVU


 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PPRA  Josefu Muozi amesema watu wenye ulemavu katika  kupata fursa za tenda za PPRA  wamefikiwa kwa kiwango kikubwa huu ni mpango maalum ulioandaliwa na serikali tangu mwaka 2011 na sheria ya PPRA  ikafanyiwa maboresho mwaka 2023  ambako maboresho haya yamesaidia kwa kiasi kikubwa watu wenye ulemavu wa aina zote kupata zabuni za tenda za PPRA. 

Pia PPRA  imeandaa majarida yenye maandishi ya nukta nundu kwaajili ya walemavu wasio Ona na vifaa vya kurekodia sauti zana hizi zimewezesha watu wenye ulemavu kupata elimu na uwelewa kuhusu  zabuni na tenda zinazotolewa na PPRA  vilevile PPRA  inatoa elimu kwa watu wote kupitia redio,tv,magazeti,na makongamano pamoja na semina  kupitia taasisi za watu wenye ulemavu. 

Josefu Muozi amewataka watu kutembelea banda la PPRA  viwanja vya sabasaba maonyesho Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam kwenye maonyesho ya 49 habari picha na Victoria Stanslaus. 


PPRA YAFUNGUA FURSA KWA WATANZANIA


 Mkurugenzi  Mkuu wa PPRA Denisi Simba amewataka watanzania kuchangamkia fursa  za Uzabuni wa tenda mbalimbali zinazotolewa na PPRA  kwani serikali imetenga kiasi cha tilioni 38  kwaajili ya wale wote wanaopata tenda za serikali .

Denisi Simba amesema PPRA  wameweka mazingira rafiki na wezeshi kwa makundi yote ikiwemo wanawake ,vijana,wazee na Watu wenye ulemavu Pia amewataka watu watembelee banda la PPRA  kwenye maonyesho ya 49 ya sabasaba yanayofanyika jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo