Tuesday 23 May 2023

BAJETI YA TRIL. 3.554 KUBORESHA MIUNDOMBINU NCHINI



Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imeliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuidhinisha zaidi ya shilingi Trilioni 3.5 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara, madaraja, viwanja vya ndege, reli, meli, vivuko, majengo ya Serikali na ununuzi wa ndege.

Fedha hizo zimeombwa ili kuimarisha huduma za usafiri na usafirishaji kote nchini na hivyo kuimarisha ukuaji wa uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Akiwasilisha mpango na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema pamoja na mambo mengine fedha hizo zinatarajiwa kujenga miradi ya kihistoria yenye urefu wa kilometa 2,035 nchini ikiwemo barabara za Kidatu - Ifakara - Lupilo - Malinyi - Kilosa kwa Mpepo - Londo - Lumecha hadi Songea KM 435.

Miradi mingine ni barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago - Maswa hadi simiyu KM 339 na barabara ya Handeni – Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboroti – Mrijochini – Dalai – Chambalo – Chemba – Kwa mtoro hadi Singida KM 460.

Aidha, Prof. Mbarawa amefafanua kuwa Serikali itaendeleza ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam – Mwanza KM 1,219 katika vipande vitano vya awamu ya kwanza ya ujenzi ili kuhakikisha vinakamilika kwa wakati na kwa thamani halisi ya fedha.

“Mheshimiwa Spika vipande hivyo ni Dar es Salaam – Morogoro KM 300, Morogoro – Makutupora KM 422, Mwanza – Isaka KM 341,  Makutupora – Tabora KM 368 na Tabora – Isaka KM 165 ambavyo ujenzi wake uko katika hatua mbalimbali za utekelezaji”, amesema Prof. Mbarawa.

Aidha, Serikali itaendelea na awamu ya pili ya ujenzi wa SGR sehemu ya Tabora – Kigoma KM 506 ambapo mkataba wake umesainiwa na kwa sasa mkandarasi anakamilisha maandalizi ya ujenzi.

Awali akitaja vipaumbele vya Sekta ya Ujenzi Prof. Mbarawa amesema ni pamoja na kuanza ujenzi wa barabara ya Express way kutoka Kibaha-Chalinze-Morogoro yenye urefu wa KM 205 kwa mfumo wa PPP na  kuendeleza  ujenzi wa barabara kuu zenye urefu wa KM 350 ambapo kilometa 282 zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na kilometa 68 ni miradi mipya.

“Wizara imepanga kufanya matengenezo ya kilometa 38,384.90 za barabara kuu na barabara za mikoa pamoja na matengenezo ya madaraja 3,129”, amesisitiza Prof. Mbarawa.  

Kuhusu vipaumbele vya Sekta ya Uchukuzi, Prof. Mbarawa ameeleza kuwa Serikali inakusudia kutekeleza miradi ya miundombinu ya reli ambapo ujenzi wa reli mpya ya SGR na ukarabati wa reli ya zamani ya MGR na TAZARA.

Waziri Mbarawa amesema katika kuimarisha bandari nchini Serikali imepanga kuboresha bandari zilizomo katika maziwa makuu ikiwemo bandari ya Bukoba, Kemondo bay, Mwanza South, Mwanza North, Kibirizi na Ujiji.

Serikali itaendelea na ununuzi wa mitambo ya kuongozea ndege na uendelezaji wa Chuo cha mafunzo ya usafiri wa anga ikiwa ni pamoja na mradi wa ununuzi wa rada mpya, na vifaa vya ujenzi wa miundombinu ya hali ya hewa.

Kati ya zaidi ya shilingi Trilioni 3.5 zinazoombwa katika bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu takriban shilingi Trilioni 1.5 ni kwa ajili ya Sekta ya Ujenzi na shilingi Trilioni 2.086 kwa ajili ya Sekta ya Uchukuzi.

Habari picha na Ally Thabiti

HANDRY SAMKY AIPONGEZA BANK YA NBC

Maneja program wa taasisi ya Mkapa Foundation aipongeza bank ya NBC kwa kuja na NBC Marathoni ambapo mbio hizi zitafanyika tarehe 23/07/2023 jijini  Dodoma ambako kiasi cha fedha kinachotarajiwa kukusanywa ni Millioni mia Tatu lengo kuweza kusaidi Hospitali ya Ocea Road kwa ajili ya wagonjwa wanaoumwa salatani ya shingo ya kizazi na fedha zingine itapewa taasisi ya Mkapa Foundation kwa ajili ya kuweza kuwafadhili kimasomo wakunga.

Hendry Samky amesema fedha hizi zitasaidia kwa kiasi kikubwa kunusuru vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua na wakunga watakuwa na taaluma pamoja na weredi kwenye kazi zao, kwani idadi ya akina mama kwenda kujifungua hospitali itaongezeka ambako mwaka 2016, 63% ya wanawake walikuwa wanajifungulia vituo vya afya na 85% wanajifungulia vituo vya afya na Hospitalini huku kukiwepo na huaba wa watumishi kwenye sekta ya afya kwa  52%  pia Hendry Samky amesema nivyema serikali kwa sasa kuweka wataaramu wa lugha za arama kwenye sekta ya afya pamoja na vyuoni. 

Kwa upande wake mkurugenzi wa benki ya NBC amesema taasisi ya Mkapa Foundation itapewa fedha itakayokusanywa na benki yao kwenye marathoni kwa ajili ya wakunga hapa nchini.

Habari picha na Ally Thabiti





Monday 22 May 2023

Wadau walioalikwa katika uzinduzi wa Ikulu mpya ya Chamwino Dodoma

 





RASI DKT. SAMIA ATEUA VIONGOZI NANE WAKIWEMO MABALOZI

 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Mabalozi kama ifuatavyo:


  1. Amemteua Meja Jenerali Ramson Godwin Mwaisaka kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo, Meja Jenerali Mwaisaka alikuwa Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Wanamaji (JWTZ).


  1. Amemteua Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Simuli alikuwa Mkuu wa Utumishi Jeshini (JWTZ).


  1. Amemteua Bw. Mohamed Awesu kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo Bw. Awesu alikuwa Konseli Mkuu, Konseli ya Tanzania, Jeddah Saudia Arabia.


  1. Amemteua Bw. Gelasius Byakanwa kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo Bw. Byakanwa alikuwa Afisa Mkuu Ubalozi wa Tanzania, Korea ya Kusini.


  1. Amemteua Dkt. Mohamed Juma Abdallah kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo Dkt. Abdallah alikuwa Katibu Tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja. 


  1. Amemteua Bw. Hassan Mwamweta kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo Bw. Mwamweta alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi na Mkuu wa Utawala, Ubalozi wa Tanzania, Uturuki.


  1. Amemteua Bw. Imani Salum Njalikai kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo Bw. Njalikai alikuwa Afisa wa Mambo ya Nje Mkuu na Msaidizi wa Waziri Mkuu – Hotuba


  1. Amemteua Bw. Khamis Mussa Omar kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi huo Bw. Mussa alikuwa Kaimu Mwakilishi wa Kudumu, Ubalozi wa Tanzania Ufaransa.


Uteuzi huu wa Mabalozi umeanza tarehe 10 Mei, 2023 na wataapishwa kwa tarehe        itakayopangwa baadae. 


Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

SILENT OCEAN WAFUNGUA OFISI INDIA KIBABE


Mohamed Kamilagwa Meneja Masoko wa Silent Ocean amesema wameamua kufungua Ofisi yao nchini India eneo la Mumbai lengo kuweza kuwasafirishia bidhaa zao wafanya biashara.

Mohamed Kamilagwa amewatoa hofu na Mashaka wafanyabiashara wote kuwa mizigo yao itasafirishwa kwa gharama nafuu na usalama wakutosha kwani kilio cha wafanyabiashara kilikuwa cha muda mrefu kwani walikuwa wanasafirisha mizigo yao miezi mitatu hadi sita. Hivyo Silent Ocean wameamua kufungua Ofisi India ambako Silent Ocean watasafrisha mizigo kuanzia siku 17 hadi 25.


Habari Kamili na Ally Thabiti

WHO KUWATHAMINI WAKUNGA

Meneja wa masuala ya MATENITE bwana Emmanuel amesema WHO inatahamini na kuwajali wakunga nchini Tanzania.

Habari kamili na Ally Thabith

TMDA KANDA YA ZIWA YAKAMATA VIFAA TIBA NA DAWA BANDIA

 Meneja wa kanda ya ziwa wa TMDA Sophia Mzilai amekamata madawa na vifaa tiba vilivyoingizwa kanda ya ziwa bila kufuata utaratibu na walivyovikamata wadai ni feki na badala yake wameviteteketeza na wahusika kupelekwa mahakaamani ambavyo vifaa tiba na hizo dawa thamani yake milioni therathini.

Habari kamili na Ally Thabiti

MSTAHIKI MEA WA KINONDONI AMPONGEZA RAISI SAMIA SULUHU HASSANI

 Songoro Mnyonge Mstahiki Mea wa Manispaa ya kinondoni kupitia baraza la madiwani lililokaa, wamempongeza na kumshukuru Rais Dr. Samia Suluhu Hassani kwa kuweza kutoa fedha za boost kiasi cha bilioni 1.5 kwaajili ya vyoo na madarasa kwenye shule za msingi za kinondoni pia kwa kuwapandisha vyeo na mishahara watumishi wa kinondoni.

Habari kamili na Ally Thabiti

TMDA WAKUTANA NA WASAMBAZAJI WA VIFAA TIBA NA MADAWA

 Emmanuel Alphonce meneja mkaguzi wa dawa TMDA amesema lengo lakukutana na wasambazaji wa dawa na vifaa tiba huweza kuwakumbusha sheria, kanuni na taratibu wa uingizaji wa vifaa tiba nchini Tanzania.


Habari kamili na Ally Thabith

DIWANI BUSORO PAZI ANDAA MASHINDANO YA QUR AN

 Busoro Pazi diwani wa kata ya buguruni amesema lengo la kuandaa mashindano ya Qur An watu wamjue Mwenyezi Mungu.

Habari kamili na Ally Thabith

Tuesday 9 May 2023

Kiongozi wa zamani wa Pakistan Imran Khan akamatwa

 

Maafisa wa usalama wa Pakistani walimkamata Waziri Mkuu wa zamani Imran Khan siku ya Jumanne alipokuwa akifikishwa mahakamani katika mji mkuu, Islamabad, kujibu mashtaka ya kesi nyingi za ufisadi, maafisa wa chama chake walisema.

Khan alitolewa nje na kuwekwa ndani ya gari la polisi na maajenti kutoka taasisi ya kupambana na rushwa nchini humo, Ofisi ya Kitaifa ya Uwajibikaji, kulingana na Fawad Chaudhry, afisa mkuu wa chama cha Pakistan Tehreek-e-Insaf.

Televisheni huru ya GEO ya Pakistan ilitangaza picha za Khan mwenye umri wa miaka 72 akivutwa na vikosi vya usalama kuelekea kwenye gari la kivita, ambalo lilimchukua.

Khan aliangushwa kwa kura ya kutokuwa na imani naye Aprili 2022. Amedai kuondolewa kwake kulikuwa kinyume cha sheria na njama ya Magharibi na amefanya kampeni dhidi ya serikali ya mrithi wake, Waziri Mkuu Shahbaz Sharif, akitaka uchaguzi wa mapema.


Chama cha Khan kililalamika mara moja kwa Mahakama Kuu ya Islamabad, ambayo iliomba ripoti ya polisi kuelezea mashtaka ya kukamatwa kwa Khan.

Maafisa wa shirika la kupambana na ufisadi walisema kuwa Ofisi ya Kitaifa ya Uwajibikaji ya Pakistan ilitoa hati za kukamatwa kwa Khan wiki iliyopita katika kesi tofauti ya ufisadi, ambayo hakupata dhamana  jambo ambalo litamlinda dhidi ya kukamatwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Maafisa hao, ambao walizungumza kwa sharti la kutotajwa majina, walisema Khan atafikishwa mbele ya mahakama ya kupinga ufisadi baadaye Jumanne.

Hakukuwa na taarifa nyingine rasmi kutoka kwa serikali kuhusu kukamatwa kwa Khan.


Habari Picha na Ally Thabiti

Expedia Group Kushirikiana Na Tanzania Kutangaza Utalii


 

Seattle, Marekani

Kampuni kubwa ya biashara ya utalii duniani kupitia mtandao, Expedia Group, imeahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Bodi ya Utalii (TTB), kutangaza na kuleta watalii wengi zaidi nchini Tanzania.

Kauli hiyo inayounga mkono pia juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuitangaza Tanzania kimataifa, imetolewa jana Mei 8, 2023, na Mkurugenzi Mwandamizi wa Masoko ya Kimataifa wa kampuni hiyo, Bw. Andrew Van Der Feltz, alipokutana na kufanya mazungumzo kwenye makao makuu yao mjini Seattle na ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi.

Expedia ni kampuni inayotumia teknolojia za kisasa kutangaza na kuhudumia watu zaidi ya milioni 400 kwa mwezi duniani na ikiwa inatumia muunganiko wa zaidi ya tovuti 200 na ikifanya kazi na mashirika ya ndege na wabia wengine zaidi ya 509 ikishika nafasi ya pili duniani na wakati fulani namba moja Marekani kwa kuaminiwa na watalii katika sekta ya usafiri na utalii.

Awali, ujumbe wa Tanzania pia ulipata wasaa wa kusalimiana na Rais wa Expedia Group anayeshughulikia Biashara ya Kimataifa, Bi. Ariane Gorin, ambaye aliueleza ujumbe huo kuwa Tanzania ambako alipata kutembelea mwaka 2016 Tarangire, Serengeti na Ngorongoro Kreta kuwa ni nchi yenye vivutio vya kipekee na anatarajia kuitembelea tena.

Kwa upande wake Dkt. Abbasi aliyeambatana na Mtendaji Mkuu wa TTB, Damasi Mfugale, aliwahakikishia watendaji hao wa Expedia kuwa Tanzania kwa sasa imeamua kuja na mtazamo mpya katika kutangaza utalii.

“Tunaamini utaalamu wenu na uzoefu wenu katika masoko na biashara ya utalii kimtandao utasaidia kuongezea juhudi za Rais wetu wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amefanya juhudi kubwa kupitia filamu ya “Tanzania; The Royal Tour” kuiweka Tanzania katikataswira pana zaidi kimataifa katika utalii na uwekezaji,” alisema Dkt. Abbasi. 

UPIMAJI NA MATIBABU YA MAGONJWA YA MOYO MKOANI MANYARA


 Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Manyara  watafanya upimaji na matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa wa Manyara. Upimaji huo utaenda sambamba na maadhimisho ya Siku ya Shinikizo la Juu la Damu Duniani yatakayofanyika  tarehe 17/05/2023.

Upimaji huo utafanyika kwa watoto na watu wazima kuanzia tarehe 15/05/2023  hadi tarehe 19/05/2023  saa mbili kamili asubuhi mpaka saa 10 kamili jioni katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Manyara.

 

Kutakuwa na wataalamu wa lishe ambao watatoa elimu ya lishe bora ambayo itawapa wananchi uelewa na  kufuata mtindo bora wa maisha ambao utawasaidia kuepukana na magonjwa ya moyo ambayo ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza na yanaweza kuepukika kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.

 

Watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu hapohapo au kupewa rufaa ya kuja kutibiwa katika Taasisi yetu.


Tunawaomba wananchi mjitokeze kwa wingi kupima afya zenu kujua kama mna matatizo ya moyo ili kuanza matibabu mapema kwa atakayebainika kuwa mgonjwa.

Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa namba 0768408984 Vailine Osward na 0714956529 Abubakar Mjaka.


        • “Afya ya Moyo Wako ni Jukumu Letu”.


Habari Picha na Ally Thabiti

 


WADAU WAKUTANA NA KUWEKA MIKAKATI YA KUENDELEZA KILIMO BIASHARA

 


SEKTA ya kilimo bado inazo fursa mbalimbali ambazo zikitumika ipasavyo zitawezesha uchumi wa nchi kukua sambamba na kuzalisha ajira nyingi kwa watanzania.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, wakati akifungua kongamano kuwajengea uwezo wakulima kuhusu kilimo biashara lililoandaliwa na ubalozi wa Uholanzi nchini na kufanyika mjini Dodoma, likiwa linawashirikisha wakulima na wadau mbalimbali katika sekta hiyo.

Kwa upande wake,Balozi wa Uholanzi nchini,Mh. Wiebe De Boer, alisema Serikali ya nchi hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania hasa katika sekta hiyo ili izidi kukua na kuongeza uchumi.


Balozi wa Uholanzi nchini, Mh.Wiebe De Boer, akibadilishana mawazo na Waziri wa Kilimo Mh.Hussein Bashe ,muda mfupi kabla ya kuanza kwa kongamano hilo.

Waziri wa Kilimo Mh.Hussein Bashe. akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa wa Uholanzi nchini,Mh.Wiebe De Boer baada ya kufungua kongamano la kuendeleza kilimo biashara nchini.

Habari Picha na Ally Thabiti

Kanisa Lahukumiwa Kulipa Milioni 70 Kwa Kosa La Gari Kugonga Na Kusababisha Kifo

 


Njombe

MAHAKAMA ya hakimu Mkazi Njombe imelihukumu Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya kusini kulipa fidia ya shilingi Milioni 70 baada ya gari mali ya kanisa hilo kugonga na kusababisha kifo cha marehemu Kaselida Mlowe wa mjini Njombe.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu wa Mahakama ya Hakimu mkazi Njombe Lihad Chamshama amesema mdaiwa namba mbili ambaye ni kanisa anahukumumiwa kulipa fidia ya milioni 70 kutokana na uzembe uliofanywa na mdaiwa namba moja bwana Rajab Kitwana ambaye alikuwa dereva wa gari hiyo wakati ikitoka mjini Makambako kwenye matengenezo na kusababisha kifo cha Marehemu Kaselida.

Aidha Mahakama hiyo imetoa jukumu kwa kanisa kulipa ghalama zote za uendeshaji wa kesi iliyoendeshwa kwa zaidi ya miaka miwili mpaka sasa huku ikitoa haki ya kukata rufaa kwa kanisa dhidi ya hukumu hiyo.

Hukumu hiyo imetolewa na Mahakama kutokana na kesi No 2 ya mwaka 2022 ya madai ya fidia ya Milioni 100 dhidi ya kanisa la KKKT iliyofunguliwa na Siglada Mligo msimamizi ambaye ni msimamizi wa mirathi wa marehemu Kaselida Mlowe baada ya kifo kilichotokana na ajali ambapo marehemu aliacha wategemezi wakiwemo watoto wake watatu.

Kesi ilifunguliwa baada ya msimamizi wa mirathi kushinda kesi No 6,2021 ya makosa ya usalama barabarani kutokana na ajali iliyotokea eneo la Kibena Mlima wa Ichunilo mjini Njombe hapo September 25,2020 baina ya Hiace Namba T 298 DNE na gari NO T 210 - AHU Mercedes Benz Track mali ya kanisa na kupelekea kifo cha Kaseleida Mlowe.

Kesi hiyo imeendeshwa na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe Lihad Chamshama huku upande wa madai ukiwakilishwa na mawakili watatu akiwemo Emmanuel Chengula,Frank Ngafumika na Gervas Semgabo huku upande wa utetezi ukiwakilishwa na wakili Marco Kisakali.

Habari na Ally Thabiti

DAWASA AWATAKA WATEJA WAAO KULIPA BILLS

 Mkurugenzi Mkuu mtendaji wa Dawasa Kiula Kingu amewataka wateja wa Dawasa kulipa bills kwa wakati na kulinda miundo mbinu ya maji.

Habari na Ally Thabiti

OCEAN ROAD KUNUSULU VIFO VYA WAGONJWA WA SALATANI

Mkurugenzi mkuu mtendaji wa Hospitali ya Ocean Road Dr. Julius Mwaiselage amesema kwa kushirikiana na wabunge na umoja wa cheif Tanzania watacheza mchezo wa mpira wa miguu mjini Dodoma kwenye uwanja wa jamuhiri tarehe 27/05/2023 kati ya wabunge na machief lengo kukusanya kiasi cha shilingi milion mia tatu (Tsh. 300,000,000/=) kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa salatanu hospitali ya Ocean Road. Dr. Julius Mwaiselage ametoa wito kwa Taasisi,makampuni na mashirika na watu binafsi kujitokeza kwa wingi katika kuchangia kiasi cha milioni mitaatu, kwani kitaenda kuokoa wangonjwa wa salatani wapatao mia moja. 

Pia kuanzia tarehe 25/05/2023 mpaka tarehe 28/05./2023 kutatolewa chanjo na elimu ya lishe ambapo Hospitali ya Ocean Road itawafikia watu wenye ulemavu wa aina yote kama wanavyofanya siku zote.


Habari na Ally Thabiti

RAIS SAMIA AWAFUTA CHOZI WAKAZI WA MAGOMENI KOTA

 Mkurugenzi mkuu mtendaji wa wakala wa majengo Tanzania (TDA) DAUDI KANDOLO amesema Rais wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassani ametoa maelekezo kwa watu wanaoishi kwenye nyumba za magomeni kota wakae miaka thelasini ambako miaka mitano watakaa bule na miaka Ishirni na Tano kwa mtu mwenye chumba kimoja atanunua kwa shilingi milioni arobaini na nani nukta tano na kwa mtu anaishi kwenye vyumba viwili atalipa kiasi cha milioni Amthini na sita nukta nane. Daudi Kandolo amesema kwa wasioweza kulipa watoe taarifa lakini watakaa bure kwa miaka mitano.

Habari  na Ally Thabiti

Tuesday 2 May 2023

WIZARA YA FEDHA YAKUTANA NA IFC

 1. Wageni waalikwa , Mabibi na Mabwana;

2. Ni heshima kubwa kuwepo hapa leo kuongoza warsha hii muhimu inayohusisha miradi

inayotarajiwa kutekelezwa kwa utaratibu wa PPP, ambayo inalenga sekta za Nishati pamoja na

Uchukuzi. Sekta ya Nishati na Uchukuzi ni muhimu kwenye ukuaji wa uchumi na maendeleo

katika nchi zinazoibukia kiuchumi kama Tanzania. Kuwekeza katika sekta hizi kupitia Ubia kati

ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi kunaweza kuweka mazingira mazuri ya ukuaji wa kiuchumi

na maendeleo.

3. Mabibi na Mabwana, tunaweza kuendeleza na kuboresha miundombinu ya usafirishaji

kupitia- utaratibu wa PPP, kutoa fursa za ajira pamoja na masoko ya kibiashara . Hii, kwa

upande wake, itasaidia kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na huduma, pamoja na kuchochea

shughuli za kiuchumi. Zaidi ya hayo, tunaweza kutoa nishati ya kuaminika na ya bei nafuu

kwenye maeneo ya majumbani, biashara, na viwanda.

4. Kwa pamoja, tunaweza kutumia utaalamu na rasilimali za sekta ya Umma na sekta

Binafsi ili kuongeza ufanisi. Warsha hii inaashiria hatua kubwa katika kutambua na kuendeleza

miradi ya PPP ambayo italeta manufaa ya kudumu kwa wananchi wa Tanzania.

Kuendeleza miundombinu kunahitaji uwekezaji mkubwa ambao unaweza kuwa mzigo mkubwa

kwa serikali, haswa wakati hazina ya nchi inapokua ndogo, na kiwango cha deni la taifa likizidi

kuongezeka . Kwa kuzingatia changamoto hizi, ushirikishwaji wa sekta binafsi umezidi kuwa

muhimu ili kuisaidia serikali kwa kuwekeza kwenye miundombinu.

5. Zaidi ya hayo, kutokana na kukua na kubadilika kwa uchumi wa dunia,utaalam na

teknolojia unahitajika ili kuchochea maendeleo ya miundombinu. Ubia kati ya Sekta ya Umma

na Binafsi (PPPs) hutoa fursa nzuri ya kutumia rasilimali na utaalamu wa sekta binafsi. Kwa

kushirikiana na Sekta Binafsi, tunaweza kutumia mitaji yao, teknolojia na maarifa itakayosaidia

ukuaji wa miundombinu muhimu na huduma zinazohitajika nchini kwetu. PPPs zinaweza

kufungua fursa mpya za ukuaji wa uchumi na maendeleo kiujumla.

6. Naipongeza Idara ya PPP iliyo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuandaa warsha

hii ya kimkakati kwa ajili utekelezaji wa miradi ya PPP,vileile Nimeridhishwa na maandalizi

yaliyofanyika kwenye warsha hii. kama Katibu Mkuu wa Wizara, naahidi kuiunga mkono idara

na kuiwezesha kila itakapo hitajika ili kuhakikisha mipango yake inafanikiwa.

Hata hivyo, ni muhimu kutambua kwamba wakati Kituo cha PPP kinatumika kama mratibu,

jukumu la kuandaa miradi na kukusanya rasilimali liko chini ya Mamlaka za usimamizi, kwa

msaada wa serikali chini ya Wizara ya Fedha.


7. Vile vile, ningependa kutoa shukrani ya dhati kwa Benki ya Dunia na IFC, washirika wetu

wa muda mrefu na wawezeshaji. Ushirikiano wenu umekuwa wa thamani sana kwa maendeleo

ya PPP nchini Tanzania, kuanzia hatua za awali hadi uundaji na marekebisho ya mifumo yetu ya

PPP. Utaalam wa kiufundi, na usaidizi wa kifedha umekuwa muhimu katika kuweka msingi

thabiti wa mafanikio kwenye utelezaji wa miradi ya PPP.

8. Kwa kipindi hiki , miradi inayotarajiwa kutekelezwa kwa utaratibu wa PPP imeandaliwa,

bila kusahau msaada wa marekebisho ya Sheria ya PPP. Zaidi ya hayo, tunashukuru sana

msaada wa Benki ya Dunia kwenye mchakato wa marekebisho ya Sheria ya PPP hapa nchini.

Ninashukuru kwa msaada wa Benki ya Dunia katika uundaji wa Kituo chetu cha PPP, ikijumuisha

uanzishaji wa miongozo mbalimbali ya uendeshaji. Tunatambua juhudi na ari kubwa

inayohusika katika kazi hii.

Warsha hii itaongeza chachu ya ushirikiano mzuri kati ya Idara ya PPP na IFC. Juhudi zetu za

pamoja zimesababisha warsha hii yenye mwelekeo wa vitendo, ambayo inaashiria hatua

muhimu ya kusonga mbele katika mpango wa utekelezaji wa miradi nchini kwa utaratibu wa

PPP.

9. Wakati wa vikao hivi vya kazi, tutafaidika kutokana na uzoefu mzuri wa sekta ya Nishati

na Uchukuzi, tukitumia mafunzo tuliyojifunza, na mikakati iliyoandaliwa kutokana na miradi

yenye mafanikio. Lengo ni kubainisha hatua za kiutendaji za kufikia malengo katika FYDP III.

10. Ni matumaini yetu kwamba majadiliano katika warsha hii yatatoa mpango kazi mzuri

kwa kila kundi la washiriki, ikijumuisha Benki ya Dunia, IFC, Idara ya PPP, Wizara za Nishati na

Uchukuzi, na Mamlaka za Usimamizi . Hii ni juhudi shirikishi, na jukumu letu kama waratibu

litaendelea kuwa muhimu hadi tutakapotoa miradi ya PPP ambayo inakidhi viwango vya juu,

ambavyo tumejiwekea wenyewe chini ya FYDP III.

Utayari wao na ushiriki wao kamili katika kikao hiki bila shaka utatoa matokeo mazuri, sio tu

katika suala la matokeo ya mradi wa PPP wa kuahidi lakini pia katika kusikia uzoefu na utaalamu

kutoka kwa wataalamu wa kiufundi wa IFC kuhusu suala hilo. Kwa hiyo, nawaomba kuchukua

fursa hii kuuliza maswali yote, hasa yale ambayo yanajikita katika uundaji wa miradi ya PPP na

namna ya kugharamia miradi husika.

11. Napenda pia kuchukua fursa hii kutoa pongezi zangu kwa Mamlaka za usimamizi kwa

kuibua baadhi miradi ya PPP na Kuwa wa kwanza kuchukua hatua.

Warsha hii inazingatia sekta za usafiri na nishati, ambazo hupokea sehemu kubwa ya bajeti ya

maendeleo. Hata hivyo, tusisahau kwamba mustakabali wa nchi yetu unategemea mabadiliko

ya sekta mbalimbali na huduma za kijamii. Haja ya miundombinu thabiti ni muhimu katika

kufikia mabadiliko haya.


12. Kutokana na utimilifu wa jukumu muhimu la miundombinu thabiti katika kuleta

mabadiliko ya viwanda na huduma za jamii, Tanzania ilijiwekea malengo madhubuti ya kufadhili

Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Tatu, ambapo TZS 21.03 trilioni zitapatikana kutoka sekta

binafsi na shilingi bilioni 9 kupitia PPPs.

13. Kwa vile hiki ni kiasi kikubwa cha fedha, ni lazima tuhakikishe mbinu iliyoratibiwa ni

thabiti kwenye utekelezaji wa miradi ya PPP. Wakati Wizara ya Fedha na Idara ya PPP ina

jukumu la kutekeleza, kazi iliyopo inahitaji ushirikishwaji wa wizara za kisekta na mamlaka za

usimamizi. Warsha hii, inayolenga sekta ya Nishati na Uchukuzi, inaashiria hatua ya kwanza

katika safari hii, na warsha kama hizi zimepangwa kufanyika kwa sekta nyingine katika siku za

usoni.

14. Tunafahamu kikamilifu changamoto zilizopo katika kufanikisha mpango wetu kabambe.

Kwa hiyo, tunarekebisha mifumo yetu ya kisheria ili kuweka mazingira mazuri zaidi ya kuvutia

mtaji wa Sekta Binafsi. Hata hivyo, tunatambua pia hitaji la dharura la kuanzisha Kituo cha PPP

na dhana zake za uendeshaji, ikijumuisha Mfuko wa Uwezeshaji wa PPP pamoja na miongozo

yake. Zaidi ya hayo, ili kuhakikisha kwamba maafisa wetu wa PPP na timu za usimamizi wa

miradi wanapata ujuzi unaohitajika wa kiutaalam, tunahitaji kuweka kipaumbele katika kujenga

uwezo kuwaunga mkono kwa kuhudhuria mafunzo mbalimbali juu ya utaalam wa PPP na

kupata uthibitisho wa kitaalamu wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Kibinafsi (CP3P).

15. Pia nimechukua hatua za kuharakisha mchakato wa kuweka muundo wa PPP chini ya

kila Wizara na Mamlaka za Usimamizi. Lengo ni kufafanua kwa uwazi majukumu na wajibu wa

maafisa wa PPP katika ngazi zote. Ili kufanikisha hili, nimewasiliana na Sekretarieti ya Ajira

katika Utumishi wa Umma na kuwaomba walipe kipaumbele suala hili.

16. Warsha hii inaashiria hatua muhimu katika juhudi zetu za kuunda mpango wa PPP

ulioratibiwa na thabiti nchini Tanzania. Ni muhimu katika kufikia malengo yetu ya maendeleo ya

kitaifa, haswa katika sekta ya uchukuzi na nishati. Kupitia PPPs, tunaweza kuunda msingi wa

ukuaji endelevu na shirikishi ambao utanufaisha wananchi wote.

17. Tunalenga kuweka mazingira mazuri ambayo yanavutia uwekezaji wa sekta Binafsi na

kusaidia maendeleo ya kiuchumi. Nina imani kuwa tunaweza kufikia malengo kupitia ushirikiano

wetu na IFC na kuendeleza programu ya PPP yenye mafanikio kwa ajili ya manufaa ya Taifa.

18. Asanteni nyote kwa kuhudhuria, na ninatarajia warsha yenye tija.

Habari na Ally Thabiti