Tuesday 28 September 2021

GODFREI ABAINISHA CHANGAMOTO ZA KUPATA TAARIFA


 Godfrei amesema swala la kupata taarifa ya bajeti imekuwa tatizo ni vyema serikali itoe ushirikiano .

Habari picha na Ally Thabiti

TWAWEZA WATAKA BAJETI YA TAARIFA


 Esta ameitaka serikali kutenga fedha kwenye halmashauri ili taarifa zitolewe Kwa jamii . 

Habari picha na Ally Thabiti

WAFAMASIA KUTEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI WA AFYA


 Methiyu Maganga ni Mfamasia Kwa niaba ya wenzake wanampongeza rais  Samia Suluhu Hassan Kwa utendaji wake mzuri wa KAZI kwani wanamuunga mkono Kwa asilimia 100 wafamasia wote.

Huku wakimuaidi Waziri wa Afya,Jinsia,Wazee na Watoto kuwa watatekeleza maagizo  na maelezo ya rais Samia Suluhu Hassan,Makamu wa rais Filipu Mipango,Waziri Mkuu Majaliwa Kasim Majaliwa na Viongozi wote wa serikali na yeye mwenyewe Waziri Dorith Ngwajima.

Habari na Ally Thabiti

Monday 27 September 2021

WAZIRI WA AFYA AJA KIVINGINE


 Dorith Ngwajima Waziri wa Afya, Jinsia Watoto na Wazee  amewataka RMO kusimamia fedha zote za miradi.

 Lengo zitumike Kama inavyotakiwa ambako itasaidia Kwa kiasi kikubwa kuokoa Maisha ya watanzania kupitia Sekta ya Afya .

Habari picha na Victoria Stanslaus


JOKETI MWENGELO AMEWATAKA VIJANA KUWEKEZA KWENYE UTALII


 Mkuu wa  Wilaya ya Temeke Joketi Mwengelo amewataka vijana wa kitanzania kujitokeza Kwa wingi katika kuwekeza kwenye misitu yetu. Pia Amewapongeza na kuwashukuru TFS Kwa kuwavutia wawekezaji kwaajili ya kuwekeza kwenye misitu yetu ili Utalii wa ndani ukue Kama anavyoonekana kwenye picha ya pamoja .

Habari picha na Ally Thabiti

TFS YAPONGEZWA


 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mery Masanja  Amewapongeza TFS Kwa kutengeneza Mazingira rafiki na wezeshi Kwa Utalii wa  ndani ivyo amewataka wawekezaji kuwaona TFS kwaajili ya kuwekeza kwenye misitu yetu.

Habari picha na Ally Thabiti

SHEE WA MKOA WA KAGERA AIMIZA WATU KUCHANGIA


 Shee  Haruna Habdalla Shee wa Mkoa wa Kagera amewataka watu kujitokeza Kwa wingi kuchangia Fedha na Mali katika kuelekea siku ya Mauridi ambako kitaifa tarehe 18 na 19 mwezi wa 10 2021 mkoani Kagera ambako kiasi cha milioni Mia tatu hamsini na tano Fedha zinazoitajika kwaajili ya shuuri hii. 

Ivyo watu wachangie kupitia banki ya CRDB 015522627900 na Mawasiliano 0784644220 mwenyekiti wa kamati. 0713350110 mratibu wa kamati  .0714 270559 katibu wa kamati.

Ametoa wito kwa wamiriki wa mabasi na wafanya biashara mbalimbali wajitokeze kutoa michango Yao ambako mgeni rasimi Rai's wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Habari picha na Ally Thabiti


Thursday 23 September 2021

WADAU WA MAFUTA NA GESI WAPONGEZA SERIKALI


 Ismaili Mfanya biashara ameipongeza serikali Kwa kutoa semina kutokana na mradi wa bomba la mafuta kwani mijadara Kama hii itasaidia wazawa  kupata fursa za kujikwamuwa kiuchumi .

Ametoa wito kwa serikali wawe wanafanya makongamano na semina za namna hii mara Kwa mara .

Habari picha na Ally Thabiti

GJB GROUP OF COMPANIES


 Emmanuel Bugabu Business Development Manager amesema Kampuni Yao imejipanga katika kutoa huduma kwenye mradi wa Bomba la Mafuta linalojengwa mkoani Tanga eneo la Chongoleani mpaka nchi ya Uganda. 

Kwani wanaishukuru serikali ya Tanzania Kwa kukubali huu mradi ambako utasaidia watanzania wengi kupata pesa . Emmanuel Bugabu amewataka watanzania kuchangamkia fursa .

Kampuni Yao inaofisi dear es salaam,Mwanza ,Arusha na Zanzibar .

Habari picha na Ally Thabiti

MZEE YUSUFU ATEMA NYONGO


 Mwimbaji Mashuuri  Mzee Yusufu amewataka waimbaji  Wa taharabu  na watunzi wa taharabu kusajili tungo zào na nyimbo zao Kosota ili wapate Haki zao.

Habari picha na Ally Thabiti

RAISI WA BONGO MOVI ATOA NENO


 ELia Mjata Raisi wa Bongo Movi amewataka wasanii wenzake kujitokeza Kwa wingi kwenye mkutano wa tarehe 29 mwezi9 2021 kwenye viwanja vya makumbusho ya Taifa posta jijini Dsm.

Lengo kujadili na kupanga mikakati namna ya kujikwamuwa na wimbi la umasikini .

Habari picha na Ally Thabiti

BASATA KUWAKUTANISHA WADAU


 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Basata Mniko amesema tarehe 29 mwezi9 2021 Wasanii watakutana kwenye makumbusho ya Taifa posta jijini Dsm kwaajili ya kujadili na kutatuwa Changamoto zinazowakabili  wasanii wa Tanzania .

Ivyo amewataka wasanii wa Aina mbalimbali kujitokeza Kwa wingi.

Habari picha na Ally Thabiti

JACKREEN WOLPA APATA MAPESA


 Jacgreen Wolpa ameingia mkataba na Kampuni ya SWEET ROLAY KIDS SHINE  kwaajili ya kutanganza nguo za watoto amewataka watu kununuwa nguo za Kampuni hii kwani zina Ubora mkubwa .

Habari picha na Ally Thabiti

FATMA WA KAMPUNI YA MO AJA NA KIONJO CHA MASHABIKI WA SIMBA

Mkurugenzi wa Masoko Wa bidhaa za Mo FATMA amesema  wameamuwa kuzinduwa katuni za Mo rafiki Lengo kuwavutia mashabiki wa Simba.

Habari picha na Ally Thabiti
 

SIMBA YAWA MOTO


 Mkurugenzi Mtendaji wa Timu ya Simba Barbra Hassani Gonzales amesema mwaka huu tutafika mbali Mashindano ya Klabu bingwa Afrika  na watabeba ubingwa wa Rigi kuu soka Tanzania bara. 

Habari picha na Ally Thabiti


Tuesday 21 September 2021

JOYCE SAIDY MBUNIFU MAJENGO AIPONGENZA TAWA


 Mbunifu wa Majengo Joyce Saidy amesema anaipongeza Uongozi wa TAWA Kwa kuweza kumjengea uwezo . Pia anaishukuru Kampuni ya Tanga Ciment kwakuweza kujitoa Kwa moyo mmoja katika Mafunzo walioyapata .

Amesema Mafunzo haya na Ujuzi aliopewa atayatumia vizuri Kwa wengine . Kwaupande wake Mwenyekiti wa Bodi ya TAWA Wini Teli amesema wataendelea Kuwajenga uwezo Wanafunzi wa kike waliopo kwenye Vyuo wanaosomea maswala ya Ukandarasi ili wawe wafanisi kwenye Kazi  zao .

Nae Meneja Miradi wa Mafunzo haya Dr Vicky Malwa amesema walikuwa Wanafunzi wakike74 waliokuwawanawajengea uwezo kutokana na changamoto mbalimbali Wasichana 33 waliacha Mafunzo na hatimae 41 Wamehitimu ..

Ameahidi wataendelea na Mafunzo na kuongeza idadi ya wafunzi wasichana  uku akiwasilisha maombi ya kusaidiwa kwenye upande WA utafiti ,ushirikiano ,kupew kumbi za mikutano Kwa mgeni rasimi wa Chuo Kikuu cha Mlimani Naibu wa Chuo cha Mlimani Prof  Benadeta .

Na amewaomba Tanga Ciment waendelee kufadhili mradi huu  .huku Mwakilishi wa Tanga Ciment ameitaka jamii na wafadhili wengine wajitokeze kufadhili mradi huu. Lakini Tanga Ciment wamemtoa Ofu na mashaka Dr Vicky Malwa wataendelea kushirikiana nae .

Habari picha na Ally Thabiti

Monday 20 September 2021

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUKUTANA NA WADAU WA SIASA


 Haji Frances Mutungi Amesema wameamuwa kukutana na wadau wa VYAMA VYA SIASA pamoja na Jeshi la Polisi tarehe 30 mwezi wa 10 Lengo kuondoa sitofaam na kujenga Mazingira rafiki Kwa wanasiasa DHIDI ya Jeshi la Polisi .

Msajili wa Vyama vya Siasa amesema yeye anatekeleza kanuni ya 24 kwani wadau wa VYAMA vya siasa wakikutana na Jeshi la Polisi  wakiwemo Viongozi wa Vyama vya siasa hii itasaidia kuwepo na muafaka na maridhoano ya pamoja .

Ametoa wito kwa Wanahabari kutopotosha jamii  amesema haya jijini Dsm alipokutana na Wanahabari .

Habari na Ally Thabiti

JOWUTA YAPEWA MAAGIZO MAZITO


 Mkurugenzi wa Mafunzo Kutoka nchi ya Ghana ameitaka chombo cha JOWUTA kulinda na kusimamia mikataba ya Wanahabari wa Tanzania .

Habari picha na Ally Thabiti

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII AMUUNGA MKONO RAISI

 Merry Masanja Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii amesema katika kumuunga mkono raisi Samia Suluhu Hassan kwenye kuitangaza Utalii wa Tanzania Wizara imeweka mikakati mbalimbali ikiwemo  kuboresha Mali kale,kutunzamisitu,kuingia mikataba na wasanii kwaajili ya kuutangaza vivutio vyetu na kuandaa machapisho mbalimbali pamoja na mabango.

Pia Naibu Waziri amesema kutakuwepo na makongamano na mijadala mbalbali ya kujadili namna ya kuutangaza Utalii wetu. Amewataka Wanahabari na wasanii na wadau wengine kuunga mkono juhudi hizi.

Pia Amewapongeza TFS Kwa kulinda na kutunza misty yetu. Mfano msitu wa KAZI Mzumbwe na mingineyo.

Habari na Ally Thabiti

BIKO SKANDA WAMWAGA MAPESA


 Meneja Masoko wa Kampuni ya K4S Security Biko Skanda amesema wameamuwa kuifadhiri Timu ya Afrika Sports Kutoka mkoani Tanga mikataba WA mwaka mmoja . Pia Biko Skanda  amewataka watu kutumia Kampuni Yao katika maswala ya Ulinzi.

Habari picha na Ally Thabiti

Wednesday 15 September 2021

CLAUD GWANDU ABAINISHA MALENGO YA KUKUTANA NA WANAHABARI


 Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari wa Serikalini JOWUTA  CLAUD GWANDU amesema Lengo la kukutana na Wanahabari wa Serikalini Kuwapa Mafunzo ya namna ya kufanya Kazi zao Kwa njia ya kisasa ya kiteknolojia anaamini kuwa Mafunzo Kwa Wanahabari yataleta chachu katika kuandika na kutanza habari Kwa njia ya kisasa.

Mwenyekiti CLAUD GWANDU amewatoa Ofu watu wenye Ulemavu kuwa watawafikia kwani Chama hiki kinatekeleza Ibara ya 14 ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania  . Kuwa kila mtu ana Haji ya kupata taarifa.

Habari picha na Ally Thabiti

Saturday 11 September 2021

UONGOZI WA SOKO LA CHATEMBO WAKIKABIDHO CHANGAMOTO KWA MAANDISHI


 Kama Inavyoonekana Pichani Msoma Lisara na kiongozi wa Soko la kitongoji cha Chatembo akimkabidhi Diwani wa kata ya Mwandege Nasoro Suleiman Nasorro changamoto zilizopo kwenye Soko lao la Chatembo. 

Lengo Diwani na Viongozi wenzake waweze kuzitatuwa . Mfano changamoto ya mitaji,kuboleshwa Kwa Soko,upatikanaji wa wajasiliamali ndani ya Soko na zinginezo.

Kwaupande wake Diwani wa kata ya Mwandege Kama Inavyoonekana Pichani akipokea Lisara uku akiaidi kuzifanyia kazi  changamoto zote zilizopo Soko la kitongoji cha Chatembo.

Habari picha na Ally Thabiti


DIWANI WA KATA YA MWANDEGE ABARIKI SOKO LA CHATEMBO


Nasorro Suleiman Nasorro awatoa Ofu na mashaka Wananchi wa Chatembo kata ya Mwandege Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani. Ameahidi kuwa ataakikisha Soko la kitongoji cha Chatembo linakamilika .

Na atawaunganisha na  fursa mbalimbali ivyo Diwani Nasorro Suleiman Nasorro ameitaka Uongozi wa kitongoji cha Chatembo na Viongozi wa kikunsi za Mwangaza wampe ushirikiano .

Habari picha na Ally Thabiti

Friday 10 September 2021

MWENYEKITI TCCIA MKOA WA NJOMBE KUWAFUTA MACHOZI WAKULIMA WA PALACHICHI


 Menard Rafael Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Njombe amesema  kutokana na Kilimo cha wafanya biashara na wakulima wa zao la Palachichi TCCIA Mkoa wa Njombe wameamuwa kutafuta Masoko ndani ya nchi na nje ya nchi .

Lengo wanachama hawa wanufaike kiuchumi  amesema jitihada zinafanyika za kuanzisha Viwanda vya kuongeza samaani kwenye zao la Palachichi Mkoa wa Njombe .

Menard Rafael amesema wameweza kuwatafutia pembe jeo na wamewapa elimu wakulima wa zao la Palachichi . Huku akitoa wito kwa wakazi wa Mkoa wa Njombe kujiunga na TCCIA Kwa maslai makubwa na mapana kwaajili ya biashara zao na mazao Yao .

Na Mafunzo alioyapata yataleta chachu kwenye Mkoa wa Njombe amesema haya jijini Dsm.

Habari picha na Ally Thabiti

AFISA WA TCCIA MKOA WA SONGWE AWATAKA WANA SONGWE KUCHANGAMKIA FURSA


 Elijah M. Simbeye ni Afisa Mtendaji wa TCCIA Mkoa wa Songwe amesema wafanya biashara Mkoa wa Songwe wajiunge na TCCIA kwani watapata mafanikio makubwa  .

Pia amesema Mafunzo alioyapata atayatumia vizuri katika Mkoa wake kwani ana mda mchache kwenye Uongozi lakini ameweza kutatuwa changamoto zilizokuwa zinawakabili wafanya biashara wa Mkoa wa Songwe.

Huku wakijiandaa wanatccia Mkoa wa Songwe kushiriki kwenye miradi midogo na mikubwa. Amesema haya jijini Dsm.

Habari picha na Ally Thabiti

TCCIA MKOA WA GEITA YACHANGAMKIA FURSA

Makamu Mwenyekiti wa Viwanda Mkoa WA Geita Judithi Karangi ambae anamwakilisha Mwenyekiti wa Mkoa  Geita TCCIA  .amesema kutokana na mradi wa bomba la mafuta wameweza kujipanga vyema ili waweze kupata fursa mbalimbali za kibiashara.

Judithi Karangi amewataka wakazi wa Mkoa wa Geita kuweza kujiunga na TCCIA  kwani moja ya faida watakazo zipata kutafutiwa Masoko,utatuwa changamoto za kikodi na tozo . Amesema haya jijini Dsm.

Habari picha na Ally Thabiti


 

Thursday 9 September 2021

MWENYEKITI WA TCCIA KIGOMA ABAINISHA FURSA ZA KIUCHUMI


 Abdull Mwilima Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Kigoma amewataka Wana Kigoma kujiunga na TCCIA kwani watapata fursa mbalimbali za kiuchumi . Kwani Mkoa wa Kigoma umekaribiana na nchi 4 na Mkoa huu Kwa mwaka unaibgiza kiasi cha Fedha bilioni Mia sita.

Amesema haya jijini Dsm kwenye mkutano wa TCCIA Taifa 

Habari picha na Ally Thabiti

DEUSI NYABIRI AISHAURI TCCIA MAMBO MAZURI

  • Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Dodoma Deusi Nyabiri amesema ni vyema wanachama wa TCCIA kukubali kujiunga na TLS kwaajili ya kutatuwa migogoro itakayokotokana na ukiukwaji wa mikataba ya kibiashara na makampuni au watu binausi.
Ambako itasaidia kuwepo Kwa maahauriano ya kisheria kupitia TLS .ambako faida kubwa ni kupunguwa Kwa gharama Kwa kutumia Kampuni ya ndani.

Amesema haya kwenye mkutano wa TCCIA .

Habari picha na Ally Thabiti
 

MWANA SHERIA WA MFUKO WA MAWASILIANO SAWA KWA WOTE ABAINISHA MIKAKATI MIZITO


 Freddy Ndonga ni Mwanasheria wa Mfuko wa Mawasiliano Sawa Kwa wote amesema Lengo lao watu kupata huduma Kwa urasi na haraka pia wanaboresha miundombinu ya Mawasiliano .

Freddy Ndonga mesema kata 200 zitajengewa minara ya Mawasiliano ,amewatoa hofu watu wenye Ulemavu kuwa watajengewa uwelewa wa pamoja .

Habari picha na Ally Thabiti

WADAU WA TEHAMA WAPONGEZA MFUKO WA MAWASILIANO SAWA KWA WOTE


 Yusuphu Hassani Afisa Tehama amewashukuru na kuwaongezea Viongozi wa Mfuko wa Mawasiliano Sawa Kwa wote Kwa kuimarisha na kuboresha miundombinu ya Mawasiliano .

Pia ametoa rai Kwa Viongozi wa Mfuko wa Mawasiliano Sawa Kwa wote kuongeza juhudi ya kuutangaza Mfuko huu .

Habari picha na Ally Thabiti

MWANDISHI WA TBC AVUTIWA NA MFUKO WA MAWASILIANO


 Shinuna Saidi ni Mwandishi wa  habari wa TBC ameipongeza Mfuko wa Mawasiliano Sawa Kwa wote Kwa kutoa elimu na kuongeza uelewa Kwa wadau wake . Ambako Shinuna Saidi ameweza kufaam Mfuko wa Mawasiliano Sawa Kwa wotekazi zake na Malengo yake.

Ametoa wito kwa Viongozi wa Mfuko wa Mawasiliano Sawa Kwa wote watumie Wanahabari katika kuitangaza Mfuko huu, pia watoe elimu zaidi Vijijini pamoja na mijini .

Habari picha na Ally Thabiti

Wednesday 8 September 2021

JULIAS TWENESHE KUTOKA OFISI YA WAZIRI MKUU AJA NA MIHAROBAINI KWA VIJANA


 Afisa Maendeleo Mkuu wa Vijana Kutoka OFISI ya Waziri Mkuu Julias Tweneshe amesema kuwepo Kwa rasimu ya Sera ya vijana yataleta mafanikio makubwa Kwa vijana .

Ivyo amewataka vijana kujadili na kutoa mawazo Yao namna ya kuleta majawabu yatakayowakwamuwa vijana kiuchumi, Julias Tweneshe amesema michango ya kimawazo yaliotolewa na watu wenye Ulemavu kwenye rasimu hii yatafanyiwa Kazina kutekelezwa Kwa vitendo. 

Amesema haya kwenye mkutano wa kujadili rasimu ya Sera ya vijana.

Habari picha na Ally Thabiti

MWANAFUNZI WA CHUO CHA DIT APAZA SAUTI KWA VIJANA


 Miriam Mkanza Mwanafunzi wa Chuo cha DIT amesema serikali kwenye Sera ya vijana kuwepo na namna ya kuwapa elimu ya Ujasilia Mali vijana , kuajiri vijana kwenye Sekta mbalimbali ,kuwapatia vijana mitaji ya kutosha bila riba kubwa ,Kuwajenga uwezo vijana waweze kujiajili .

Ambako itasaidia kujikwamuwa kiuchumi na kuondokana na umasikini Kwa vijana na kuwaondolea vikwazo vijana kwaupande wa Kodi katika biashara zao.

Miriam Mkanza Mwanafunzi wa Chuo cha DIT anaamini kuwa mabadiliko ya Sera ya vijana yataleta chachu kubwa na mapinduzi Kwa vijana katika kupiga atua kubwa za Maisha na Maendeleo ya Uchumi . Amesema haya jijini Dsm katika maboresho ya Sera ya vijana.

Habari picha na Ally Thabiti

ANSAFU YAWATOA OFU WAFUGAJI


 Mkurugenzi wa ANSAFU  Audax Rukonge  amesema kuwa serikali ikiwezesha kuwepo Kwa marisho Bora ,kuwepo na Sera borana maafisa Hugani itawezesha Kwa kiasi kikubwa kukuwa Kwa Sekta ya ufugaji Tanzania.

Habari picha na Ally Thabiti

KAIMU MKURUGENZI WA SERA NA MIPANGO MBARAKA SEMBURI ABAINISHA MIKAKATI MIZITO

Mbaraka Semburi Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango amesema katika kuimarisha Sekta ya mifugo wanaakikisha kuwepo na marisho yalio Bora ,matumizi ya mifumo ya kiteknolojia ,kuwepo na tafiti za kutakuwa changamoto zinazowakabiri wafugaji na mifugo Yao.

Tozo ambazo zilikuwa ni kikwazo Kwa wafugaji serikali emeziondoa . Pia Mbaraka Semburi amesema serikali imeweka mikakati ya kupatikana tilioni 5 kwaajili ya kuendeleza mifugo.

Swala la kuwepo Kwa ardhi kwaajili ya kutengeneza malisho serikali imezingatia ametoa wito kwa watanzania kuwekeza katika Uwekezaji kwani maafisa Hugani wapo wa  kutosha  Mazingira na miundombinu ni rafiki.

Amesema haya kwenye mkutano wa wadau wa Mifugo

Habari picha na Ally Thabiti
 

Tuesday 7 September 2021

PETER MSOFE ATOA NENO KWA WAFUGAJI


 Mkurugenzi Mtendaji wa NARKO Peter Msofe amewataka wafugaji kuchangamkia fursa kuwekeza kwaajili ya kulishia mifugo Yao kwenye ranji za NARKO , Pia amewataka vijana wa kitanzania waweze kufika NARKO kwani watapata Ajira 

Ambako NARKO Wana ranji 14 kwenye Mikoa 9 na karibuni watafunguwa ranji moja  mkoani Kagera amesema haya kwenye mkutano wa wadau wa Mifugo jijini Dsm.

Habari picha na Ally Thabiti

WAZIRI MKUU AZINDUWA ASASI YA NMB


 Majaliwa Kasim Majaliwa Waziri Mkuu wa Tanzania amesema anawapongeza NMB Bank Kwa kuanzisha Asasi ya kiraia kwani wataisaidia serikali Kwa kiasi kikubwa katika Sekta ya Afya,Kilimo,Mazingira, Elimu na Ujasilia Mali .

Ambako uzalishaji kwenye Sekta ya Kilimo utakuwa mkubwa hivyo anawataka watu wote watakaopata fursa Kutoka kwenye Asasi ya kiraia ya NMB Bank waitumie vizuri . Kama anavyoonekana kwenye picha ameambatana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Bank ya NMB Lusi Zaipuna wakizinduwa Asasi ya kiraia ya NMB.

Habari picha na Ally Thabiti

Monday 6 September 2021

MWENYEKITI WA NMB BANK AWAFUNDA VIJANA

 Dr Edwini Muhede Mwenyekiti wa Bodi ya NMB amewataka vijana wa kitanzania watakao pata fursa ya kusaidiwa na Asasi ya NMB kwenye Sekta ya Elimu watumie vizuri . Pia amezitaka Asasi zingine kushirikiana na Asasi ya NMB.

Habari na Ally Thabiti

HAMOSI MAKALA AIPONGENZA NMB

 Mkuu wa Mkoa wa Dsm Hamosi Makala ameipongeza  Bank ya NMB Kwa kuanzisha Asasi Yao kwani itawezesha Kwa kiasi kikubwa kutakuwa changamoto za watanzania. Kwenye Sekta ya Afya,Mazingira, Elimu, Kilimo, na Ujasilia Mali.

Hamosi Makala ameiomba NMB kusaidia ujenzi wa shule kwenye Mkoa wa Dsm.

Habari na Ally Thabit

NMB YAZINDUWA ASASI YAKE

 Afisa Mtendaji Mkuu wa  Bank ya NMB  Lusi Zaipuna amesema Lengo la kuzinduwa Asasi ya NMB kuweza kusaidia Sekta ya Afya,Mazingira,Elimu,Kilimo na Ujasilia Mali.

Lusi Zaipuna amesema NMB ina mawakala elfu kumi ,10000. Ivyo amewataka watu  kuiamini Bank ya NMB na waitumie.

Habari na Ally Thabit

Friday 3 September 2021

MWIJAKU AMPIGA MANALA


 Mwijaku amtaka Muamasishaji wa Tanga Haji Sandé Manala aacha kusema vibaya Timu ya Simba. pia Mwijaku amemtaka Manala Kama amesoma aoneshe vyeti vyake.

Habari picha na Ally Thabiti

VUNJA BEI KUINOGESHA SIMBA DAY


 Wakala wa Kuuza na Kusambaza Jezi za Timu ya Simba anawataka wapenzi,mashabiki na wafuasi wa Timu ya Simba wanunue jezi za Timu Yao kwaajili ya kuchangia Timu Yao.

Habari picha na  Victoria Stanslaus

JOHN BOSKO KALISA ABAINISHA CHANGAMOTO ZA KIBIASHARA E A C


 Mwenyekiti wa Baraza la EAC John Bosko Kalisa amesema maswala ya Forodha ,Ubora wa bidhaa na miundombinu,Soko la pamoja la kibiashara hizi ni changamoto zilizokuwa zikiwakabili wafanya biashara wa EAC.

Lakini zimejadiliwa na kufanyiwa kazi.

Habari picha na Victoria Stanslaus

KAMPUNI YA WLC YAJA NA MIKAKATI KABAMBE

Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Kampuni ya  World Logistics Company Limited (WLC) Agnes Daniel amewataka watu kutumia Kampuni Yao katika kusafirisha bidhaa zao .

Kwani gharama zao ni nafuu wameanza kazi  hizi mwaka elfumbili na nne 2004 Chino ya mwanzilishi Regnold George .ambako wanatumia Nyenzo ya Google Excel Spreadsheet.

Agnes Daniel Mkuu wa Kitengo cha Masoko amesema japo kunachangamoto ya KORONA 19 richa ya Kuenea Kwa ugonjwa wa KORONA wanaendelea kusafirisha mizigo nchi za  China,Uingereza,Japan, Afrika Kusini,Falme za Kiarabu,India,Malaysia na nchi zinginezo. 

Lengo la kuendelea na Usafirishaji Kwa gharama nafuu ni kumuunga mkono raisi  Samia Suluhu Hassan, katika kukuza Uchumi wa tanzania.

Habari na Victoria Stanslaus