Saturday 20 February 2021

AFISA VIWANGO WA TBS AWATOA MCHECHETO WADAU WA MABATI NA COILI


 Henry Masawe Afisa viwango wa TBS amesema kuwa wanafanya Operation Mbalimbali kwa ajili ya kukagua Mabati na Coili kwa Wazalishaji, Wauzaji na wasambazaji wa bizaa hizi  lengo kuwepo na biadhaa za Mabati na Coili zenye Viwango bora, Pia hatua kari zikichukuliwa zidi yao kusiwepo na malalamiko ndiyo maana wanawashirikisha kila hatua.

amesema haya jijini Dar es Salaam makao makuu ya TBS huduma walipokutana na wadau wa Mabati na Coili.

Habari na ALLY THABITI

SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA (TBS) LAJA NA MIKAKATI MIZITO


 Kaimu mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Davis Mtebalemwa amesema wameamua kukutana na Wazarishaji, Waagizaji na Wasambazaji wa Mabati na Coili kwa ajili ya kujiajili namna ya kutengeneza bizaa bora za Mabati na Coili hii itasaidia kuimalika kwa biashara zao za Mabati na Coili pamoja na kuimalisha afya za watumiaji na kulinda maslahi ya wanunuaji wa bizaa hizo kwani endapo Mabati na Coili zikikosa ubora uchumi wa watu utayumba na Taifa litayumba na afya za watumiaji zitateteleka.

Hivyo amesema ndiyo maana wamekuja na mikakati bora ya viwango vya ubora wa mabati TZS 353 toleo ya mwaka 2020 na TZS 1077 ya Mabati na Coili ambazo zipo kwenye umoja wa jumuiya ya Afrika Mashariki na Kati amesema haya jijini Dar es Salaam Makao makuu ya Shilika la Viwango Tanzania (TBS) Ubungo walipokutana na Wazalishaji, Waagizaji na Wasambazaji wa Mabati na Coili.

Habari na ALLY THABITI

TPSF YASIKILIZA KILIO CHA UWEKEZAJI


 Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Francis Nanai amesema lengo la kukutana na wawekezaji hapa Nchini kuweza kujadili changamoto zinazowakabili, amesema kodi ya VAT na kodi ya sukari ya viwandani imekuwa ni kilio kikubwa kwa wawekezaji hivyo amesema kupitia taasisi hii watakaa na serikali ili waweze kujadili kwa pamoja jinsi ya kuondoa vikwazo vinavyowakabili wawekezaji.

Amesema haya jijini Dar es Salaam alivyokutana na wawekezaji tofautitofauti.

habari picha na

Ally Thabiti

NANDY AWA BAROZI WA PADS ZA LOWLESS SANITARY


 Msanii Nandy amesema Watanzania na wasio Watanzania watumie pad za LOWLESS SANITARY kwani ni salama na ubora pia zinamfanya mtumiaji ajisikie vizuri, ameishukuru kampuni hii kwa kumchagua yeye awe barozi wao amesema haya jijini Dar es Salaam

Habari picha 

Ally Thabiti

Thursday 18 February 2021

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ATOA MAAGIZO MAZITO


 

Mashimba ndaki waziri wa mifugo na uvuvi amesema kuanzia tarehe 17 mwezi 12, 2021 kuku watauzwa kwa kilo, pia ameitaka Bodi ya nyama kwasambalatisha mara moja watu wanaouza vifaranga vya kuku eneo la Tazara wawasambaratishe mara moja na kampuni zinazo walazimisha wateja kununua kuku au chakula cha kuku hatua kali zitachukuliwa dhidi yao na wale ambao wanatotolesha vifaranga vya kuku kienyejienyeji na wanaojifanya mawakala chamtema kuni watakipata maana selikari haiwezi kuwacha uhuni huu ufanyike kwani sector ya kuku ni sector muhimu nchini Tanzania ndio maana Rais Magufuli anaipa kipaumbele ili iweze kuchangia pato la Taifa.

Waziri Mashimba Ndaki amewatoa hofu na mashaka wafugaji wa kuku kuwa changamoto ya kodi na bei elekezi yakuuza kuku amelibeba na kulifanyia kazi.

Mashimba Ndaki amempongeza kaimu msajili wa bodi ya nyama kwa ubunifu wake kwa kuwakutanisha wadau wa sekta ya mifugo kwaajili ya kupata Suruhisho ya changamoto wanazokutananazo wadau hawa kwaajili ya masilahi mapana ya Taifa. Amesema haya jijini Dar es Salaam alivyokutana na wadau Mbalimbali wa Sekta ya mifugo.

Habari picha na Ally Thabith

KAIMU MSAJILI WA BODI YA NYAMA AWAPA FARAJA WAFUGAJI WA KUKU

 


Imani Sichalwe kaimu msajili wa bodi ya nyama ameweza kuwakutanisha wafugaji wa kuku na wadau wanao uza chakula cha kuku vifaranga vya kuku, watalaam wa mifugo, benki ya CRDB pamoja na waziri wa mifugo na uvuvi Mashimba Ndaki lengo kukuza na kuistawisha sector ya ufugaji kuku ambapo changamoto zifuatazo ziliweza kujadiliwa na kupatiwa ufumbuzi ikiwemo ukuaji wa bei na viranga vya kuku kutoka shilingi 1700 hadi 2300 ambapo hiki ni kilio kikubwa cha wafugaji kuku Dar es Salaam. Bei ya chakula cha kuku bei yao imekuwa kubwa swala la kuuza kuku kwa kilo wafugaji wa kuku wamewasilisha kwa waziri na kutafutiwa masoko na machinjio ya kuku. 

Kaimu msajili wa bodi ya nyama amesema amehitisha kikao hiki ili kumsaidia Rais Magufuli katika hazima yake ya ujenzi wa viwanda na kukuza uchumi wa Tanzania ambapo wafugaji hao wa kuku watasaidia kwa kiwango kikubwa katika kukua uchumi wa Tanzania, amewatoa hofu wafugaji wakuku nchini Tanzania kuwa Bodi ya nyama imewawekea mazingira ya rahisi na rafiki ili waweze kujikwamua kiuchumi na milango ipo wazi kwa watakao hitaji mawazo, ushauri na wataalam, amesema vikao hivi vitakuwa vinafanyika mara kwa mara huku akiwataka wauza viranga vya kuku na chakula cha kuku pamoja na chanjo za kuku wasiwakandamize na kuwaonea kwakuwauzia viranga vya kuku visivyokuwa na ubora dawa pamoja na chakula wakifanya hivyo watauwa mitaji ya wafuagaji kuku amesema. Amemshukuru waziri wa mifugo na uvuvi Mashimba Ndaki pamoja na Mkuu wa wilaya ya Ilala kwa kuwaweza kuwasiliza wafugaji kuku na kutatua kero na changamoto zinazowakabiri wafugaji kuku.

Habai picha na Ally Thabith 

Tuesday 9 February 2021

AIRTEL YAPASUA ANGA


Airtel yaboresha mtandao kwenda masafa ya Supa-4G. Yaja na ofa kabambe za internet

  1. Ukianza kutumia aini ya Airtel utapata intaneti mara mbili bure BURE kwa kipindi cha miezi sita (Airtel dabo Data)
  2. Airtel imepunguza bei ya Airtel Mi-Fi kwa kurudisha GB 40 bure ili wateja wafuahie mtandao wa Airtel supa 4G kwenye simu za 3G.
  3. Airtel inatoa 7GB bure kwa wateja wote ambao watabadili laini kutoka 3G kwenda laini 4G
Dar es Salaam tarehe 09/02/2021. kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza kukamilisha maboresho makubwa kwenye mtandao wake wa 4G kwenda kwenye masafa ubora zaidi ya Airtel Supa 4G ili wateja wake waendelee kuperuzi kwa uharaka zaidi popote. Akizungumza jijini Dar es salaam leo wakati wa kutangaza maboresho ya masafa hayo ya Airtel supa 4G, Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema kuwa kwasasa "wateja wa Airtel kupitia maboresho ya mtndao wa Airtel Suapa-4G watapata huduma bora zaidi ya ilivyokuwa awali, watafurahia kuperuzi mtandao kwa kasi zaidi ndani ya miji mikubwa zaidi ya 500 nchini Tanzania iliyofanyiwa maboresho haya ya kufurahia huduma za kidigitali kama video za mfumo wa HD.

Tumewekeza kwa kiasi kikubwa katika maboresho ya mtazamo wetu ili kukamilisha ahadi yetu ya kutoa huduma bora ya intaneti (Data) pamoja na huduma za kupiga simu kimataifa kwaajili ya wateja wetu.

Huduma ya Airtel Supa 4G inapatikana kwenye masafa y a700MHz NA 2100 MHz, ambapo kasi yake inawezesha wateja wetu sasa KUPERUZI kwenye mtandao kwa kasi ya 40Mbps kasi hii inafanya huduma yetu kimtandao kufikia viwango vya kimataifa zaidi na kwafaidisha wateja wote.

Mkurugenzi huyu wa mawasiliano wa Airtel Tanzani ameongeza kuwa kufuatia kuambaa kwa mtandao huu wa supa 4G, Airtel tumefanya mawasiliano kuwa nafuu zaidi kwa wateja wetu ili kufaidi mtandao wa Supa - 4G. Airtel saas imezindua huduma tatu kwa wateja ambazo zinapatika kwa kasi zaidi ili kuperuzi kutpita supa 4G ambazo ni 

  • Wateja wote wa Aitel ambao wanatumia laini za 3G endapo watabadilisha laini zao za simu kwenda kwenye mfumo wa 4G watapata ofa ya 7GB ndani ya wiki mbili bure
  • Ipo ofa ya intaneti mara mbili (Dabo data) kwa wateja ambao wataanza kutumia smartphone zao kwa mara ya kwanza na mtandao wa Airtel kwa miezi 6
  • Airtel tumepunguza bei ya Airtel Mi-Fi sawa na Tsh 75,000 ikiwa na 40 G0GB bure sawa punguzo la shilingi 30,000. Mi-Fi hii pia itawezesha wateja asio na simu za smartphone za 4G kutumia Mi-fi na kufurahia kasi ya Airtel Supa 4G yenye uwezo wa kuunganisha zaidi ya wateja 10 kwa mara moja
Nae Meneja wa huduma za intaneti wa Airtel Ezekiel Kahatano ilielezea kuwa "uzinduzi wa Mtandao wa Airtel 4G-supa pamoja na kuanzisha ofa za bei rahisi za Airtel Supa 4G ni sehemu ya mipango ya Airtel ya kuboresha huduma za mawasiliano na kukuza utumiaji wa kuperuzi mtandao wa Airtel kwa kasi ya Airtel supa 4G kwani inakuja na teknolojia ya kisasa inayolenga kupunguza gharama za huduma za mawasiliano.

Habari na Ally Thabiti