Thursday 23 February 2023

TAASISI YA AG GENERGIES YAWATAKA WANANCHI KUTUMIA BIDHAA ZAO

MUSSA IBRAHIM ni mkurugenzi wa Kampuni ya AG ENERGIES amewataka watanzania na wasio kuwa watanzania kutumia bidhaa zao za Solar na kila mtu anapata solar kulingana na solar yake, pia wanamahospital na mahotesl

Habari kamili na Victor Stanslaus

RISHIT RADIA MKURUGENZI

 Mkurugenzi Rishit Radia Mkurugenzi mkuu wa kiwanda cha kahawa amesema wanafanya kazi na wakulima zaidi ya 800 kiwanda cha kusaga na kusafisha alafu wanapaki kwenye paketi

ujazo milimita 250 wanaweka kwenye gunia kilo 60 kwaajili ya kahwa inaladha tamu, watu wanje wanafurahia pamoja na wakulima wameenea Tanzania nzima na kimataifa zaidi. kiwanda kipo talime

Haya yamesemwa na mkurugenzi wa kiwanda cha NORTHERN HIGHLANDS COFFEE COMPANY

Habri kamili na Victoria Stanslaus

Madaktari bingwa wa MOI wapewa mbinu za kisasa za upasuaji wa vivimbe vya mishipa ya damu kwenye ubongo.

 



Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya  na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) zimeanza kutoa  mafunzo maalum ya upasuaji wa  vivimbe vya mishipa ya damu kwenye ubongo kwa mbinu za kisasa kwa madaktari bingwa waliohitimu katika chuo hicho ambapo wagonjwa 4 wamefanyiwa upasuaji huo.

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface  amesema mafunzo hayo yanaongozwa na Mkufunzi maalum kutoka hospitali ya St. Luke`s, Ugiriki kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutoa matibabu ya kibobezi.

“Mafunzo haya ni endelevu ambapo wataalam wetu  watafundishwa upasuaji wa vivimbe vya mishipa ya damu kwenye ubongo kwa mbinu za kisasa  ambapo mpaka sasa wagonjwa wanne kati ya saba waliopangwa wameshafanyiwa upasuaji huo” amesema Dkt. Boniface

Aidha,  Dkt. Boniface ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongwa na Rais  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya kwani zaidi ya Millioni 50 zimeokolewa kama wagonjwa hao wangetibiwa nje ya nchi.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa Ubongo  na  Mishipa ya Fahamu Dkt. Nicephorus  Rutabasibwa amesema Madaktari bingwa watatu wa MOI waliohitimu Chuo cha MUHAS watafundishwa mbinu za kisasa za na za kibobezi zakutibu magonjwa ya  mishipa ya damu kwenye ubongo.

“Mafunzo haya yamegawanyika katika sehemu nne ambapo tunalengo la kuwafanyia wagonjwa  40 katika kipindi cha mwaka mmoja kwa ajili ya  kuwajengea uwezo wataalam wetu ili baadae wawafundishe wenzao waliopo katika hospitali mbalimbali nchini” amesema Dkt. Rutabasibwa

Naye, Mtaalamu Bingwa Mbobezi wa Mishipa ya damu kwenye Ubongo kutoka hospitali ya St. Luke`s kutoka Ugiriki Prof. Athanasios Petridis amesema anafuraha kubwa kuwa MOI na kutoa mafunzo ya kibobezi ya upasuaji wa kuzibua vivimbe vya mishipa ya damu kwenye ubongo na  baada ya mafunzo hayo wataalam hao watakuwa na uwezo mkubwa wa kufanya upasuaji huo.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa Ubongo Dkt. John Michael Mtei  ameushukuru uongozi wa Taasisi ya MOI kwa mafunzo hayo kwani yamewajengea  uwezo  wa kutibu magonjwa ya mishipa ya damu kwenye ubongo .

habari picha na Victoria Stanslaus

Friday 17 February 2023

Picha: Rais Samia amewasili Addis Ababa nchini Ethiopia

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amewasili Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU)




MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AWATAKA TANROADS NA TARURA KUTEKELEZA MIRADI

Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala amewataka TANROADS na TARURA kutekeleza ujenzi wa Barabara zilizopo ndani ya mkoa wa Dar es Salaam kwani mbunge wa Mbagala Chaurembo amesema katika jmbo lake la mbagala kwa kiwango kikubwa barabara bado hazijatengenezwa nae mbunge wa kibamba amelalamikia kutopewa kipaumbele barabara zake. Huku Mbunge Bona Kalua akiwataka TARURA waeleze lini watatengeneza barabara kwenye jimbo lake na wathibitishe kama pesa wanazo nae Mbunge Ndungulile wa Kigamboni akitoa kilio kuhusu ujenzi wa barabara wa mwendo kasi katika jimbo lake la kigamboni.

Meneja TARURA amesema barabara za DMDP zitajengwa katika jiji la Dar es Salaam kwani Benki ya Dunia iko Tayari kutoa hizo fedha na michakato imeanza hivyo ifikapo mwezi 11-2023 miradi ya barabara itatekelezwa kwa vitendo. Amewatoa hofu wabunge na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa TARURA itatekeleza kwa vitendo na sio kwa maneno.

Habari kamili na Ally Thabith

RIDHIWANI AGAWA PIKIPIKI KWA WATENDAJI WA KATA SITA NA KUPOKEA

 


Naibu Waziri wa Ardhi ambae pia ni mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amegawa pikipiki kwa watendaji wa kata 6 za Halmashauri ya Chalinze, pamoja na kutembelea kiwanda cha Uzalishaji wa marumaru cha Keda.

Pia, amepokea vifaa tiba kwa ajili ya Vituo Vya Afya kwa ajili ya Vituo Vya Afya Viwili Kata za Kibindu na Msata na Zahanati vijiji 11.

Akigawa Pikipiki hizo, Ridhiwani amewakumbusha Watendaji kutumia vifaa hivyo kwa kuzingatia makusudio ya kutolewa kwa vyombo hivyo vya moto ikiwemo kwenda kusikiliza wananchi na kutoa ufumbuzi wa changamoto zao.

Vilevile akikabidhi vifaa tiba wamehimizwa kuvitunza na kuvitumia kwa makusudio vifaa hivyo.

"Kazi kubwa inaelekezwa kituo cha Afya Miono ambapo kazi ya ujenzi wa miundo mbinu inapaswa kuwa kipaumbele";: Kwa upande wa kiwanda tumewashukuru wawekezaji kwa kutambua mchango wa Raisi Dkt. Samia Suluhu #KaziInaendelea

Habari Picha na Ally Thabith

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AKUTANA NA VIONGOZI WA CCM NA WASERIKALI

 Amos Makala Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam tarehe 15/02/2023 amekutaka na viongozi wa ccm mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam wa ngazi zote pamoja na viongozi wa Serikali wa Mkoa wa Dar es Salaam wakiwemo wakuu wa wilaya, wakurugenzi na wakuu wa idara mbalimbali lengo kuweka mikakati ya maendeleo ya chama cha mapinduzi kwa kuitekeleza kwa vitendo, pia waweze kutambuana kwani ni wapya.

Habari kamili na Ally Thabith

Thursday 16 February 2023

MBUNGE WA KAWE AWATAKA WATU WENYE ULEMAVU KUCHANGAMKIA FURSA

 Askofu Gwajima Mbunge amewataka watu wenye ulemavu waende kwenye almashauri wapate mkopo wa asilimia mbili (2%).

Habari kamili na Ally Thabith 

Sunday 12 February 2023

RC Makalla afunguka kuhusu Machinga na Bodaboda kwenda Afrika Kusini

 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam CPA Amos Makalla ametoa tamko rasmi kwa Viongozi wa machinga na bodaboda kwenda ziara ya mafunzo Afrika ya Kusini, ameyasema hayo leo Februari 11,2023 katika Ukumbi wa DMDP Ilala wakati akipokea taarifa kwa Viongozi hao baada ya kurejea kutoka ziara ya mafunzo nchini Rwanda.

CPA Makalla amesema amefurahishwa na matokeo ya ziara ya mafunzo waliyoifanya 

nchini Rwanda kufuatia taarifa waliyoiwasilisha kwake.

Aidha CPA Makalla amefafanua kuwa miji ya Cape Town na Johanesburg Afrika ya Kusini ni miji katika tano bora kwa usafi Afrika hivyo ziara ya mafunzo nchini humo itapelekea kuleta mapinduzi makubwa zaidi ya Kampeni ya Usafi Jijini Dar es Salaam.

CPA Makalla amewataka Viongozi wa Machinga na Bodaboda kuitisha makongamano kushirikisha elimu waliyoipata nchini Rwanda kwa wanachama wao ili kuwa na uelewa wa pamoja ambao utalifanya Jiji la DSM kusonga mbele katika mikakati yake.

Hata hivyo CPA Amos Makalla amesema “Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuyalea makundi haya kufanya Kazi vizuri anachokifanya yeye katika Mkoa ni utekelezaji kwa vitendo maelekezo na maono ya Mhe Rais”- RC Makalla

CPA Makalla amewahakikishia Viongozi wa Machinga na Bodaboda kuendelea kuwapatia ziara za mafunzo kwa kadri inavyo wezekana kwa kuwa kuelimishana ni njia pekee na bora ya kuleta mabadiliko chanya.


Habari picha Ally Thabit

Picha: Ajali yaua mmoja, majeruhi 7 “Basi lilifeli breki na kutumbukia korongoni

 

Mtu mmoja amefariki Dunia na wengine Saba kumjeruhiwa katika Kata ya Sigino Wilayani Babati Mkoani Manyara baada ya gari la abiria aina ya Costa kufeli breki na kutumbukia katika korongo.

Akizungumza na Ayo TV kwa njia ya simu kuthibitisha tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara Acp George Katabazi amesema gari hilo lilikuwa likitokea Mkoani Singida kuelekea Arusha na baada ya kufika eneo la 

Kona ya Logia ndipo likafeli breki na kumshinda dereva.

“Ajali imetokea asubuhi gari lilikuwa na watu 29 abiria ni 27 dereva mmoja pamoja na utingo wake, dereva amefariki huku majeruhi wakiwa 7 ambapo kati yao watatu hali zao ni mbaya ila abiria wengine walipata mshtuko tu, chanzo cha ajali ni kufeli kwa mfumo wa breki wa gari hali iliyopelekea kumshinda dereva kulimudu gari hilo na kuingia kwenye korongo”-RPC Katabazi

Habari picha na Ally Thabit

Rais Samia afunguka “akikupa Stress achana nae, maisha yako ni zawadi pekee Mungu amekupa




Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu amewasihi Wanafunzi wa Vyuo kuweka mkazo kwenye masomo na maisha yao na kujiepusha na mambo ambayo yatawarudisha nyuma na kusema hata kama Mtu ana Mpenzi ambaye anampa mawazo ni bora kuachana nae kwasababu kupigania maisha ni muhimu kuliko kupigania upendo wa kuharibiana maisha.

Rais Samia amesema hayo leo wakati akizungumza na Wawakilishi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) na Zanzibar (TAHLIFE) leo February 11,2023 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma “Nimuombe Mungu awashushie wote baraka mfanikiwe na yale mnayofanya, mnaosoma msome vema ile kurudia mwaka isiwepo, uki-disco usirudishwe nyumbani lakini kwanini udisco Mwanangu kwanini udisco kama kuna Mtu anakutia mawazo sio ebu achana nae angalia maisha yako kwanza”

“yapo tumetoka huko, inawezekana kuna lijitu huko kila ukigeuka lipo ukigeuka lipo linakusumbua achana nae, your life is yours ni zawadi pekee Mungu amekupa, chunga maisha yako haya mambo mtakutana nayo mbele, pale utatafuta unayeweza kuishi nae
vizuri”

“Kwa sasa chunga maisha yako usimpe Mtu mwingine nafasi ya kukuharibia maisha yako hapana, hakuna upendo wa kuharibiana maisha, akisema ‘nitakufa juu yako’ akafe umuone, nitakufa juu yako chozi linamtoka unamwambia kajinyonge haendi asikuharibie maisha, someni kwa bidii lakini msiacha kumtegemea Mungu”.


Habari picha na Ally Thabit

Mkali wa Amapiano Musa Keys akifanya Soundcheck, kuimba live Usiku wa leo Eleme

 



habari picha na Ally Thabith

RAIS MSTAAFU DKT. KIKWETE AONGOZA KAMATI YA UANGALIZI YA SADC NCHINI

 Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Panelof Elders, POE) ameongoza Ujumbe wa Kamati ya Uangalizi ya SADC inayofuatilia Utekelezaji wa Makubaliano ya Amani nchini Lesotho katika ziara nchini humo tarehe 08 – 11 Februari 2023.

 

Ziara ya Kamati hiyo ya Uangalizi ni utekelezaji wa agizo lililotolewa na Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC katika Mkutano wa 42 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika Kinshasha, DRC mwezi Agosti 2022 ambapo walilielekeza Baraza hilo la Wazee la SADC kufuatilia kwa karibu jitihada za usuluhishi wa migogoro inayoendelea kwa muda mrefu katika Falme za Lesotho na Eswatini.

 

Rais Mstaafu Kikwete ameongozana na Makamu wa Rais Mstaafu wa Mauritius,

Paramasivum Vyapoory, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo la Wazee 

amepata wasaa wa kukutana na Mtukufu Motlotlehi Letsie III, Mfalme wa Lesotho, viongozi wakuu wa Serikali ya Lesotho pamoja na wadau wengine muhimu katika mgogoro huo.

 

Kamati pia imepata fursa ya kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Lesotho ambaye ndiye Mkuu wa Serikali, Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Haki, Sheria na Masuala ya Bunge, Spika wa Bunge, Makamu Rais wa Seneti, Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Mabadiliko, Viongozi wa Vyama vya Siasa vya Upinzani vilivyo Bungeni, Vyama vya Siasa vilivyo nje ya Bunge, Wawakilishi wa Asasi za Kiraia, Askofu Mkuu wa Baraza la Kanisa la

Kikristu nchini Lesotho pamoja na Mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Marekani, Uingereza, AfrikaKusini na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa.

 

Katika mikutano yote iliyofanyika, Kamati hiyo imesikiliza kwa kina maoni ya wadau hao wote kuhusu namna bora zaidi ya kuweza kuendeleza kazi nzuri ambayo tayari imeshafanyika katika kupata suluhu ya kudumu ya mgogoro uliopo nchini humo. Kamati hiyo inaripoti kwa Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC Organ Troika) ambaye kwa sasa ni Hage Geingob,Rais wa Namibia.

OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAWANOA MAAFISA WA SERIKALI MPAKANI


Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Dustan Shimbo leo Februari 11, 2023 akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (Kanuni za Kudhibiti Kemikali Zinazoharibu Tabaka la Ozoni), 2022, katika siku ya pili mafunzo kwa maafisa wa Serikali waliopo katika mpaka wa Horohoro mkoani Tanga, kuhusu udhibiti wa uingizaji nchini wa gesi na vifaa vyenye gesi zinazomong’onyoa tabaka la ozoni.

MAWAKALA TIGOPESA WAJINYAKULIA ZAWADI ZA MAMILIONI YA PESA

KANISA LA TAG LATIMIZA MIAKA 50

Mchungaji Taitas Kamani wa kanisa la TAG wila ya Ilala amesema kanisa hili lilianza mwaka 1973 hivyo wanajivunia mafanikio mbalimbali ikiwemo kuhudumia gereza la watoto.

Habari kamili na Ally Thabith

Saturday 11 February 2023

UONGOZI WA BODABODA NA WAMACHINGA WAKABIDHI TAARIFA NZITO KWA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Uendesha bodaboda na bajaji ndug. Saidi amemueleza mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala, ziara walioenda nchini Rwanda imekuwa ni nzuri kwani wamejifunza namna ya udhibiti ajali ya bodaboda namna ya kuzingatia sheria barabarani nae mwenye wa machinga Namoto Yusuph Yusuph amesema elimu walioipata kwenye nchi ya Rwanda watawapa wamachinga mkoa wa Dar es Salaam ili vipato vyao vikue na mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amewataka viongozi wa machinga, bodaboda na bajaji waanze kutoa elimu kupitia makongamano.

Habari Kamili na Ally Thabith

Thursday 9 February 2023

CUFF YALIA NA WALIOWEKA FEDHA NCHINI CHINA

 

(CUF- Chama Cha Wananchi)

 


 
Office of the National Chairman

P.O. BOX 10979 Dar es Salaam, Tanzania

E-mail: lipumba@yahoo.com

 

TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI, 08 FEBRUARI 2023

SAKATA LA FEDHA ZA PLEA BARGAINING ZILIZOKUSANYWA NA AFISI YA  MWENDESHA MASHTAKA (DPP) NA UCHUNGUZI WA KILE KILITOCHOKEA MPAKA BAADHI YA FEDHA HIZO KUTOJULIKANA ZILIPO

Ndugu wana habari, Tarehe 31 January, 2023 Mheshimiwa Rais alizindua Tume ya kuangalia jinsi ya kuboresha taasisi za haki ikiwemo taasisi ya Taifa inayosimamia na kuendesha mashtaka ya jinai nchini.Wakati wa uzinduzi huu Rais Samiaalinukuliwa akielezea juu ya kutoonekana kwa sehemu ya fedha zilizokusanywakutokana na makubaliano kati ya waliokuwa watuhumiwa wa makosa ya jinai na Mkurugenzi wa Mashtaka yaani “Plea Bargaining” na kuripotiwa kwa kuwepo kwa akaunti ya benki nchini China ambako baadhi ya fedha hizo ziliwekwahuko. Katikakipindi hicho Jaji Biswalo Mganga ndiye aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka.

Sambamba na uzinduzi wa Tume hiyo, Chama cha Wanaanchi-CUF tunafahamu juu ya uwepo wa uchunguzi wa fedha zaidi ya shilingi bilioni50 unaofanywa na ofisi ya  Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG. Fedha hizizilipatikana kutokana na utaifishwaji wa mali za Watanzania waliotuhumiwa kwa makosa ya jinai mbalimbali na kupelekea makubaliano na serikali kupitia ofisi ya DPP yaani “Plea Bargaining”  ambao utahusisha kuhojiwa kwa watu mbali mbali waliohusika katika jambo hilo.

Ndugu wanahabari, kama mtakumbuka “Plea bargaining” ililetwa na mabadiliko ya sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai yaliyofanyika mwaka 2019 na kuendeshwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa kuingia makubaliano na Watuhumiwa wa makosa ya jinai ambao wengi wao hawakuwa wamepewa dhamana kutokana na makosa yao kutokuwa na dhamana. Hata hivyo sheria hii ilitekelezwa na DPP hata kabla ya Mhe. Jaji Mkuu kutunga kanuni za namna bora ya kutekeleza utaratibu wa “Plea bargaining” ambao ungeainisha mambo muhimu kama akaunti ipi ambayo fedha hizi zipelekwe na kuweka wazi namna ya matumizi ya fedha hizi.Jambo la kusikitisha zaidi, sehemu ya fedha hizi zilipokelewa na DPP mwenyewe kwa njia ya fedha taslimu kinyume cha sheria za nchi na zingine kuwekwa katika akaunti nchini Chinakama alivyoeleza Mhe. Rais.

Ndugu wanahabari, Sisi CUF-Chama Cha Wananchi tunaamini kwamba, kazi ya kuchnuguzana kutazama nini kimetokea na nini kiliharibu ofisi hii ya DPP na kupelekeasehemu ya fedha hizo za umma kutojulikana zilikowekwa haitoweza kufanikiwa kutekelezwa kwa uhuru na TUME hii iliyoundwa na Mhe. Rais iwapo aliyekuwa Mkurugenzi wa Ofisi hiyo kipindi cha Plea Bargaining; Jaji Biswalo bado anashikilia nafasi ya juu katika moja ya ofisi ya utoaji haki, yaani Mahakama Kuu.

Na kama alivyosema Mheshimiwa Rais kuwa kubadilisha Mkurugenzi wa ofisi hizi peke yake  hakutotosha kumaliza mizizi inayopelekea kujitokeza kwa mapungufu haya ya kiofisi, Sisi CUF -Chama Cha Wananchi tunaamini ili kuhakikisha ofisi hizi zinabadilika kabisa na kutekeleza majukumu yake kwa Muktadha wa Misingi ya Kikatiba,  Demokrasia, Haki sawa  kwa wote na Utawala bora  kwa mujibu wa sheria, basi hata wale watumishi waliokuwa wakimsaidia Mkurugenzi wa Mashtaka kwa kipindi hicho cha “Plea Bargaining” wasimamishwe kazi ili kupisha uchunguzi huru wa TUME hiyo na uchunguzi wake utakuwa wenye tija na kufuata Utawala wa Sheria pamoja na kurejesha imani ya Watanzania katika ofisi husika.

Tume pia ichunguze na kubainisha kama kuna viongozi na taasisi nyingine zilizohusika katika sakata hili.

Pamoja na uchunguzi wa fedha zilizopokelewa taslimu na zilizowekwa kwenye akaunti za benki, pia Tume ichunguze mali zisizohamishika zilizowekwa kama dhamana kwa wale walioshindwa kulipa fedha taslimu, kama bado ziko mikononi mwa Serikali au zimerejeshwa kinyemela.

Na mwisho, wale watakaobainika wamehusika katika sakata hili ama la upotevu wa fedha au matumizi mabaya ya ofisi husika basi wachukuliwe hatua za kisheria ili kuzuia matukio kama haya kujirudia tena.

Tuna matumaini Tume itafanya kazi kwa uadilifu wa hali ya juu, bila woga wala upendeleo na tunaitakia utekelezaji mwema wa majukumu yake.

HAKI SAWA NA FURAHA KWA WOTE

Prof. Ibrahim Haruna Lipumba

Mwenyekiti CUF - Taifa


Habari kamili na Ally Thabith

AIRTEL YATOA BILIONI 1.6 KWA WATEJA WAO

 


Habari kamili na Ally Thabit

JESHI LA POLISI KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI KIMETANGAZA UKAGUZI WA MAGARI


Kamishna mkuu msaidizi kikosi cha usalama barabarani nchini Tanzania RAMADHANI NG'ANZI amesema kuanzia tarehe 6/02/2023 wameanza ukaguzi wa magari makubwa na madogo pamoja na bajaji na pikipiki.

Lengo ni kudhibiti ajali pia amesema vyombo vya moto vitakavyo kaguliwa vitabandikwa stika mbele ya kioo cha gari ambako magari makubwa yatatozwa shilingi elfu saba, magari madogo Tsh 5000/= Bajaji na Pikipiki watatonzwa Ths 2000/= ametoa wito wakuwa vikosi vya usalama barabarani kutenga maeneo kwaajili ya ukaguzi wa vyombo hivi vya moto pia amewataka wenye vyombo vya moto kupeleka vyombo vyao vikaguliwe kwani ifikapo tarehe 11/03/2023 ndio mwisho wa ukaguzi hivyo sheria ya kukamata itatumika.







Habari picha na Ally Thabit

Saturday 4 February 2023

PJM TANZANIA YAJA NA KIPODOZI KABAMBE

 Mkurugenzi wa Kampuni ya PJM TANZANIA amesema kutokana na tatizo la Chunusi na matatizo ya ngozi wameamuwa kuja bidhaa kabambe yenye ubora na raisi kupatikana Kwa beinafuu bidhaa hii inaitwa BLUE VALLEY .

Mkurugenzi Piusi Morris amewataka watu wote kuchangamkia bidhaa yao BLUE VALLEY ili ngozi zao ziwe nyororo.

Nae Kwa upande wake Zai wa Kijiwe Nongwa ambae ni barozi wa bidhaa ya BLUE VALLEY amewataka watu watumie bidhaa hii kwani ngozi zao zitanawia.

Habari picha na Ally Thabiti

WAZIRI MCHENGERWA KUKUZA SEKTA YA SANAA


 Waziri wa Sanaa, Michezo na Utamaduni amewaakikishia watanzania kuwa sekta ya Sanaa Michezo na Utamaduni zitakuwa Kwa kiwango kikubwa kwani Wizara Yake inatekeleza maagizo na maelekezo ya Ràis Samia suluhu Hassan ambako Kwa sasas wizara imetoa mikopo ya Fedha isiyo na riba kwenye sekta mbalimbali za Sanaa.

Pia Wizara inakuja na vazi la taifa na mdundo wa taifa ,Waziri Mchengerwa ametoa Rai Kwa jamii kutowaficha na kuwafungia ndani watu wenye maitaji maalum wakiwemo wenye ulemavu  wa Aina zote kwani wanauwezo makubwa na Wizara inawaunga mkono.

Mfano Wizara ya Sanaa Michezo na Utamaduni kupitia serikali ya Tanzania imempamkopo usio na riba msanii mwenye ulemavu CHIBAKISMATI milioni 10 Fedha ya kitanzania.

Habari picha na Ally Thabiti

MENEJA WA CHIBAKISMATI AJIVUNIA


 Jilbert Rema ni Meneja wa CHIBAKISMATI amesema yangu aanze kumsimamia msanii wake wameweza kupata mafanikio makubwa.

Mfano kufanya Miradi mbalimbali kwenda kuimba kwenye matamasha makubwa na ameweza kujitangaza kitaifa na kimataifa mpaka kupelekea Wizara ya Sanaa, Michezo na Utamaduni Chini ya Waziri mchengerwa kumpa mkopo ambao auna riba msanii CHIBAKISMATI.

Habari picha na Ally Thabiti 

MSANII ALI KIBA AKIPONGEZA WIZARA YA SANAA ,MICHEZO NA UTAMADUNI


 Ali Kiba amesema Wizara ya Sanaa, Michezo na Utamaduni imefanya Jambo zuri na Jena Kwa kuwapa mikopo isiyo na riba wasabi kwani itasaidia Kwa kiasi kikubwa kufanya kazi zao Kwa ufanisi na ajira zitaongezeka nchini Tanzania.

Ali Kiba amesema kupitia taasisi Yake wataendelea kuwasaidia watu wenye maitaji maalum kiuchumi na kisanaa.

Habari picha na Ally Thabiti

NMB BANK YAJIDHATITI KUWAKWAMUWA WAENDESHA BODABODA NA WAMACHINGA


 Kiongozi wa NMB BANK amesema Lengo la kuwapeleka nchini Rwanda Wamachinga,waendesha Bodaboda na Bajaji ili waweze kuongeza wigo wa masomo nje ya nchi kama anavyoonekana Pichani akiwa na tiketi ya ndege .

Uku akiambatana na Mkuu wa mkoa wa DSM Amosi Makala ameahidi kuwa NMB bank itaendelea kuwatafutia fursa ya masomo Wamachinga, waendesha Bodaboda na Bajaji ndani ya nchi na nje ya nchi.

Habari picha na Ally Thabiti

PICHANI MWENYEKITI WA MACHINGA AKIAGANA NA UONGOZI WA MKOA WA DSM NA VIONGOZI WA NMB

Kanma inavyoonekana Pichani Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa DSM Namoto Yusufu Namoto akiwa na tiketi Yake taayali Kwa Safari ya nchini Rwanda Kwa mafunzo ya siku4.

Habari na Ally Thabiti
 

MKUU WA MKOA AWAPA BARAKA VIONGOZI WA MACHINGA NA BODABODA ZIARA YA RWANDA

 

Mkuu wa Mkoa wa DSM Amosi Makala amewataka viongozi wa Bodaboda ,Bajaji na Wamachinga wayatumie vizuri mafunzo wanayoenda kuyapata nchini Rwanda. 

Pia wachangamkie fursa za kibiashara ili wapanue Wigo mpana kwenye Biashara zao ambako itasaidia Kwa kiasi kikubwa kukuwa uchumi wa Tanzania na mtu mmojammoja.

Ameipongeza bank ya NMB Kwa kufadhili mafunzo haya kama wanavyoonekana kwenye picha ya pamoja .

Habari picha na Ally Thabiti

WAMACHINGA WAIPONGEZA NMB BANK


 Mwenyekiti wa Machinga Mikoa wa DSM Namoto Yusufu Namoto ameipongeza na kuishikuru bank ya NMB Kwa kuwapeleka nchini Rwanda kwaajili ya mafunzo hivyo elimu watakayoipata watakuja kuwafundisha wengine.

Pia ametoa ofu Mkuu wa mkoa wa DSM Amosi Makala kuwa Wamachinga awatamuangusha  na watachangamkia fursa nchini Rwanda.

Habari picha na Ally Thabiti

JUKWAA LA WAARIRI LAIPONGEZA UNITED NATIONS TANZANIA

Mwenyekiti wa Jukwaa la Waariri nchinitanzania ndugu Barile ameipongeza na kuishikuru United Nations Tanzania Kwa kuwawapa elimu ya utendaji kazi Kwa Waariri wa vyombo vya habari Tanzania.  na kupewa fursa ya ushirikiano kwenye nguzo4 za maendeleo ya dunia .

Ndugu Barile ameumba umoja wa mataifa kutoa elimu Kwa Waariri na Wanahabari katika kuelekea uchaguzi wa wenyeviti wa serikali za mtaa mwaka 2024 na uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 .

Lengo wanahabari wakitanzania waandike habari sahihi za uchaguzi .

Habari picha na Ally Thabiti


 

U.N. YATETA NA WAARIRI WA VYOMBO VYA HABARI

 

Muwakilishi Mkaazi wa United Nations Tanzania amekutana wa waariri wa vyombo vya habari pamoja na wanahabari Lengo ni kuwaeleza nguzo 4 za Mipango ya U.N.kwani amesema nguzo. hizi za maendeleo ili zikamilike zinaitaji ushirikiano wa vyombo vya habari nchinitanzania.

Ametoa wito Kwa wanahabari na waariri wafanye kazi Kwa bidii na kushirikiana .

Habari picha na Ally Thabiti 

Thursday 2 February 2023

WAZIRI ASHATU KIJAJI AWATAKA WATU WENYE ULEMAVU KUSHIRI KWENYE BIASHARA


Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Dkt Ashatu Kijaji anawataka watu wenye maitaji maalum watumie mikopo ya 2% inayotolewa kwenyehalmashauri ili wazitumie kufanya Biashara,

Wizara Yake inahudumia makundi tote 

Habari picha na Ally Thabiti



DR GODWILL G WANGA EXECUTIVE SECRETARY WAFANYABIASHARA WACHANGAMKIE FURSA


 Prime Minister's Office Dr Godwill G Wanga Executive Secretary amesema wafanyabiashara, wawekezaji na wenyeviwanda wachangamkie fursa za kiuchumi ilikukuza patio la Tanzania, amewataka ofu washiriki wa mkutano kuwa changamoto walizowasilisha watafanyia kazi.

Habari picha na Ally Thabiti 

WAZIRI ANJERA KAIRUKI ALEJESHA TUMAINI KWA WALIMU

 

Waziri wa Tamisemi Anjera  Kairuki amewaakikishia Walimu kelo na changamoto zao zote ikiwemo kupandishwa madaraja na makazi zitatatuliwa na pia Kwa Walimu wenye maitaji maalum changamoto zao zitapatiwa ufumbuzi.

Habari 

GODWIN GONDWE AIMIZA UADILIFU NA UAJIBIKAJI


 Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni amewataka watumishi na watendaji Wilaya ya Kinondoni wawe waadilifu na wawajibikaji pia washirikiane kwenye utendaji kazi.

Habari picha na Victoria stanslaus

MENEJA TARURA KINONDONI AELEZA MIKAKATI


 Meneja Tarura Kinondoni amesema Tarura Wilaya ya Kinondoni inatatuwa kelo za barabara kwa Rami na changarawe, pia tarura wanashirikiana na Tra  na Idara zingine kwenye ujenzi wa barabara.

Habari picha na Ally Thabiti

TAASISI YA JAKAYA KIKWETE YA MOYO YAFANYA KAMBI YA SIKU MBILI


 Kaimu Mkurugenzi waTaasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete amesema kupitia madaktali wa India wameweza kutibu watu Moyo bila kufanya upasuaji wa kifua Kwa watanzania 12 ambako madaktali wa kitanzania wameweza kupata ujuzi ambako itasaidia kuokoa  pesa Kwa kiasi kikubwa.

Habari picha na Ally Thabiti

WAZIRI WA VIWANDA ,BIASHARA NA UWEKEZAJI AKUTANA NA WADAU IN

 Waziri Dr Ashatu Kijaji amesema Lengo la wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kukutana na Wadau wake kuweza kujadili changamoto walizonazo wafanya Biashara, wawekezaji,wenye kampuni na viwanda. Pia kufanya mabolesho ya Sera,Sheria na kanuni ili vipato vyawafanyabiashara na wananchi vikuwe.

Habari na Ally Thabiti


PICHANI WANAFUNZI WA JANGWANI WAKIWA KWENYESIKU YA SELI MUNDU


 Habari picha na Ally Thabiti 

MSTAIKI MEA WA JIJI LA DSM APONGEZA UZINDUZI WA DUKA LA VIATU


 Omary Kumbiramoto Mstaiki Mea wa Jiji la Dsm amepongeza uzinduzi wa Duka la Viatu liitwalo SPARX lililopo kata ya mchafukoge kwani Duka ililitasaidia watukupata ajira na Biashara zao  zinauzwa Kwa bei nafuu.

Habari picha na Ally Thabiti 

HAMAD MUSA SALUM AVUTIA WATU KUNUNUA BIDHAA ZAO


 Mkurugenzi wa Kampuni ya Sparx Hamad Musa Salum amesema watu wajitokeze kununua viatu vya Aina mbalimbali kwani nibei nafuu na imara.
 
Pia amesema wanampango WA kufungua maduka 20 DSM na mikoani .

Habari picha na Ally Thabiti

DOKTA AIMIZA JAMII KUPIM SELIMUNDU


 Dkt anaeusika na Maswala ya Selimundu amekitaka jamii kupima jenetiki zao ili kugunduwa selimundu.

Habari na Ally Thabiti

MSANII CHIBA KISMATI ATOA NENO KUUSU SELIMUNDU


Martini (Chiba Kismati)  amesema Jamii iwapeleke shule watoto wenye selimundu kwani wanauwezo mkubwa mfano yeye ni msanii na mkurugenzi wa wenye taasisi Yake.

Habari na Ally Thabiti