Friday 15 December 2023

Habari kubwa Magazetini Kenya leo December 13, 2023

 


Habari picha na Ally Thabiti

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUFUNGUA USHOROBA

 Waziri wa Maliasili ANJERA KAILUKI amesema lengo la kufungua USHOROBA 61 ili Wanyama waweze kupita kwenye njia zao za Asili ambako wizara itaanza na kufungua USHOROBA 42 lakini USHOROBA 20 zipo kwenye mkakati wa kufunguliwa, ambako USAID wamenza kushughulikia USHOROBA 7 Tanzania inashughulikia USHOROBA 2. 

Waziri AJENLA KAILUKI ametoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano zoezi la kufungua USHOROBA likianza nae kwa upande wake PROF wa Chuo Kikuu cha Dodoma JULIUS amesema sekta ya utalii inachangia pato la Taifa kwa asilimia 20% na inasaidia kuwezesha vijana wengi kujiajili na kuajiliwa ameipongeza Serikali kwa kuamua kufungua USHOROBA hapa nchini.

Habari na ALLY THABITI

PROF LIPUMBA AIPA PONGEZI NBS

Mwenyekiti wa Chama cha CUF Prof Ibrahim Lipumba amesema ofisi ya Taifa ya Takwimu imefanya kazi mzuri kwenye zoezi la sensa kwani matokeo haya yatasaidia kupanga mipango ya nchi nae kwa pande wake naibu katibu Mkuu wa CHADEMA upande wa Zanzibar SALUM MWALIMU ameitaka NBS kuweza kuboresha mifumo  ya namna ya kupata taarifa ya matokeo ya sensa.

Habari na VICTORIA STANSLAUS

NBS YAKUTANA NA VIONGOZI WA KIASA

Kamisaa wa sensa na pia alikuwa spika wa Bunge la Tanzania ANNA MAKINDA amewataka wanasiasa nchini Tanzania kuyatumia matokeo ya sensa kwenye kazi zao, nae Mkurugenzi wa Sensa DEVOTHA MINJA amesema wanaenelea kutoa matokeo ya sensa kwa awamu tofauti tofauti kuanzia ngazi ya kata mtaa, wilaya, mkoa na Kitaifa amewataka wananchi kutumia matokeo ya sensa pamoja na viongozi wa kiasa.

Habari na Ally Thabiti

Monday 11 December 2023

Kampuni ya Amsons Group yakabidhi hundi ya Sh.milioni 100 kusaidia waathirika wa mafuriko Hanang

 

LHRC NA WADAU WAWEKA MIKAKATI HAKI ZA BINADAMU

 LHRC na wadau wa haki za binadamu wameamua kuweka mikakati yakupigania usawa wa haki za binadamu kwa makundi yote kuanzia ngazi za chini hadi za juu, wamesema haya katika maazimisho ya miaka 75 ya tamko za haki za binadamu

Habari kamili na Victoria Stanslaus Gaitan




LHRC YAAZIMISHA MIAKA 75


Mkurugenzi mkuu mtendaji wa LHRC Dr. Anna Enga amesema kupitia miaka 75 ya tamko la haki za binadamu zimetolewa na umoja wa mataifa Tanzania imeweza kupiga hatua kwa kiasi kikubwa ikiwemo uhuru wa kujieleza haki ya kuchagua au kuchaguliwa uwemo wa mfumo wa vyama vyingi vya siasa Dr. Anna Enga amemtaka Rais wa Jamuhuri ya muungano ya Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassani kuweza kufanya maboresho kwenye sera na sheria ambazo kandamizi nchini Tanzania Mfano wa Sheria ya ndoa.

Dr Anna Enga amesema miaka 75 hii imefanya kundi la watu wenye ulemavu kupata haki mbalimbali ikiwemo haki ya Ajira, Elimu na zinginezo.

Habari picha na Ally Thabit


THE GLOBAL LEADERSHIP KUWAFIKIA WATU WENYE ULEMAVU

Mkurungezi wa Global Leadership Mbutho amesema mikakati yao kuweza kuyafikia makundi yote kwaajili ya kuwajengea uwezo wakuwa viongozi bora kundi la watu wenye ulemavu ni miongoni mwa mikakati yakuwapa elimu ya uongozi katika nchi 128 nchi 70 zinatoa mafunzo kwakutumia lugha za alama wenye uziwi kwa upande wasio ona wanamipango yakuweka maandishi ya nukta nundu.

habari picha na Ally Thabit