Tuesday 28 June 2022

RAIS SAMIHA HASSAN SULUHU AWAPA TUZO GLOBAL LINK EDUCATION




Rahisi Samiha Suluhu Hassani  amesema anatambua mchango na jitiada zinazofanywa na Global Link Education nchini Tanzania kwa kuwatafutia kijana wa Kitanzania wa Bara na Zanzibar vyuo vya gharama nafuu, usalama na vyenye elimu bora vya Kimataifa nchi za nje ndiyo maana ameamua kuwapa tuzo Global Link Education akiwa Zanzibar.

Rais Samiha Suluhu Hassan amewataka wazazi na walezi kuwatumia Global Link Education kwa elimu bora kwani awana ubabaishaji.

Habari picha na 

Ally Thabiti.

ABDULMALIKI MOLLEL ATETA NA WAZIRI WA ELIMU ZANZIBAR




Mkurugenzi Mtendaji wa Global Link Education amesema wanawapa fulsa wanafunzi wa Zanzibar kwenda kusoma vyuo vya nje amemueleza Waziri wa Elimu wa Zanzibar waitumie Global Link Education katika kuwaunganisha na vyuo vya nje kwani awatajuta. Nae waziri wa Elimu wa Zanzibar amempongeza na kumshukuru mkurugenzi wa Global Link Education Abdulmalik Mollel kwa kuwapa fulsa na kuwafungulia milango kwakwenda kusoma nje ya nchi watu wa Zanzibar.

Habari Picha na 

Ally Thabiti

GLOBAL EDUCATION KUTEKELEZA PLOGRAME HEET PROJECT KWA VITENDO


 
Mkurugenzi Mtendaji wa Blogal Link Education Abdulmalik Mollel ameitoa hofu Serikali kwenye HEET Project kwa wahaziri ambao wataenda kusoma nje ya Nchi kwani watatafutiwa vyuo vya gharama nafuu, usalama wa uwakika na ufuatiliwaji wa kozi watakazo maliza.

Abdulmalik Mollel ameiakikishia serikali nafasi za kwenda kusoma wahaziri nje ya nchi wapewe wao Global Link Education kwani ni wazoefu wa masomo kuanzia miaka ya zamani mpaka leo na hawana ubabaishaji hivyo hata kwa elimu za ndani Global Link Education ni wakongwe.

Amesema haya kwenye uzinduzi wa HEET PROJECT uliofaziliwa na Benk ya Dunia kwa miaka mitano yenye samani ya Bilioni 942 fedha za kitanzania.

Habari picha na.

ALLY THABITI

AFISA UHAMIAJI MSAIDIZI AWAPA TANO TANTRADE

Afisa Uhamiaji Msaidizi amempongeza TANTRADE Kwa Kutoa semina elekezi Kwa washiriki Kutoka nje ya nchi,Pia amesema VIsa ni bule Kwa wanachama wa Africa Mashariki 

Amesema haya kwenye maonyesho ya 46 viwanja vya Saba Saba  ambako kauli mbiu inasema TANZANIA NI SEHEMU SAHIHI KWA BIASHARA NA UWEKEZAJI..
Habari na Ally Thabiti 

FORUM CC YAJA NA MIKAKATI YA KUTUNZA MAZINGIRA

 Msololo Onditi Afisa Miradi FORUM CC amesema mikakati Yao ni Kutoa elimu Kwa Jamii namna ya Kutunza mazingira Kwa njia ya upandaji miti. pia wanaenda mashuleni na Wanawatumia mawakala 70 kwenye mikoa yote Tanzania.

Habari picha na Ally Thabiti

Sunday 26 June 2022

JAMII YAOMBWA KUWATHAMINI WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU.

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mkoani Dar es salaam Godwin Gondwe ameitaka jamii kuwathamini watu wenye mahitaji Maalumu ikiwemo Walemavu kwani wanapaswa kupatiwa haki kama watu wengine.


Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe (mwenye Miwani) akiangalia ubunifu wa kazi  za sanaa zilizofanywa na Watoto wenye Mahitaji Maalum.

DC Gondwe ametoa rai hiyo wakati wa tamasha la Watoto wenye Mahitaji Maalumu lililoandaliwa  na Kijiji Cha Makumbusho ya Taifa  lenye ujumbe usemao"Haki Sawa Kwa Wote" lengo ni kuwakutanisha Watoto wenye mahitaji mabalimbali ikiwemo ulemavu wa viungo na walemavu wa ngozi( Albino).

Aidha amesema kwamba Watoto wenye mahitaji maalum wanatakiwa,kutambuliwa, kuthaminiwa na kupatiwa haki zao za msingi ikiwemo elimu ili kuwafanya waweze kuishi katika maisha bora ,huku akikemea jamii kuacha  vitendo vya unyanyapaa kwa Watoto hao.

" Nakipongeza Kijiji Cha Makumbusho ya Taifa  kwa kuandaa tamasha hili ambalo limelenga kutambua thamani ya Watoto wenye ulemavu,natoa wito kwa jamii,taasisi na mashirika mbalimbali kuendelea kuwathamini watu wenye ulemavu" amesema DC Gondwe.

Watoto wenye ulemavu kutoka shule mbalimbali za msingi ikiwemo shule ya Mgabe,Shule ya Msingi mchanganyiko,Shule ya Msingi Jeshi la Wokovu ,wamekutana kwenye tamasha hilo nakuweza kushiriki Mambo mbalimbali ikiwemo michezo na burudani.

Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Kijiji Cha Makumbusho Bi.Wilhelmina Joseph amesema kwamba Makumbusho ya Taifa itaendelea kuthamini makundi mbalimbali ya jamii ikiwemo Watoto wenye mahitaji mbalimbali ili kuwafanya wapate haki zao za msingi.
Watoto wenye Mahitaji Maalum wakionyesha burudani kwenye Tamasha la Watoto wenye Mahitaji Maalum lililoandaliwa na Makumbusho ya taifa Mkoani Dar es salaam.
'
"Tumeandaa tamasha hili ili kuthamini haki za Watoto hawa ,hivyo sisi Kama Makumbusho ya Taifa tumeandaa tamasha hili la Watoto wenye mahitaji Maalumu na tukaweka kauli mbiu ya Haki Sawa kwa Wote" ili kuifanya jamii itambue kuwa hata watu wenye ulemavu wana haki sawa na wengine hivyo wasiwafiche majumbani" amesema Bi Wilhelmina.

Akizungumza kwa niaba ya Walimu Wenzake kutoka shule hizo Bw.Emanuel Ibrahim kutoka shule ya Msingi ya Jeshi la Wokovu ( Salvation Army) amesema kwamba ulemavu siyo kushindwa hivyo wameiomba Makumbusho ya Taifa kulifanya tamasha hilo kuwa endelevu.

Habari Picha na Ally Thabiti

HAKIELIMU YAPONGEZA BAJETI YA SERIKALI



 


Habari picha na Ally Thabit

AMOS MAKALA AWATAKA WATUMISHI WALIOKULA BILIONI KUMI WAZITAPIKE


 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam ametoa maagizo na maelekezo ndani ya siku saba mkurugenzi wa jiji la Ilala, watumishi kumi na tisa na mawakala wa ukusanyaji taka watoe maelezo ya kiasi cha bilioni kumi zilivyopotea na amewataka ndani ya siku sitini kiasi hicho cha fedha cha bilioni kumi ziwe zimerejeshwa Amos Makala Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam amewataka madiwani kusimamia kwa uweredi fedha za serikali nae naibu meya wa jiji la ilala Sadi Kimji amemwahidi mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam watasimamia na kutekeleza maagizo na maelekezo aliyoyatoa.

habari Picha na Ally Thabiti

DSTV YAJA KIVINGINE


 Mtendaji mkuu wa DSTV LEONARD SHELUKINDO amewataka watu kutoa 9900/= ili kuwangalia vipindi bora vya DSTV.

Habari na Ally Thabith

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM ATOA MAAGIZO MATANO

 AMOS MAKALA, amewataka wenyeviti wa serikali za mtaa, watendaji, madiwani na mamea kuhakikisha wanawaondoa wamachinga maeneo yasiyofaa kwa biashara, kusimamia usafi.

Habari kamili na Ally Thabith 

MKURUGENZI WA TANTRADE AKUTANA NA WANAFANYA BIASHARA



 Latifa Mohamed Hamisi, Mkurugenzi mkuu wa TANTRADE amesema maonyesho ya ALBAINI NA SITA (46) ya Sabasaba yatakayofanyika tarehe 28/06/2022 yatakuwa yenye  kufana na mafanikio makubwa ambapo nchi zaidi ya sabini (70) zitashiriki na kwa wafanya biashara watanzania wataonesha bidhaa zao amewataka watu kujitokeza kwa wingi kwenye viwanja vya sabasaba kwani kiingilio ni nafuu na miundo mbinu yote imeboreshwa pia kutakuwa na makongamano ya aina mbalimbali lengo kuwatafuia fursa wafanyabiashara wa kitanzania na wageni kutoka nchi za nje kuwaonesha fursa za uwekezaji nchini Tanzania ambako kauli mbiu kwa mwaka huu inasema "Tanzania ni mahali sahihi kwa usalama wa biashara na uwekezaji". Bi. Latifa Amesema haya kwenye semina iliyowakutanisha wafanya biashara watakao shiriki kwenye maonesho ya sabasaba. Maada zilizowasilishwa ni Afya, ambaye aliwasisha Rehema kutoka halmashauri ya Temeke amesisitiza na UVICO 19 ambako chanjo zinapatikana za UVICO 19. Wa pili, Loyce Kibuta, Ameelezea namna ya kujikinga na majanga ya moto na jinsi yakutumia vifaa vya kuzimia moto nawataka watu kupiga namba 114 la jeshi la zima moto kwaajili ya msaada.

Abdallah Seif Abdallah amewataka wafanyabiashara kutoa risiti na wanunuaji wa bidhaa kudai risiti ambaye atatoa risiti atapigwa faini ya shinilingi milioni tatu mpaka milioni nne na nusu na atakae nunua kitu bila kudai risiti atatozwa elfu thelathini mpaka milioni moja na nusu.

Nora wa Tantrade amezungumzia tuzo za banda bora ambazo zitakuwa na category 26 nae SUDI afisa biashara wa Tantrade amezungumzia mfumo wa vibali.

Kwa upande wake Masha amezungumzia kanuni za ushiriki 

Haya ndiyo ambayo yamezungumziwa kwenye semina kati ya Tantrade na washiriki wa maonyesho ya sabasaba.

habari Picha na Ally Thabith

Friday 24 June 2022

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI AIPONGEZA MAKUMBUSHO YA TAIFA

 Godwin Ggondwe amesema Kitendo cha MAKUMBUSHO ya TAIFA ya Kijito nyama  Kwa kufanya tamasha la watoto wenye maitaji maalum ni Jambo zuri  Kwani watu wenye ulemavu Wana haki sawa Amesema wilaya ya kinondoni inawathamini watu wenye ulemavu wote.

Kwa kuwapa elimu na Huduma zinginezo.

Nae Kwa upande wake Afisa elimu wa Makumbusho Wilhimina Josephu amesema ili ni tamasha la 34 amesema wameamuwa kuwakutanisha watoto wenye ulemavu lengo kuonyesha Wana haki Sawa na watoto wengine.

Pia amesema Makumbusho ya Taifa kuna miudombinu rafiki na wezeshi Kwa watu wenye ulemavu,swala la kuandika vipeperushi Kwa nukta nundu wamelibeba watalifanyia kazi.

Mwanafunzi Teresa wa darasa la sita shule ya misingi Kesho la wokovu kwaniaba ya watoto wenye ulemavu wamempongeza Makumbusho ya Taifa Kwa kuwajali na kuwathamini ivyo wameaidi watakuwa mabarozi Kwa Jamii .

Lengo watoto wenye ulemavu wapelekwe shule wakasome .

Habari na Victoria Stanslaus

Wednesday 15 June 2022

TGNP YAWATAKA WANAHARAKATI KUPAZA SAUTI KWENYE BAJETI YA TILIONI 41.48

Mkurugenzi mtendaji wa TGNP Liliani Liumbi amesema bajeti iliyowasilishwa na Migulu Lameck Nchemba haijazingatia mlengo wa kijinsia hivyo amezitaka hasasi za kiraia nchini Tanzania na wanaharakati kuweka nguvu ya pamoja katika bajeti ijayo lengo izingatie mlengo wa kijinsia. TGNP imepongeza serikali kwa kufuta ada ya kidato cha tano hadi cha sita na kufanya elimu ya msingi mpaka kidato cha sita kuwa bure.

habari Picha na Ally Thabith
 

BAJETI YA TILIONI 41.48 YAWASILISHWA NA WAZIRI WA FEDHA MWIGULU NCHEMBA


Waziri wa fedha na mipango Mwigulu Lameck Nchemba amesema bajeti ya Tilioni 41.48 itakuwa mkombozi kwa watanzania kwani kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha sita elimu ni BURE, pia mabadiliko ya sheria kumi na tisa zimepitishwa kwenye bajet hii huku sekta ya kilimo, Afya, maji na miundo mbinu mfano barabara zimetengewa fedha za kutosha.

habari picha na Ally Thabith

TAIFA WAZIRI DORITHY GWAJIMA AJA NA BAJETI YA KIMKAKATI

 

Kiasi cha fedha bilioni 43.4 imetengwa kwenye wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na makundi maalum. 

Waziri Dorithy Gwajima amesema kiasi hichi cha fedha kinasaidia katika kupambana na ukatili dhidi ya watoto ambako zaidi ya asilimia 60 watoto wanafanyiwa ukatili majumbani kwao na asilimia 40 mashuleni, waziri Dorithy Gwajima amesema fedha hizi zitaimarisha maafisa ustawi na watendaji wengine.


Habari picha na Ally Thabith