Thursday 29 April 2021

HAKI ELIMU YAJA NA MUHAROBAINI KABAMBE

 Taasisi ya Haki Elimu imezindua Mipango ya kuboresha Elimu ndugu Meena amewasilisha mapendekezo ya matumizi ya lugha,mabadiliko ya sera na maswala mengineyo yanayoushu Elimu 

Habari picha na Ally Thabiti

Wednesday 28 April 2021

NEDHIRI MEENA AWAKOSOA UNA


 Muandishi Mkongwe Nedhiri Meena amewataka UNA kuachakujifungia wenyewe kwenye mikutano yao bila kuwashirikisha Wanahabari


Habari picha na Victoria Stanslaus

MUHARIRI AIKOSOA KATIBA YA TANZANIA


 Muhariri wa Gazeti la Jamuhuri Deodadisi Balile amesema kuwa Ibara ya 152 ya katiba ya tanzania  aitoi fursa na nafasi kwa Wanahabari .ameitaka selikari kuweka mazingira rafiki na wezeshi kwa Wanahabari ili wafanye kazi zao kwa uhuru,Amani na usawa

Pia amewataka Wanahabari  watoe taarifa sahihi 

Habari picha na Victoria Stanslaus

MUFUTI WA TANZANIA KUWAINUA WENYE ULEMAVU


Mufuti Mkuu wa Tanzania  Abubakari bin Zuberi  amewataka wazazi na walezi wa watoto wenye Ulemavu wawapeleke wakasome maswala ya Dini  ,kwani baraza kuu la waislam Tanzania  (BAKWATA)  litatoa  mafunzo ya kwa wasio Ona kwa kutumia maandishi ya nukta nundu ambako kutakuwa na mwalimu kutoka Morogoro .

Mufuti ametoa wito kwa waislam na watanzania kipindi hili cha mwezi mtukufu wa ramadhani kuwaombea viongozi wetu wa nchi  na kuiombea Amani iendelelee kuwepo Tanzania . amesema haya nyumbani kwake Magomeni Mikumi jijini Dsm wakati akiongea na Wanahabari .

Habari picha na Ally Thabiti


Tuesday 27 April 2021

WATAARAM WA HALI YA HEWA WAJA NA MIKAKATI MIZITO


 James  ni Mratibu mwandamizi anaesimamia maswala ya Hali ya Hewa Africa Mashariki  amesema Kutokana na mabadiliko ya Hali ya Hewa wameamua kukutana kwaajili ya kuweka mipango mikakati kwaajili ya kuwasaidia watu wa Africa Mashariki.

Namna ya kukabiliana na kujilinda na maswala ya  Hali ya Hewa pia amesema wanna mipango wa kuwafikia watu wenye Ulemavu . Nae Chili Sangarugembe  Principal Meteorologist amesema rasilimali watu ,uchache wa pesa,upungufu wa vifaa ni jambo ambalo linakwamisha  vita ya kukabiliana  na mabadiliko ya Hali ya Hewa Africa Mashariki picha ya changamoto hizi kazi kubwa  unafanyika .amesema haya jijini Dsm

Habari picha na Ally Thabiti


MJASILIA MALI ATAKA KUUNGWA MKONO


 Mjaailia Mali  kutoka Kigamboni amewataka watu watumie bidhaa zake kwani anaziandaa katika ubora unao faa .ambako miongoni mwa bidhaa zake ni Viungo mbalimbali pamoja na Unga 

Habari picha na Victoria Stanslaus

BRITISH YAWATOA HOFU WANAWAKE


 Merry Samweli  amesema wameandaa kongamano la Wanawake ,Lengo kuwajengea Uwezo katika matumizi ya Tehama .wataendelea na mradi huu mara kwa marahabari picha na Victoria Stanslaus




TPSF YAJA KIVINGINE


 Mbunge wa Kibaha ndugu Koka amewataka watanzania kujiunga na TPSF Lengo changamoto wanazokutana nazo kwenye Biashara zao ziwezwe kitatuliwa kwa wakati .

Pia ndani ya TPSF kuna fursa mbalimbali ambazo zinapatikana Mbunge Koka amesema haya jijini Dsm wakati wa Uzinduzi wa kamati mbalimbali jijini Dsm

Habari picha na Victoria Stanslaus

WAZIRI MKUU AKAGUA MRADI WA KIMKAKATI


 Pichani Waziri Mkuu wa Tanzania Majaliwa Kasim Majaliwa akipewa maelezo namna mradi wa Treni ya Umeme ulipofikia na Mkurugenzi Mkuu wa TRS  Masanja Kadogosa jijini Dsm 

Habari picha na Ally Thabiti

NAIBU KATIBU MKUU AWAFUNDA WANAHABARI


 Ally Posi amewataka wana habari kutoa habari zao zenye kujenga pia wazingatie  Uweledi,Uadilifu na Uzarendo . Anewapongeza UNESCO kwa kutoa Tuzo kwa  Wanahabari Wanawake kwani itawawezesha  kufanya kazi kwa kasi na nguvu kubwa . Amesema haya jijini Dsm

Habari picha na Ally Thabiti

MKURUGENZI WA ITV ATEMA CHECHE


 Joyce Mwaziri  Mkurugenzi wa ITV amewataka Wanawake  kujitokeza kwa wingi katika kusomea maswala ya wahandishi wa habari ili wapate sauti kwa kiwango kikubwa .

Pia amewataka wahandishi wa habari Wanawake na wasichana kutoa taarifa za ukatili wanaofanyiwa kwenye vyumba vyao vya habari  , amesema haya jijini Dsm baada ya kupewa Tuzo na UNESCO 

Habari picha na Victoria Stanslaus

Monday 19 April 2021

MSHINDI WA JUZUU 32 ATOA NENO

 Kasimu Ayubu amewataka watanzania kuwapeleka watoto wap madrasa ili waweze kujifunza kusoma kolohani ,pia Ameipongeza taasisi ya bi Aisha Suluhu kwa kuendesha mashindano haya ya 19 kwani yanawasaidia Vijana wengi. Kwa kumjua Mungu na kujikwamua kiuchumi .

Kasimu Ayubu amepata zawadi ya milioni 4 baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika kuifadhi  kolohani .

Nae mgeni rasimi kwa niaba ya Waziri  Mkuu naibu Waziri wa Uvuvi na Mifugo Habdallah Hamisi Ulega amewatoa hofu wale ambao  wameshindwa wasikate tamaa ,pia anewapongeza washindi na waandaaji wa mashindano amesema haya kwenye viwanja vya mnazi mmoja jijini Dsm 

Habari na Ally Thabiti

Sunday 18 April 2021

TAMWA YAZINDUA KAMPENI YA KUZUIA UKATILI MTANDAONI

 Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania  (TAMWA ) kwa kudhirikiana na Friedrich Ebert Stiftung (FES) Kutokana na mabadiliko ya Tekinolojia wameamua kuja na kampeni  maalum ya kupinga ukatili  wa kijinsia unaofanywa mitandaoni(ZIMICA )

Kampeni hii ya mwezi 1 kuanzia mwezi 4 hadi 6 mwaka 2021 ,Inalenga kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji  dhidi ya Wanawake na watoto wa kike.

 Ataivyo Roes Reuben Mkurigenzi wa Tamwa amesema ukatili wa kijinsia unaofanywa katika hali ya kudhuru mwili,vipigo,ubakaji,ulawiti,ukeketaji,ndoa za utotoni ,mimba za mapema,rushwa ya ngono na matusi .

Ukatili huu unafanyika kwa njia ya intranet kama fece book,whatsapp,instagram, you tubu na twitter 

Ambako Takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaonyesha ongezeko kubwa la watumiaji wa intanet .ambako mwaka 2017 waliongezeka kwa asilimia 16 na kufikia 23 milioni na asilimia82 kati yao walitumia mitandao hivyo kwa njia ya simu .

Mala kadhaa tunaona video za utupu za Wanawake,watoto wa kike zinasambazwa kwa makusudi na video za ngono huu ni uzalilishaji unaofanywa mitandaoni  ,udhalilishaji huu una madhara kisaikolojia na hata kupelekea kujiua na kupoteza mwelekeo wa maisha.

Roes Reuben Mkurigenzi wa Tamwa amesema nia ya TAMWA na FE S ni kuzuia ukatili na kuongeza uelewa kwa jamii na kujua madhara ya ukatili hasa kwa Wanawake  na kujua mbinu za kuepuka  udhalilishaji.

Zipo sheria zinazozuia ukatili mfano sheria ya maudhui ya mitandaoni (online content Regulation) inakataza kutoa na kurusha maudhui ya udhalilishaji unaokwenda kinyume na Tamaduni ya Mtanzania.

Kuendelea kwa ukatili huu pengine kwa waasirika kutofahamu sheria  na au kuona aibu katika kuitafuta haki  na hofu ya kuzalilika zaidi pindi kesi inapopelekwa mahakanani .

Tamwa wamesema ni vyema kujua kuwa udhalilishaji huu haukubaliki, ni muhimu kutambua kuwa zipo sheria zinazotulinda na muhimu kujua wapo wadau wanao weza kutusaidia.

Aidha kuna hadhabu kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii vibaya ikiwemo faini ya sh milioni 5 au kifungo kisichopungua miezi 12 au vyote kwapamoja . Tamwa wametoa wito kwa selikari na asasi za kiraia kuzungumzia madhara ya vitendo vya ukatili wa mitandaoni ,na kutoa elimu kwa jamiii na kwa kizazi cha sasa , kuusiana na madhara ya kuitumia  mitandao ya kijamii kama njia ya kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Pia Tamwa wametoa wito kwa jamii kuwa maswala ya ukatili wa kijinsia ni jukumu la kila mmoja wetu ,asasi za kiraia,madawati ya kijinsia,selikari,jeshi la polisi wasaidizi wa sheria na wasanii  kukemea na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia 


Habari na Victoria Stanslaus

STANDARD CHARTERED YAJIVUNIA MAMBO MAKUBWA

 Standard Chartered Bank yapata wateja laki moja wenye akaunti. Ivyo wanatoa wito kwa watanzania na wasio watanzania  kuitumia bank ya standard Chartered kwaajili ya usalama wa pesa zao 

Jonita Malamba Mkuu wa kitengo cha Mausiano na Masoko wa Standard Chartered amesema wameamuwa kuwapeleka washindi watakao shinda kwenye shindano lao . Watakao pata pwenti 200 watapelekwa Wingereza  eneo la Afridi kwenye klabu ya Riva pool kwaajili ya kujifunza mambo mbalimbali  

Habari na Victoria Stanslaus



Wednesday 14 April 2021

KIWANDA CHA BORA CHAWATOA OFU WATANZANIA

 Meneja Masoko wa Kiwanda cha BORA amesema wataendelea kuzalisha kwa wingi Mifuko  Mbadala amewataka watanzania na wasio watanzania kuitumia Kiwanda cha BORA kwa bidhaa mbalimbali 

Kwani bidhaa zao ni nzuri na bora pia azichafui mazingira amesema haya kwenye wadau wa Mazingira na CTI 

Habari na  Ally Thabit  

BARAZA KUU LA CHAMA CHA CUF LATOA NENO ZITO

 Mwenyekiti wa Chama cha CUF profesa Hiblaim Alina Lipumba  wamemtaka rais Samia Suluhu Hasani kuondoa uminywaji wa demokrasia nchini,kuwepo kwa Tume huru ya Uchaguzi ,kuendeleza mchakato wa katiba mpya. 

Pia wameikosoa taarifa ya C AJ kuwa nagari yalio nunuliwa yameandikwa kwa jina la Chama cha CUF. Pia Chama kinataka kuwepo na mikutano na maandamano .

Swala la kuachiwa kwa Muamsho litekelezwe Chama cha CUF kinasikitishwa na hali ngumu ya kimaisha .ambako kwa takwimu za Tanzania watu milioni 15 no masikini na takwimu za kidunia watu milioni 28 ni masikini .

Hivyo amemtaka rais wa Tanzania waweke mikakati mizito ya kupambana na umasikini nchini Tanzania  

Habari na Victoria Stanslaus


MAENDELEO BENK YAPEWA TANO

 Gadiel Msuya Ameipongeza Benk ya Maendeleo kwa kutoa mkopo wa bajaji kwa Vijana  kwani itawasaidia kwa kiasi kikubwa katika kupata fedha za kujikimu kimaisha ivyo amewataka Vijana wengine kuchangamkia furusa  za Benk ya Maendeleo 

Pia ametoa wito kwa vipngozi wa Benk ya Maendeleo waendelee kufanya hivyo wanavyo fanya kwani kiwango cha asilimia 20 wanachochangia  Vijana kwenye Benk ya Maendeleo kwaajili ya kupata mkopo wa bajaji no sawa 

Habari na Victoria Stanslaus 

HIMANUELI MWAYA ATOA NENO

 Mkuu wa Idara ya Biashara Masoko Benk ya Maendeleo Himanueli  Mwaya amesema richa ya  kutoa Mkopo wa  Bajaji150  . Pia Benk yao ya Maendeleo wanatoa Mikopo  kwa Mamantilie 

Ambako mpaka hivi sasa wameweza kuvifikia vikundi vingi vya Mama nitilie lengo kuu waweze kujikwamua kiuchumi iliwaingize vipato vyao wenyewe . Ametoa wito kwa jamii kuitumia Maendeleo ya Benk 

Habari na Victoria Stanslaus 

 

MAENDELEO BANK YAWAFUTA CHOZI VIJANA

 Joji Wandwalo Mkuu wa  Idara uendeshaji Benk na Tehama amesema wameamua kutoa bajaji 150 kwa Vijana wa Kitanzania lengo la mkopo huu vijana waweze kujiajili wenyewe hili wajikwamuwe kiuchumi 

Joji Wandwalo amewataka watanzania watumie Benk ya Maendeleo ili wapate furusa mbalimbali za mikopo 

Habari na Victoria Stanslaus