Monday 29 April 2019

SHIRIKISHO LA WANASAYANSI CHIPUKIZI, WAJIVUNIA MAMBO MAZITO.

Na. Ally Thabiti

Mtendaji mkuu wa shirikisho la wanasayansi wanaochipukia, Dkt. Gosbert Kamugisha, amesema kuelekea miaka saba ya maonesho ya wanasayansi wanaochipukia wameweza kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na tafiti wanazozifanya kutatua changamoto za hapa nchini Tanzania hasa katika sekta ya teknolojia, afya, maji.

Dr. Gosbert Kamugisha, Mtendaji Mkuu Shirikisho la Wanasayansi Wanaochipukia


Pia imeelezwa kuwa  Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTEC) wametumia tafiti za vijana hao wanasayansi hadi kuwa mawazo ya kibiashara na wafanyabiashara wa sekta binafsi wamenufaika kwa kiasi kikubwa kutokana na mawazo ya vijana hao.

Dkt. Kamugisha ameyasema hayo wakati wa mkutano na wanahabari jijini Dar es salaam ikiwa ni maandalizi ya mwisho ya maonesho ya saba ya wanasayansi wanaochipukia yanayotarajiwa kufanyika mwezi August mwaka huu wa 2019 katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC)

Dkt. Kamugisha ameongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa shirikisho hilo, wameweza kuhamasisha vijana wa kitanzania katika shule za msingi na sekondari kupenda masomo ya sayansi.

Tuesday 23 April 2019

UCHUMI WA TANZANIA MASHAKANI KUPOLOMOKA


Mwenyekiti wa chama cha CAF Prof Ibrahimu Haruna Lipumba amemtaka wazili wa fedha Philip Mpango awezekukubali machapisho ya shilika la fedha duniani IMF yawekwe hazalani ilitupate kujifunza makosa yetu.

Habari Picha na

Ally Thabiti

WATANZANIA WATAKIWA KUWA WAZALENDO


Steve Nyerere amewataka watanzania hapa Nchini kuwa wazalendo katika kutangaza utalii wetu kwani mapato yataongezeka kwa kiasi kikubwa.

Habari Picha na

Ally Thabiti

HLRC YAVUNA MAPESA


Pichani Balozi wa Nolwe Elizabeth Jacobsen akitiliana saini na mkurugezi wa kituo cha haki za binadamu HLRC Anna Enga kwaajili ya kutoa msaada wa fedha Dola za kimarekani Bilioni Mbili Nukta Mbili  kwa ajili ya utetezi wa hazi za binadamu nchini Tanzania.

Habari Picha na

Ally Thabiti

Thursday 11 April 2019

MUFTI MKUU WA TANZANIA ATEMA CHECHE


Mufti Mkuu wa Tanzania Abubakari Bin Zuberi amezitaka taasisi za kidini za Kiislamu hapa nchini wawape walimu wao maslayi mazuri ya Kifedha na mahali pa kuishi. Pia amewataka wanafunzi waliohitimu mafunzo ya kidini wawemabarozi wema pia amesema ameipongeza taasisi ya Al-Hikma Foundation kwa juhudi na bidii kwa kutoa elimu ya kidini hapa nchini amemalizia kwa kusema pia wataendelea kushilikiana na taasisi zote hapa nchini.
Ametoa pwito kuhubili amani na kumpongeza Sheikhe Nurudin Kishki kukuza na kueneza Uislamu.

Habari Picha na

Ally Thabiti

PICHANI MUFTI MKUU WA TANZANIA HAKITOA ZAWADI


Mufti Mkuu wa Tanzania Abubakari Bin Zuberi akiwapa tuzo wanafunzi wa Al-Hikma Foundation.

Habari Picha na
Ally Thabiti

SHEIKHE KISHKI ATOA NENO LA FARAJA


Kiongozi wa Taasisi ya Al- Hikma Foundation Nurudin Kishki amesema wana mipango ya kuleta Quruan yenye maandishi ya nukta nundu kwaajili ya kuwafundisha watu wenyechangamoto ya kutokuona pia Kishki nje nyingi alizozunguka za Kialabu wanafunzi wasiona wanatumia kusoma Quruan kwa kutumia maandishi ya nukta nundu ndiyo maana wao wameamua kutatua changamoto hii kwa kuleta nukta nundu lengo wawafikie wasiona kwa kiasi kikubwa ametoa wito kwa taasisi zingine za dini ya Kiislamu katika kuwapokea na kuwafundisha watu wasiona maswala ya kidini.
Amesema haya Hoteli ya Kilimanjaro wakati wa kuwapa tuzo wanafunzi kumi na mbili wa Al-Hikma Foundation.

Habari Picha na
Ally Thabiti.

MWENYEKITI WA HAZBATI HATOA NENO ZITO


Mwenyekiti wa chama cha HAZBATI amewataka wazazi wawatoto wenyevichwa Viikubwa na Mgongo wazi wachane na zana potofu hivyo na kuwataka watumie madini joto kwenye vyakula vyao wakati wakiwa na ujauzito na wakati wa kujifungua.
Pia wawape watotot vyakula vyenye lishe.

Habari Picha na
ALLY THABITI

TAKUKURU WILAYA YA TEMEKE YAWAFUTA CHOZI WANYONGE


Naibu  kamishna wa Takukuru wilaya ya Temeke Ramadhani Mbwata amesema kiasi cha shilingi Bilioni moja na Milioni Miambili Harobaini na Moja za ujenzi wa shule za sekondari ya mbagala kuu ya kidato cha tano na cha sita pia wameokoa kiasi cha shilingi Milioni Mianne za ujenzi wa Zahanati ya eneo la kimbiji na huduma za kiafya zinatolewa mpaka sasa na kwa upande mwengine wamezibiti makato ya mechi za simba na FC VITA pamoja na timu ya Taifa na Uganda.
Pia ametoa wito kwa watanzania kutoa taarifa na kushilikiana nao kiukamilifu

Habari Picha na
ALLY THABITI

CHAMA CHA HASBATI CHALETA MATUMAINI


Mratibu wa chama cha watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi Hidaya Harawi wanatoa mafunzo mbalimbali lengo kuhamasisha wazazi wenye watoto wenyevichwa vikubw na mgongo wazi wawapeleke mahospitalini

Habari Picha na
ALLY THABITI