Tuesday 14 November 2023

MEA WA DAR ES SALAAM AWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI VIWANJA VYA MNAZI MMOJA KUPIMA MAGONJWA YASIOAMBUKIZA

 


Omary Kumbilamoto Mstahiki mea wa Jiji la Dar es Salaam amewataka wananchi wote wa Dar es Salaam na mikoa jirani wajitokeze kwa wingi kupima afya zao na kupata huduma bure kwa magonjwa yasioambukiza viwanja vya mnazi mmoja kuanzia tarehe 14/11/2023 mwisho tarehe 18/11/2023 pia kutakuwepo na utoaji wa elimu wanamna kukabiliano na magonjwa yasiyoambukiza mfano kansa, Figo, Kisukali, Presha na mengineyo.

Omary Kumbilamoto ameshukulu wizala ya afya kwa kutoa huduma hii bure kwani wataokoa maisha ya watu wengi pia amemshukuru mweshimiwa Rais Dr. Samia Saluhu Hassan kwa kuweka kutoa vifaa tiba kwa wizara ya afya.

Habari picha na Ally Thabiti 

No comments:

Post a Comment