Friday 27 May 2022

BRELA KUSHUSHA RUNGU LA KUYAFUTA MAKAMPUNI 5676


 
Afisa Mtenadaji Mkuu wa Brela Godfrey Nyaisa Amesema Tangu uteuzi wangu wa BRELA mojawapo ya changamoto niliyokutana nayo ni uwepo wa makampuni mengi ambayo hayafanyi kazi au shughuli yoyote ya kibiashara katika Daftari la Kampuni. Yapo makampuni yenye miaka zaidi ya 50 na hayana uthibitisho kuwa yanafanya biashara na hayawasilishi taarifa za mwaka (Annual Return) kwa kampuni zilizosajiliwa hapa nchini au mizania ya Mwaka (Financial Statement) kwa kampuni zilizosajiliwa nje ya nchi. 

kifungu cha 128 cha Sheria ya makampuni, sura 212 kinazitaka kampuni zilizosajiliwa hapa nchini kuwasilisha Taarifa za mwaka " Annual Return" ambapo kutofanya hivyo kunatupa tafsiri kuwa huenda kampuni hii haifanyi biashara kulingana na lengo la uanziliashwaji wake.

Kifungu cha 438 cha sheria ya makampuni kinazitaka kampuni zilizosajiliwa nje ya nchi ambazo zina ofisi za biashara nchini kuwasilisha Mizani ya Mwaka (Financial Statement) ambazo kutofanya hivyo pia kunatoa tafsiri kuwa kampuni hizo hazifanyi biashara hapa nchini.

Vifungu vya 400 na 441 vya sheria ya makampuni vinanipa mamlaka mimi kama msajili wa makampuni kufuta makampuni ambayo hayafanyi biashara. uwepo wa makampuni mengi yasiyofanya biashara ni kinyume na sheria na ni mzigo kwa wakala kwa kutunza kumbukumbu za makampuni. Mengi ambayo hayafanyi biashara au yameshikilia majina kinyume cha sheria kwaajili ya kuwauzia watu wengine wenye uhitaji wa majina hayo.

Habari picha na Ally Thabith






habari picha Ally Tabith

Wednesday 25 May 2022

KATIBU MKUU ZAINABU CHAULA ATOA NENO KWA UONGOZI WA TAASISI YA USTAWI WA JAMII


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Zainabu Chakula ameutaka Uongozi wa Bodi ya Magavana wav Taasisi ya  Ustawi wa Jamii kufanya kazi Kwa Uweredi,Uamifu na Ubunifu.  

Pia amewataka kuandaa wahitimu vizuri ili wakimaliza waweze kuajiliwa na kujiajili pamoja na kwenda kutatuwa matatizo yaliyopo kwenye Jamii Lengo watu waache kujinyonga,kunywa simu na kufanya vitendo vya ukatili WA kijinsia  amesema haya Wakati wa Uzinduzi wa Bodi ya Magavana kwenye Taasisi ya Ustawi wa Jamii Kijitonyama jijinidsm.

Habari picha na Ally Thabiti

JOYCE NYONI WA TAASISI YA USTAWI WA JAMII AMPONGEZA WAZIRI DOROTHY NGWAJIMA


 Mkuu wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii Joyce Nyoni amesema anamshukuru Waziri  Dorothy Ngwajima ,Katibu Mkuu Zainabu Chakula ,Naibu Katibu Mkuu Amoni Mpanju pamoja na Uongozi wote wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi maalum kwazi wanayoifanya za kukuza na kuendeleza Chuo cha Ustawi wa Jamii.

Amesema haya Wakati wa Uzinduzi wa Bodi ya Magavana ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii.

Habari picha na Ally Thabiti


Friday 20 May 2022

MKURUGENZI MSAIDIZI KUTOKA WIZARA YA HABARI ,MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI ABAINISHA MIKAKATI

 Peter Mwasalyanda Mkurugenzi Msaidizi wa Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya habari amesema serikali imebadili sheria,kanuni,Sera na miongozo kwenye upande wa Teknolojia lengo kukukza ICT.

Peter Mwasalyanda amempongeza Uongozi wa Huawei nchini tanzania Kwa Juhudi na jitihada wanazozifanya kwenye kukuza ICT .

Habari na Ally Thabiti

RAHUL BHATI MENEJA WA REDINGTON TANZANIA AMESEMA ICT KUKUZA UCHUMI


 Rahul Bhati Meneja wa Redington Tanzania amesema ICT inasaidia  Kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi Kwa Kasi kubwa zaidi na kutatuwa tatizo la Ajira nchini tanzania ,Mfano watu wanavyotumia mitandao ya kijamii Kwa kupashana habari. 

Habari picha na Ally Thabiti

NAIBU MKRUGENZI WA HUAWEI NCHINI TANZANIA TOM TAO AJIVUNIA KUKUZA ICT TANZANIA


 Tom Tao amesema Huawei Wanasaidia kwa Kiasi kikubwa kukuwa Kwa ICT Kwa kutatuwa changamoto mbalimbali na Miradi ya Tanzania kukamilika Kwa alaka na mapema Mfano SGR.

Habari picha na Ally Thabiti

JOSEPHINE MATIRO MKURUGENZI WA HAKI ZA WANAWAKE TAASISI YA WANAWAKE LAKI MOJA AVUTIWA NA UTENDAJI KAZI WA RAIS SAMIA SUHULU HASSAN

 Mkurugenzi wa Haki za Wanawake Taasisi ya Wanawake Laki Moja amempongeza rais Samia Suluhu Hassan Kwa ongezeko la mshahara la asilimia 3.3 kwani itasaidia Kwa kiasi kikubwa kupunguwa Kwa ugumu wa maisha ,kuongezeka Kwa morari Kwa wafanyakazi na uweredi katika kazi.

Ambako raisi amevunja rekodi Kwa mwaka mmoja Kuongeza mshahara kwani ndani ya Miaka Saba mishahara aikuongezwa.

Habari picha na Ally Thabiti

NANGASU WAREMA MKURUGENZI WA MIRADI TAASISI YA WANAWAKE LAKI MOJA KUITANGAZA ROYAL TOUR

 Mkurugenzi wa Miradi ya Maendeleo Kutoka Taasisi ya Wanawake Laki Moja Nangasu Warema na barozi wa Utalii amesema wanamuunga mkono rais Samia Suluhu Hassan kuanziaha Royal Tour.

 kwani itasaidia Kwa kiasi kikubwa Kuongeza idadi ya watalii na wawekezaji kwenye sekta ya Utalii,pia kukuwa Kwa uchumi wa tanzania na kuongezeka Kwa fursa za Ajira Kwa watanzania .

Nangasu Warema amesema Wana mikakati wa kuzunguka nchi nzima kutangaza vivutio vya Utalii wataanza nyanda za Juu Kusini .

Habari na Ally Thabiti

Habari na 

MWENYEKITI WA TAIFA WA TAASISI YA WANAWAKE LAKI MOJA VICKY KAMATA AMUUNGA MKONO RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

 Taasisi ya Wanawake Laki Moja Tanzania Chini ya Mwenyekiti Vicky Kamata wamempongeza rais Samia Suluhu Hassan Kwa Kutoa ruzuku ya fedha kiasi cha bilioni Mia moja kwaajili ya kupunguza ongezeko ya bei ya mafuta, amesema itasaidia Kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa mafuta Kwa bei nafuu na itapelekea kupunguwa bei Kwa vitu mbalimbali.

Amesema yeye na Taasisi Yao wanamuunga mkono rais Kwa hatuwa alioifanya.

Habari na Ally Thabiti

Wednesday 18 May 2022

MAKAMU WA RAIS ATETA NA NIMR

 Dr Philip Mpango Makamu wa Rais Tanzania ameitaka NIMR Kuongeza Kasi kwenye Tafiti wanazozifanya lengo kukabiliana na milipuko ya magonjwa Kwa wakati na ameiagiza NIMR wawe na chanjo zenye kudhibiti magonjwa, pia ameiagiza Tafiti za Dawa za Tiba asili ziwe za kukamilika Kwa wakati na haraka na Matokeo yaonekane lengo tuwe na Dawa za asili  Kwa wingi nchini tanzania.

Makamu wa Rais amesema serikali imejipanga kujenga vituko vya Afya kila Kona ya tanzania kwaajili ya kunusulu vifo Ndio maana imetenga fedha za kutosha kwaajili ya Tafiti mbalimbali. 

Philip Mpango ameipongeza NIMR Kwa Kongamano la 31 la Kisayansi kwani litaibwa mambo mengi ambayo yataleta tija na faida Kwa nchi Yetu ya tanzania.

Habari na Ally Thabiti

CHUO KIKUU SUACHAISHUKURU NIMR KWENYE KONGAMANO LA 31

 Fidelis John Kutoka Chuo Kikuu SUA amemshukuru taasisi ya Utafiti wa Afya NIMR Kwa kufanya Kongamano la 31 kuanzia tarehe 17 na mwisho tarehe 19/2022 kwani Chuo Kikuu SUA kimepata fursa ya kuelimisha watu namna Panya Buku anavyoweza kutambuwa Ugonjwa wa Kifua Kikuu Kwa haraka zaidi .

Fidelis John amesema kupitia Panya Buku Tanzania inaweza  kutibu wagonjwa wa Kifua Kikuu Kwa wakati na haraka tena Kwa gharama nafuu ambako itapelekea pesa nyingi za serikali kuokolewa na vifo vyingi kupunguwa na kutokomeza  Kifua Kikuu.

Fidelis John amesema nchi ya Marawi na Ethiopia Wamechukuwa Panya Buku Kutoka Tanzania kupitia Chuo Kikuu SUA kwaajili ya Kupambana na kutokomeza Kifua Kikuu  kwenye  nchi zao.

Habari na Ally Thabiti


JANICE MAIGE AIPONGEZA NIMR

 Mtafiti wa Ifakara Health Institute Janice Maige amempongeza Taasisi ya Utafiti wa Afya ya Binadamu NIMR Kwa kufanya Kongamano la Kisayansi la 31 kwani itasaidia Kwa kiasi kikubwa kujuwa Mbinu mbalimbali za kuweza kukabiliana na milipuko ya magonjwa na namna ya kupata chanjo ya magonjwa yanayojitokeza nchini Tanzania na Duniani.

Janice Maige amesema Taasisi ya Ifakara Health Institute inafanya TAFITI kwenye upande wa Mareria Mfano Rufiji wamepunguza Mareria Kwa asilimia 34,upande wa Ukimwi na wanatoa elimu na Mafunzo kwenye matumizi ya Lishe Bora .

Habari na Ally Thabiti

TCRA YAISHANGAZA DUNIA

 Mwandisi Kisaka wa TCRA amesema Wameamuwa kukutana na Wanahabari wanaoandika habari za mtandaoni lengo kuwatambuwa na kuthamini mchango wao , na kuwataka wawe wanahandika habari za Miradi na Matukio Tu.

Mwandisi Kisaka Kutoka TCRA amewataka wanahabari wanaoandika habari za mtandaoni wazingatie sheria,kwanini na taratibu za Tanzania na Maadili ya nchi , huku akiwataka wafuate mizania wakati wa kuandika habari zao amesema haya jijini dsm makao makuu ya TCRA Ubungo wakati WA Mafunzo na Wanahabari wanaoandika habari za mtandaoni.

Habari na Ally Thabiti

MWANAHABARI AIPONGEZA TCRA


 Tunu Mwanahabari wa Tanzania Yetu Tv amesema anaipongeza na kuishukuru Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kwa kuwapa Mafunzo na kuwajengea uwezo wanahabari wa mtandaoni , Kwani wameweza kuzitambuwa sheria nakanuni za TCRA na kuepukana na hadhabu walizokuwa wanakutana nazo . 

Habari  Picha na Ally Thabiti

Tuesday 17 May 2022

ASASI ZA KIRAIA ZINAMATUMAINI MAKUBWA


 Mratibu wa Asasi za Kiraia amesema wanamatumaini makubwa ya Utendaji kazi wa rais Samia Suluhu Hassani na wasaidizi wake wa Wizara akiwemo Waziri Dorith Ngwajima na Katibu Mkuu Zainabu Chakula.

Habari picha na Ally Thabiti

MWENYEKITI WA ASASI ZA KIRAIA AIPONGEZA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ,JINSIA,WATOTO,WAZEE NA MAKUNDI MAALUM


 Liliani Mwenyekiti wa Asasi za Kiraia amesema Wizara ya Maendeleo ya Jamii imefanya kazi kubwa ya kuziunganisha Asasi zote za Kiraia nchini Tanzania, ambako Asasi hizi zimekuwa na Uhuru mkubwa wa kufanya kazi nchini.

 amemshukuru Waziri Dorith Ngwajima na Katibu Mkuu Zainabu Chakula Kwa Ushirikiano na utendaji kazi wao mzuri na ulio tukuka Kwa Asasi za Kiraia za Kitaifa na kimataifa .

Habari picha na Ally Thabiti

MRATIBU WA THRDC ATOA NENO


 Abdalla Abedi Mratibu wa THRDC Zanzibar amesema katika kufikisha Miaka 10 ya THRDC wameweza kunufaika Kwa kiasi kikubwa Kwa majaji na mahakimu wa Zanzibar Kwa kujengewa uwezo wa Uendeshaji wa kesi ambako imepelekea kupunguwa Kwa mrundikano wa kesi Zanzibar.

Pia wameweza Kutoa magodoro na elimu kwenye chuo cha Mafunzo .

Nae Kwa upande wake Waziri wa Latina na Sheria Dr Damasi Ndumbalo amempongeza rais Samia Suluhu Hassani Kwa kuwa mtetezi namba moja wa haki za binadamu kwenye sekta zote . 

Huku Mratibu wa THRDC Onesmo Ole Ngurumo amemongeza rais Samia Suluhu Hassani Kwa Juhudi na jitihada anazofanya katika uongozi wake Kwa kuzingatia misingi ya haki za binadamu .

Habari picha na Ally Thabiti

JAJI MSTAAFU TOMASI MIHAYO APONGEZA JUHUDI ZA RAIS SAMIA SULUHU HASSANI


 Jaji Mstaafu Tomasi  Mihayo amesema Kitendo cha rais Samia Suluhu Hassani kuzinduwa Loyo Tuwa itasaidia Kwa kiasi kikubwa kuongezeka Kwa Ajira,kukuwa Kwa uchumi na kuimarika na kukuwa sekta ya Utalii Tanzania .

Jaji Mstaafu Tomasi Mihayo amewataka watu kumuunga mkono rais Samia Suluhu Hassani Kwa vitendo. 

Habari picha na Ally Thabiti

MKURUGENZI MTENDAJI WA BODI YA UNUNUZI NA UGAVI ATANGAZA VITA KALI


 Godfred Mbanyi Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalam wa  Ununuzi na Ugavi (PSPTB) amewataka Waajiri nchini Waajili wataalam wa Ununuzi na Ugavi wenye sifa na waliosajiliwa na PSPTB lengo kuwa na wataalam wenye uweredi zaidi.

Ambako itasaidia kuondokana na upotevu wa fedha mpaka kupelekea serikali kupoteza mapato na hatinaye kukosa kukusanya Kodi,  Godfred Mbanyi amewataka wataalam wa Ununuzi na Ugavi kujisajili kwenye PSPTB .

 Yeyote atakae puuza maagizo haya hatuwa Kali za kisheria zitatumika  Ikiwemo kutozwa faini  milioni mbili na kwenda jera miakamiwili.

Mkurugenzi wa PSPTB amesema wameamuwa kuja na kampeni kwenye vyombo vya habari lengo Kutoa elimu Kwa Jamii umuhimu wa kuwaajili maafisa Ununuzi na Ugavi waliosajiliwa na PSPTB.

Habari na Ally Thabiti

Sunday 1 May 2022

COSOTA YAGUSWA NA WATU WENYE ULEMAVU


 Mkurenzi mtendaji wa COSOTA, DORIS SINALE amesema kupitia mkataba wa MARA CASH utasaidia kiasi kikubwa watu wenye ulemavu kuweza kupata haki ya kuchapisha vitabu mbalimbali na majalida kupitia maandishi ya Nukta nundu kwaaajili wasioona lengo la COSOTA ni kuyafikia makundi yote.


Habari picha na Ally Thabit

WILAYA YA MKURANGA YAMUUNGA MKONO RAIS SAMIA.

 


KHADIJA NASRI ALI Mkuu wa Wilaya ya mkuranga mkoa wa pwani amesema katika mbio za mwenge ambako wilaya ya mkuranga itatembekewa na mwenge tarehe 03/05/2022 ambapo jumla ya miradi saba itazinduliwa na mingine itawekewa mawe ya msingi thamani ya miradi hii ni kiasi cha Bilioni saba nukta sita (7.6) Bi. Khadija Nasri Ali amesema wanapongeza juhudi na jitihada za utendaji kazi za Raisi Samia Suruh Hassan ndio maana wilaya yake ya mkuranga itakeleza kwa vitendo maagizo na maelekezo ya Rais Samia Suruh Hassan ikiwemo uzinduzi wa msitu wa vikindu ambao watalii zaidi ya mia tano (500) hutembelea kila mwezi na ujenzi wa miundo mbinu sehemu za kihistoria. Bi Khadija Nasri Ali ametoa wito kwa watu wote kumuombea Rais Samia Suruh Hassan na kumuunga mkono kwa moyo na vitendo pia ametoa rai kwa wanamkuranga na watanzania kwa ujumla kulinda na kudumisha amani iliyopo nchini Tanzania.

Habari Picha na Ally Thabiti