Saturday, 6 November 2021

TAASISI YA MWANAMKE NI TUNU YAWAKOMBOA WANAWAKE


 Mkurugenzi wa Taasisi ya MWANAMKE NI TUNU Adera amesema Lengo lao ninkuwainuwa wanawake kiuchumi ambako wameweza kuwafikia wanawake zaidi ya elfu moja nchini Tanzania. Pia Wana matawi jijini Mbeya ,kanda ya kaskazini, Mkoani Iringa na Mikoa mingineyo .

Habari picha na Ally Thabiti

TARURA YAJA NA MIKAKATI MIZITO DSM


 Meneja wa Talura Mkoa wa Dsm Bwana Mkinga amesema wamepokea maelekezo ya maboresho ya mfumo wa Ukusanyaji wa tozo za uegeahaji wa magari Kwa njia ya mtandao yaliotolewa na Waziri wa Tamisemi Humi Mwalimu watayafanyia  kazina kutekeleza Kwa vitendo. 

Ikiwemo kutoa elimu ,matumizi ya Lugha nzuri na mengineyo. Pia amesema watu wenye Ulemavu watashirokishwa Kwa kiasi kikubwa .Mkinga ametoa wito Kwa waegesha magari Kwa Dsm kutoa ushirikiano wakati WA utoaji elimu na Baada ya mfumo kurejeshwa tarehe 1/12/2021.

Lengo ni kudhibiti upoteaji wa mapato ya Maegeaho ya magari.

Habari picha na Ally Thabiti

WIZARA YA TAMISEMI YATATUWA KELO YA MFUMO


 Waziri wa Tamisemi Humi Mwalimu amesema Kwa kushirikiana Tarura wametatuwa kelo zilizokuwa zimejitokeza kwenye mfumo wa tozo za kukusanya maeneo  ya Maegeaho ya magari .

Kwani watu walipokuwa wakiegesha magari yao waliweza kubainisha changamoto walizokutana nazo jijini Dsm wakati wa kulipa Kwa njia ya mtandao ...Ikiwemo kupigwa faini ya elfu30,kutopewa taarifa za madeni,kutopewa namba ya malipo,Lugha chafu Kwa watumishi na zinginezo.

Waziri Humi Mwalimu amesema Kwa sasa mteja atatozwa shilingi elfu kumi Kama atachelewa kulipa ndani ya siku 14, Kwa sasa atatozwa shilingi 500 na Kwa siku 2500 Baada ya kuegesha gari.  Pia Waziri ameitaka Talura kutoa elimu Kwa waegesha magari ndani ya siku 21 kwani mfumo huu utaanza tena tarehe 1/12/2021.

Waziri Humi Mwalimu ametoa wito Kwa waegesha magari nchi mzima kutumia mfumo huu Kwa kulipa tozo Kwa njia ya mtandao kwani inasaidia kutokupotea pesa za serikali.kabla ya kutumia mfumo huu Dsm ilikuwa inakusanya milioni25 na Baada ya kutumia mfumo huu imekusanya milioni 40.

Humi Mwalimu ametoa Rai Kwa Talura kutoa asilimia 40 ya Fedha kupelekwa kwenye halmashauri pia kutowachaji tozo ya Maegeaho watu wenye Ulemavu kupitia Sura ya 288.

Habari picha na Ally Thabiti

Thursday, 21 October 2021

MWENYEKITI WA NCCR MAGEUZI ATANGAZA VITA


 James Mbatia Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi amewataka Viongozi wa Serikali ya Tanzania,wanasiasa, Viongozi wa Kidini, Viongozi wa kimira na kijadi na watu wote wawapige Vita na wawapige watu wote wanaoalibu UTU wa Watu. 

kwani kutowapiga Vita watasababisha kuvunjika Kwa Amani na utulivu wa nchi yetu ya Tanzania .

Habari picha na Victoria Stanslaus

MENEJA WA TANROAD AHAIDI MAZITO


 Japhet Kivuyo Meneja wa TANROAD wa Mizani amesema Kwa sasa wanafanya makongamano na semina mbalimbali Kwa wadau mbalimbali wa Usafirishaji namna ya kutumia Mizani ambako wameanza elimu Kwa Mkoa wa Dsm na Pwani na wamefurahishwa na mwitikio mkubwa wa wadau wa Usafirishaji na jinsi walivyopokea Mafunzo haya.

Mikoa mingine watakayoenda Lindi ,Mtwara,Dodoma,Singida ,Morogoro,Tanga Iringa,Mbeya Ruvuma,Katavi,Geita,Mwanza,Arusha na Mikoa mingine. Lengo la semina hizi ni kuwaongezea uwelewa na ufahamu  na umuhimu wa kuzingatia Sheria,kanuni na Taratibu za Mizani.

Ametoa wito Kwa wadau wa Usafirishaji wazingatie Uzito unaotakiwa kwenye magari Yao kwaajili ya kutunza na kulinda barabara na madaraja hili yaweze kudumu Kwa muda mrefu.

Kwani wakizingatia haya tutapunguza gharama za ujenzi wa barabara na madaraja ambako Fedha hizi zitasaidia katika kutatuwa Changamoto ya Afya, Elimu,maji na maeneo mengineyo.

Japhet Kivuyo Meneja wa TANROAD amesema haya wakati wa semina na wadau wa Usafirishaji jijini Dsm.

Habari picha  Victoria Stanslaus

TANROAD YAJIVUNIA


 Mkurugenzi wa Matengenezo ya Mizani TANROAD amesema mpaka sasa wameweza kuiboresha na kuimarisha Mizani ya kupinga Nagari .amewataka wadau wa Usafirishaji wazingatie sheria ,kanuni na Taratibu za Mizani .

Lengo la TANROAD kuweka Mizani ya kupinga magari hili kudhibiti Uzito uliopitiliza ,ambako kutaepusha uhalibifu wa barabara na madaraja.

Amesema moja ya jitihada anazofanya kutoa elimu na kufanya semina mbalimbali Kwa wadau wa Usafirishaji.

Habari picha Ally Thabit

MCHUNGAJI ATAKA WATU KUZINGATIA UTU


 Mchungaji Masanja anawataka Watu Wote Kuzingatia UTU kwani Ndio msingi wa Amani pia amekipongeza Chama cha NCCR Mageuzi Kwa kuzinduwa Kampuni ya UTU .

Ivyo amevitaka Vyama vingine kuunga mkono .

Habari picha na Victoria Stanslaus