Thursday, 30 November 2023
WIZARA YA ARDHI YAIPONGEZA LIBERTY SPARKS
Naibu katibu mkuu wa wizara ya Ardhi, nyumba maendeleo na makazi Dr. Pendo Makokolo amesema Liberty Sparks utafiti walioufanya ni mzuri kwani serikali itatumia report hii walioizindua kwaajili ya kuboresha sera, sheria, kanuni na taratibu ambazo zinamnyima mwanamke haki ya kumiliki ardhi.
Dr. Pendo amepongeza kwa kusema kuwa watafanya maboresho na kwenye mabaraza ya ardhi lengo kuweza kuweka mifumo thabit ili mwanamke aondokane na manyanyaso na matesho anapodai haki ya kumiliki ardhi.
Habari kamili na Ally Thabit
MWENYEKITI WA BODI WA LIBERTY SPARKS
Mwenyekit i wa Liberty Sparks ni vyema Serikali kuwapa elimu na uelewa wanawake waweze kumliki ardhi pia bunge litenge bajeti ya kutosha nakuweka mifumo rafiki kwenye mabaraza ya ardhi pamoja na mahakamaza. Yote haya yatafanyika migogoro ya Ardhi itapungua kwa kiasi kikubwa na wanawake watapa fursa yakuweza kumiliki ardhi
Mwenyekiti wa bodi wa taasisi ya LIBERTY SPAERK Dr Tumsifu amesema utafiti unaonesha kwenye ripoti yao asilimia 10% ya watanzania wanahati za Ardhi.
habari kamili na Ally Thabit
MKURUGENZI WA LIBERY SPARKS ATOA NENO JUU YA REPORT WALIOITOA
Evans ni mkurugenzi wa Liberty Sparks amesema wamefanya utafiti na kugundua kuwa wanawake wanakosa haki ya kumiliki ardhi nchini Tanzania hii yote kutokana na mila na desturi dhidi ya wanawake pia sheria ya mwaka 1967 haimpi haki mwanamke kumiliki ardhi hivyo upitia utafiti yaiomba serikali kuweka mazingira wezeshi ili mwanamke kumiliki ardhi ambapo mwanamke huyu itamsaidia kwa kiasi kikubwa kushiriki katika shughuli za kiuchumi ikiwemo kulima na shughuli zinginezo.
habari kamili na Victoria Stanslaus
LIBERTY SPARKS YAJA NA RIPOTI YA UMILIKI WA ARDHI KWA WANAWAKE
Dr. Samwel ni mshauri na mtafiti wa taasisi Liberty Sparks amesema wameamua kufanya utafiti kwa namna wanawake wanavyopata changamoto kwenye kumiliki Ardhi nchini Tanzania ambako kwa vijijini imekuwa ni tatizo kubwa sana ndio maana wameamua kufanya utafiti huu lengo serikali iweze kubadili sela, sheria, kanuni na taratibu kandamizi dhidi ya wanawake katika kumiliki ardhi.
Habari kamili na Ally Thabith
UGANDA YAIPONGEZA TEMINATE KWA MKUTANO WA ELIMU
Mwakirishi kutoka Uganda John Samwel amesema mkutano ulioandaliwa na mtandao wa elimu nchini Tanzania utasaidia kwa kiasi kikubwa kukua kwa elimu Tanzania na Africa kiujumla.
Habari picha na Ally Thabith
TBA YAANZA KUWAONDOA WADAIWA SUGU DAR ES SALAAM
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mkoa wa Dar es Salaam umeanza zoezi la kuwaondoa wapangaji waliolimbikiza madeni ya kodi ya pango.

