Friday 25 November 2022

Kwa mara ya kwanza madaktari wazawa wafanya upasuaji wa kubadilisha sehemu ya mshipa mkubwa wa damu (Aorta)

 24/11/2022 Madaktari wazawa mabingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa mara ya kwanza wamefanya upasuaji wa kubadilisha sehemu ya mshipa mkubwa wa damu (Aorta) ambao unatoka kwenye moyo mpaka sehemu inayotoa matawi ya mishipa inayopeleka damu kwenye kichwa na ubongo (ascending aorta and arch).

Upasuaji huo unaojulikana kwa jina la kitaalamu la Bental Procedure and hemi-arch aortic repair ulichukua masaa kumi kukamilika kutokana na mshipa wa mgonjwa kutanuka ukihusisha na mshipa unaopeleka damu kwenye kichwa na ubongo.

Mbali na kuusimamisha moyo kutokana na upasuaji huo kuhusisha sehemu ya Aorta inayotoa mishipa ya damu kupeleka kwenye ubongo ilibidi wataalam hao kusimamisha msukumo wote wa damu kwenda kwenye ubongo na mwili mzima kwa muda wa dakika 45 ( Deep hypothermia and circulatory arrest).

Akizungumzia kuhusu upasuaji huo Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa JKCI Evarist Nyawawa alisema baada ya kumfanyia vipimo mgonjwa huyo waligundua kuwa valvu inayopitisha damu kutoka kwenye moyo kwenda kwenye mshipa mkubwa na kusambaza damu mwilini (Aortic Valve) ulikuwa unavujisha damu.

Dkt. Nyawawa alisema wataalam walishauri mgonjwa huyo afanyiwe kipimo cha CT Scan ili kuchunguza mshipa wa aorta kwa kutumia kipimo kinachoitwa  CT Angiograph na kuthibitisha kuwa mshipa mkubwa wa damu ulikuwa umetanuka kwa kiwango kikubwa kutoka kwenye valvu kwenda mpaka kwenye ascending aorta na sehemu ya arch of aorta.

“Tulipokea mgonjwa ambaye alikuwa na tatizo la kuumwa kifua na kubanwa kifua huku akijisikia mwili kuchoka sana hivyo kumfanyia kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO Cardiograph) na kugundua kuwa valvu inayopitisha damu kutoka kwenye moyo kwenda kwenye mshipa mkubwa na kusambaza damu mwili mzima (Aortic Valve) ulikuWa unavujisha damu,” alisema Dkt. Nyawawa.

Dkt.Nyawawa alisema kwa kawaida mgonjwa akiwa na mshipa uliotanuka hadi kwenye arch of aorta upasuaji wake unakuwa mgumu na wa hatari kwa sababu mbali na kuusimamisha moyo unahitaji vilevile wakati wa upasuaji usimamishe msukumo wote wa damu kwenda kwenye ubongo na mwili mzima.

 “Tumefanikiwa kupandikiza mshipa bandia sehemu ambayo mshipa wake ulikuwa umetanuka na kubadilisha valvu lakini pia tulitoa ile mishipa midogo midogo ya moyo (Coronary) ambayo inapeleka damu kwenye misuli ya moyo na baadaye kuipandiza tena kwenye ule mshipa bandia,” alisema Dkt. Nyawawa.

Dkt. Nyawawa alisema baada ya upasuaji mgonjwa amepona na ataweza kufanya kazi zake zote bila ya kupata dalili alizokuwa nazo hapo awali za kuchoka, maumivu ya kifua na kushindwa kupumua.

“Wagonjwa wanaopata dalili za kuchoka, pumzi kukata na kifua kubana wanapaswa kupumzika kwanza na kufika hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ili waweze kupatiwa matibabu mapema kwani ni hatari mshipa wa damu mkubwa ukitanuka na kupasuka husababisha mgonjwa kupoteza maisha yake,”.

“Kuna sababu nyingi zinazosababisha mshipa mkubwa wa damu kutanuka na kupasuka lakini sababu kubwa huwa ni shinikizo la damu kwani wagonjwa wengi tuliowaona wamepata tatizo hili kutokana na kuwa na shinikizo la damu,”alisema Dkt. Nyawawa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Upasuaji wa JKCI Dkt. Angela Muhozya alisema JKCI kwa kutumia madaktari wazawa imefanikiwa kufanya upasuaji huo mkubwa kwa wagonjwa wawili ndani ya wiki moja mafanikio makubwa ambapo tofauti yao mgonjwa mmoja mshipa wake ulikuwa umetanuka sana hadi sehemu ambapo kuna mishipa midogo inayopeleka damu kwenye ubongo.

Dkt. Anjela alisema upasuaji huo unatakiwa kufanyika kwa uangalifu mkubwa kwasababu mishipa midogo ya damu isipopandikizwa vizuri mgonjwa anaweza kupata matatizo kwenye ubongo, sehemu zote za kichwa pamoja na mishipa ya damu.

“Mgonjwa mwingine tuliyemfanyia upasuaji wa aina hii  alikuwa na umri wa miaka 35 ambaye mshipa wake mkubwa wa moyo ulikuwa umetanuka sana na kuchanika kwa ndani hivyo kutengeneza njia mbili kubwa ambazo zimekuwa zikipitisha damu na kuathiri mishipa ya kupeleka damu katika kichwa na ubongo,” alisema Dkt. Angela.

Dkt. Anjela ambaye pia ni daktari bingwa wa usingizi na wagonjwa mahututi alitoa wito kwa wagonjwa wanaopata maumivu ya ghafla ya kifua au kupoteza fahamu waende hospitali haraka kwa ajili ya kufanyiwa vipimo zaidi pamoja na kupata matibabu.

Naye mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji huo Mohamed Dinya alisema amefarijika kuona wataalam wa JKCI wana utaalam mkubwa kwani hakutegemea kama angefanyiwa upasuaji huo kutokana na hali yake ilivyokuwa hivyo kuwafanya wataalam wageni waliofika katika Taasisi hiyo kuhairisha upasuaji zaidi ya mara mbili.

“Hivi karibuni kulikuwa na wataalam wa afya kutoka nchi tofauti na hapa ambao walinifanyia uchunguzi na kuondoka bila ya kunifanyia upasuaji kutokana na upasuaji wangu kuwa mgumu na wa hatari lakini madaktari hawa wa JKCI hawakukata tamaa wakasema watanifanyia upasuaji na leo kama unavyoniona naendelea vizuri,”.

“Madaktari wa hapa ni wazuri sana, watanzania wenzangu msiogope kupatiwa matibabu hapa na kukimbilia nje ya nchi kwani labda leo ningeenda nje ya nchi nisingefanyiwa upasuaji kutokana na tatizo langu kuwa kubwa na wataalam kuogopa kunifanyia upasuaji huo,” alisema Dinya.

Habari kamili na Ally Thabit



NICOL YAWAFUTIA WATU KUWEKEZA


Mkurugenzi mkuu wa NICOL Erasto amewataka watu kutumia taasisi yao kwenye uwekezaji kwani watapata manufaa makubwa pia hisa zinapatikana kwa wingi.

Habari kamili na Ally Thaibit

NMB YAPATA TUZO ZA KIBABE


Mkurugenzi wa NMB Bank Lucy Zaipuna amesema wanashukuru kupata tuzo za Bank Bora hivyo wataendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Habari kamili na Ally Thabit

MKURUGENZI WA TAFIRO AMESEMA WANAFANYA UTAFITI WENYE TIJA

 Mkurugenzi mkuu wa shirika la utafiti wa misitu nchini Tanzania amesema utafiti unaofanywa unasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuzibiti upotevu na uaribifu wa misitu nchini Tanzania.

Habari na Ally Thabit

NAIBU WAZIRI WA MARIASILI NA UTALII HAJA NA MIKAKATI YAKUDHIBITI UARIBIFU WA UOTO WA ASILI

 Marry Masanja naibu waziri wa Mariasili na utalii amesema wanasibitishwa na upotevu wa uoto wa asili kiasi cha milion 5.2 hivyo wakuja na mpango mkakati kwaajili ya kuzuia na kurejesha uoto wa asili kwa kutoa elimu kwa jamii namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya Nchi.

habari Picha na Ally Thabit

KAMISHNA WAKALA WA MISITU AELEZA NAMNA WANAVYO WAFIKIA WATU WENYE ULEMAVU

 Kamishina wa Wakala wa misitu Nchini Tanzania TFS amesema wanaendesha miradi kwenye mkoa wa Kagera, njombe na Iringa ambako watu wenye ulemavu wanajishughulisha na shughuli mbalimbali ikiwemo ufugaji nyuki. Kamishna amesema TFS inawashirikisha watu wenye ulemavu kwa kiasi kikubwa.

habari na Ally Thabit

MRATIBU WA MRADI WA MAISHA BORA ATOA NENO

 Mratibu Agness Sameja amewataka wazazi na walezi nchini Tanzania kutowafungia ndani watoto wenye ulemavu pia ametoa wito kwa watoto wenye ulemavu waliopo mashuleni kusoma kwa bidii na watoe taarifa pindi wanapotendewa vitendo vya ukatili wa kijinsia. Amesema haya wakati wa kukabidhi pea 30 za uniform kwa wanafunzi wasio ona shule ya msingi Toangoma kupitia mradi wa Maisha Bora chini ya kanisa la FCPT.


Habari picha na Ally Thabit

MCHUNGAJI WA FCPT AHAIDI MAZITO

 Mchungaji wa kanisa la FCPT lililopo Toangoma Henry Katamba amesema mradi wao wa maisha bora ambao unatekelezwa kwenye mikoa saba Tanzania utaendelea kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu amesema haya wakati wa kukabidhi Pair 30 za uniform kwa wanafunzi wasioona shule ya msingi Toangoma Dar es  Salaam.



Habari Picha na Ally Thabit

WIZARA YA MARIASILI NA UTALII WAJA KUZIBITI WA UOTO WA ASILI




 




Habari picha na Ally Thabith

Monday 21 November 2022

MWENYEKITI WA CCM WILAYA YA KIGAMBONI AMPONGEZA SAMIA

 SIKU NJEMA YAHAYA SHABANI mwenyekiti wa ccm wilaya ya kigamboni amesema rais Samia Suluhu Hassan amefanya makubwa kwenye nchi ya Tanzania pia ameweza kufungua miradi mikubwa wilaya ya kigamboni nakutoa fedha nyingi katika wilaya hii.


habari kamili 

Ally Thabith

AZAM TV YAFUNGUA DUKA JIPYA KARIAKOO


 

HABARI PICHA NA ALLY THABITH

Sunday 20 November 2022

MBUNGE WA SEGEREA KUIBUWA VIPAJI

 Mbunge Bona wa jimbo la segerea ameamua kuja na michuano wa mpira wa miguu ambako tarehe 03 December uzinduzi unafanyika jumla ya timu 64 zitashirki ambako mshindi wa kwanza atapata shilingi milioni tano. mshindi wa pili milioni tatu amesema lengo hili la michuano hii nikuibua na kukuza vipaji vya vijana ili waweze kuajiliwa huku akijipanga kuanzisha michuano ya watu wenye ulemavu.

Habari na Ally Thabith

WAZIRI NAPE AIPONGEZA TBC

NAPE MOSES NAUYE waziri wa habari technologia na habari amelipongeza shirika la habari nchini Tanzania TBC kwa kupata haki za kuonesha michuano ya kombe la dunia inayofanyika nchini Qatar nae kwa upande wake msemaje mkuu wa serikali Gereson Msigwa amevitaka vyombo vya habari nchini Tanzania kutoa habari zenye uweredi kama TBC ambako ameahidi kutoa ushirikiano kwenye kuonesha na kutangaza michuano ya Kombe la michuano nchini Qatari uku mwenyekiti wa bodi ya TBC anaitwa STEVEN KAGAIGAI amewataka watu kujitokeza kwa wingi kutangaza nakuonyesha bidhaa zao kupitia TBC pia Mkurugenzi mkuu wa TBC Dr. Ayubu Ryoba amesema TBC itaonesha mechi 28 kwenye kombe la Dunia kwa lugha ya kiswahili na kwa muonekano wa HD na upande wa radio TBC itatangaza mechi 24.

Meneja masoko wa TBC ametoa wito kwa makampuni viwanda kuweza kutangaza na TBC kwenye kombe la dunia.

Habari 

Ally Thabith

Friday 18 November 2022

UTT AMIS YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI


 

TAASISI YA HATUA GROUP YAJA KUWAKOMBOA MAMA WAJAWAZITO

Mkurugenzi Derick Mgaya wa taasisi ya hatua group imeamua kuja na program ya mazoezi kwa mama wajawazito, elimu ya lishe na maswala ya kisaikolojia lengo kunusuru na kuokoa vifo vya mama wajawazito wakati wa kujifungua na kabla ya kujifungua ambapo program hii itaanza mwezi wa pili 2023 uzinduzi umefanyika kwenye hospitali ya Mbagala Zakhiem. Nae kwa upande wake mkurugenzi wa vifaa vya kujifungulia wa mama wajawazito RENATUS ameunga mkoni juhudi na jitihada zilizofanywa na taasisi ya hatua group nae mwakirishi wa mkuu wa wilaya amesema ni vyema mama wajawazito kuunga mkono mradi huu kwani itawasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuimalisha Afya zao na watoto waliopo tumboni.

Nae Dakatari wa ushauri wa program hii ndug. Michael amesema watahakikisha wanawafikia mama wote wajawazito.

Habari kamili

Ally Thabith

MAMLAKA YA ANGA YASIBITISHA UWANJA WA BUKOBA NI SALAMA

 Mkurugenzi Hamza Johar amesema uwanja wa Ndege wa Bukoba ni salama kwa ndege kutua na kupaa

Habari kamili 

Ally Thabiti

RAISI WA IST APANGA MIKAKATI MIZITO

 Bilauri Tryphon Pastory rais wa IST amemshukuru Raisi Samia Suluhu Hassan kwakuweza kuwaunga mkono masavea nchini Tanzania pia ameiomba serikali kuweza kufanya mabadiriko ya sheria sura namba 270 na Namba 324.

Hbari kamili na Ally Thabith

TANROAD YAJA KIVINGINE

 



UTT AMIS YATOA NENO

 




TAHLISO YAIPONGEZA SERIKALI KWA KUTENGA FEDHA BODI YA MIKOPO