Friday, 6 September 2019

WANAHARAKATI VIJANA WAPEWA MBINU NZITO

                                        WANAHARAKA VIJANA WAPEWA MBINU

ELIZABETH JOSEPHAT, Ni mwanaharakati kijana  KUTOKA TGNP MTANDAO amesema mafunzo aliyoyapata ya kutumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kupinga ukatili wa kijinsia atatumia vizuri. Nae LILIAN SECHELELA MADEGE Amesema anazidi kutoa elimu na mafunzo kwa wanaharakati vijana jinsi ya kutumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kufichua maswala ya kijinsia ametoa wito kwa vijana waache kutumia mitandao ya kijamii kwa kuweka picha za ngono amesema haya kwenye makao makuu ya TGNP MTANDAO MABIBO jijini DAR ES SALAAM
Habari picha na ALLY THABITI  

Wednesday, 28 August 2019

MAKONDA AWATANGAZIA NEEMA WANAUME WALIOTOSWA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Sala PaulMakonda amesema anapeleka maombi bungeni kuwepo na Sheria ya wanaume ambao walioahidiwa na wapenzi wao kuwa wakiwanunulia magali au kuwajengea nyumba za kifahari watawaoa baada ya kufanyiwa hivyo hao wanawake wanachukuwa hizo mali na kukataa kuolewa na hao wanaume hivyo ameliomba Bunge la Tanzania kutunga Sheria Dhidi ya wanawake wenye tabia hizi lengo kukomesha na kuondoa utaperi wa namna hii.
Amesema haya Jiji Dar es Salaam kwenye Ofisi yake wakati akiongea na wanahabari.
Habari picha na Ally Thabith

BODI YA FILAMU YATANGAZA VITA KALI


Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya filamu Dr. Kiagho amekamata CD ambazo hazina vibali na kutoa onyo kali kwa wote ambao wanasambaza CD ambazo hazina vibali kwani hatua kali zidi yao zitachukuliwa uku akisema kusambaza CD ambazo hazina vibali ni uhujumu uchumi kwani Serikali inapoteza mapato yake na uku wachache wakinufaika kama inavyoonekana pichani akiwa ameshikilia CD ambazo hazina vibali baada ya kubaini nakwenda kuzikamata. Ametoa wito kwa wananchi wa Wasanii wa Filam kutoa Taarifa pindi watakapo baini kuna watu hawalipi vibali vya CD kupitia bodi ya filamu.

Amesema haya Jiji Dar es Salaam kwenye ofisi ya bodi ya Filamu akiongea na wanahabari na akiambatana na viongozi wa Bodi ya Filamu.
Habari Picha na Ally Thabith 

ELIMU SOLUTION YALETA CHACHU NA MAPINDUZI MAZITO SEKTA YA ELIMU


Meithani Swedi mkurugenzi wa Elimu Solution amesema wameamua kutoa Tuzo kwenye Sekta ya Elimu lengo kuwamasisha wanafunzi wasome kwa bidii na waweze kufaulu kwa kiwango kikubwa kwenye Mitihani yao, Pia kuleta muamko kwa walimu wawe Molali na Juhudi za kufundisha na kuletha hamasa kwa wadau mbalimbali kutoa michango yao kwenye Sekta ya Elimu.
Mkurugenzi wa Elimu Solution amesema washiriki zaidi ya 70 watawania Tuzo za Elimu Award Tarehe 31/08/2019 viwanja vya mlimani city. Ambako mgeni Rasmi atakuwa waziri wa Serikali za mitaa Selemani Jafu Mkurugenzi wa LEmu Solution wanafunzi wenye ulemavu na walimu watapa tuzo kwa Juhudi walizozifanya na ufaulu waliouonyesha kwenye Elimu pia kutakuwa na zawadi kwa wilaya iliyofanya vizuri. Watanzania, Afrika Mashariki na kati na Afrika kwa ujumla ni mala ya kwanza Tuzo za Elimu zinatolewa Tanzania na Afrika kwa Ujumla
Amesema haya jijini Dar es Salaam kwenye Hotel ya Selena
Habari Picha na Ally Thabith

CATHERINE AWATAKA WADAU KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI





























Catherine Ndosi amewataka wadau mbalimbali wa muunge mkono Raisi Magufuli kwakuchangia Sekta ya Elimu Catherine Ndosi amewataka watanzania na wasio watanzania kujitokeza kwa wingi kwenye viwanja vya mlimani city tarehe 31/08/2019 kwenye Elimu Awards ambazo tuzo hizi zitatolewa na Elimu Solution. Catherine Ndosi ameshukuru Kampuni ya ASAS, AZAM TV na COCACOLA kuwazamini na kufanikisha tuzo hizi,
Amesema haya jijini Dar es Salaam kwenye Hotel ya Selena.

Habari Picha na Ally Thabith

KAMPUNI YA ASAS YAIPA TANO TANZANIA ELIMU AWARDS


Abdul Twalib amesema wanaipongeza Taasisi ya Elimu Solution kwa kuandaa tuzo therasini na mbili kwa kategori 11 ambazo tuzo hizi zitatolewa tarehe 31/08/2019 katika ukumbi wa mlimani city.
Amesema kampuni ya ASAS inamiaka 19 katika biashara na usambazaji wa maziwa na bidhaa nyingine ambapo mpaka hivi sasa lita za maziwa laki tatu zimetolewa bure kwenye shule mbalimbali hapa nchini Tanzania na Kampuni ya ASAS lengo ni kuwafanya wanafunzi wapate Elimu bora na kuunga mkono juhudi za Rais magufuli kwakuelekea Tanzania ya Viwanda na uchumi wa kati.
Abdul Twalibu pichani akiwa kushoto ambaye ndio mzamini mkuu wa Elimu Awards kutoka kampuni ya ASAS amesema haya Jijini Dar es Salaam kwenye Hotel ya Selena.

Habari Picha na Ally Thabith

Tuesday, 20 August 2019

Leah Mollel mshiriki wa maoenesho katika mkutano wa nchi jumuiya ya maendeleo kwa nchi za kusini mwa afrika SADC akizungumzia changamoto wanazokutana nazo watoto wa kiafrika na kusababisha kushindwa kuendelea na masomo sababu ya umbali wa shule na kulazimishwa kuolewa wakati wakiwa bado wadogo kiumri. Picha na ALLY THABITI

Moja ya washiriki wa maonesho ya nchi jumuiya ya SADC Kwa jina la Poges akiongelea changamoto wanazokabiliana vijana wanaopatikana kwenye nchi zinazounda jumuiya hiyo nakutoa pendekezo kuwa mkutano huo ulete tija ya kutatua changamoto hiyo ili vijana waendelee kujivunia kuishi kwenye mataifa yao nakuongeza uazalendo. Picha na ALLY THABITI

Mkurugenzi wa shirika la Oxfam Francis Odokorach akielezea namna shirika lao linavyoendelea kutoa elimu kwa wanawake ili waweze kujikwamua kiuchumi na kupambana na hali ngumu ya uchumi akitolea mfano kabila la wamasai ambao wamejitahidi kuwakwamua kielimu ili waweze kusimamia miradi yao na kupiga hatua za kimaendeleo? Picha na ALLY THABITI