Thursday, 18 February 2021

KAIMU MSAJILI WA BODI YA NYAMA AWAPA FARAJA WAFUGAJI WA KUKU

 


Imani Sichalwe kaimu msajili wa bodi ya nyama ameweza kuwakutanisha wafugaji wa kuku na wadau wanao uza chakula cha kuku vifaranga vya kuku, watalaam wa mifugo, benki ya CRDB pamoja na waziri wa mifugo na uvuvi Mashimba Ndaki lengo kukuza na kuistawisha sector ya ufugaji kuku ambapo changamoto zifuatazo ziliweza kujadiliwa na kupatiwa ufumbuzi ikiwemo ukuaji wa bei na viranga vya kuku kutoka shilingi 1700 hadi 2300 ambapo hiki ni kilio kikubwa cha wafugaji kuku Dar es Salaam. Bei ya chakula cha kuku bei yao imekuwa kubwa swala la kuuza kuku kwa kilo wafugaji wa kuku wamewasilisha kwa waziri na kutafutiwa masoko na machinjio ya kuku. 

Kaimu msajili wa bodi ya nyama amesema amehitisha kikao hiki ili kumsaidia Rais Magufuli katika hazima yake ya ujenzi wa viwanda na kukuza uchumi wa Tanzania ambapo wafugaji hao wa kuku watasaidia kwa kiwango kikubwa katika kukua uchumi wa Tanzania, amewatoa hofu wafugaji wakuku nchini Tanzania kuwa Bodi ya nyama imewawekea mazingira ya rahisi na rafiki ili waweze kujikwamua kiuchumi na milango ipo wazi kwa watakao hitaji mawazo, ushauri na wataalam, amesema vikao hivi vitakuwa vinafanyika mara kwa mara huku akiwataka wauza viranga vya kuku na chakula cha kuku pamoja na chanjo za kuku wasiwakandamize na kuwaonea kwakuwauzia viranga vya kuku visivyokuwa na ubora dawa pamoja na chakula wakifanya hivyo watauwa mitaji ya wafuagaji kuku amesema. Amemshukuru waziri wa mifugo na uvuvi Mashimba Ndaki pamoja na Mkuu wa wilaya ya Ilala kwa kuwaweza kuwasiliza wafugaji kuku na kutatua kero na changamoto zinazowakabiri wafugaji kuku.

Habai picha na Ally Thabith 

Tuesday, 9 February 2021

AIRTEL YAPASUA ANGA


Airtel yaboresha mtandao kwenda masafa ya Supa-4G. Yaja na ofa kabambe za internet

  1. Ukianza kutumia aini ya Airtel utapata intaneti mara mbili bure BURE kwa kipindi cha miezi sita (Airtel dabo Data)
  2. Airtel imepunguza bei ya Airtel Mi-Fi kwa kurudisha GB 40 bure ili wateja wafuahie mtandao wa Airtel supa 4G kwenye simu za 3G.
  3. Airtel inatoa 7GB bure kwa wateja wote ambao watabadili laini kutoka 3G kwenda laini 4G
Dar es Salaam tarehe 09/02/2021. kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza kukamilisha maboresho makubwa kwenye mtandao wake wa 4G kwenda kwenye masafa ubora zaidi ya Airtel Supa 4G ili wateja wake waendelee kuperuzi kwa uharaka zaidi popote. Akizungumza jijini Dar es salaam leo wakati wa kutangaza maboresho ya masafa hayo ya Airtel supa 4G, Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema kuwa kwasasa "wateja wa Airtel kupitia maboresho ya mtndao wa Airtel Suapa-4G watapata huduma bora zaidi ya ilivyokuwa awali, watafurahia kuperuzi mtandao kwa kasi zaidi ndani ya miji mikubwa zaidi ya 500 nchini Tanzania iliyofanyiwa maboresho haya ya kufurahia huduma za kidigitali kama video za mfumo wa HD.

Tumewekeza kwa kiasi kikubwa katika maboresho ya mtazamo wetu ili kukamilisha ahadi yetu ya kutoa huduma bora ya intaneti (Data) pamoja na huduma za kupiga simu kimataifa kwaajili ya wateja wetu.

Huduma ya Airtel Supa 4G inapatikana kwenye masafa y a700MHz NA 2100 MHz, ambapo kasi yake inawezesha wateja wetu sasa KUPERUZI kwenye mtandao kwa kasi ya 40Mbps kasi hii inafanya huduma yetu kimtandao kufikia viwango vya kimataifa zaidi na kwafaidisha wateja wote.

Mkurugenzi huyu wa mawasiliano wa Airtel Tanzani ameongeza kuwa kufuatia kuambaa kwa mtandao huu wa supa 4G, Airtel tumefanya mawasiliano kuwa nafuu zaidi kwa wateja wetu ili kufaidi mtandao wa Supa - 4G. Airtel saas imezindua huduma tatu kwa wateja ambazo zinapatika kwa kasi zaidi ili kuperuzi kutpita supa 4G ambazo ni 

  • Wateja wote wa Aitel ambao wanatumia laini za 3G endapo watabadilisha laini zao za simu kwenda kwenye mfumo wa 4G watapata ofa ya 7GB ndani ya wiki mbili bure
  • Ipo ofa ya intaneti mara mbili (Dabo data) kwa wateja ambao wataanza kutumia smartphone zao kwa mara ya kwanza na mtandao wa Airtel kwa miezi 6
  • Airtel tumepunguza bei ya Airtel Mi-Fi sawa na Tsh 75,000 ikiwa na 40 G0GB bure sawa punguzo la shilingi 30,000. Mi-Fi hii pia itawezesha wateja asio na simu za smartphone za 4G kutumia Mi-fi na kufurahia kasi ya Airtel Supa 4G yenye uwezo wa kuunganisha zaidi ya wateja 10 kwa mara moja
Nae Meneja wa huduma za intaneti wa Airtel Ezekiel Kahatano ilielezea kuwa "uzinduzi wa Mtandao wa Airtel 4G-supa pamoja na kuanzisha ofa za bei rahisi za Airtel Supa 4G ni sehemu ya mipango ya Airtel ya kuboresha huduma za mawasiliano na kukuza utumiaji wa kuperuzi mtandao wa Airtel kwa kasi ya Airtel supa 4G kwani inakuja na teknolojia ya kisasa inayolenga kupunguza gharama za huduma za mawasiliano.

Habari na Ally Thabiti



Monday, 25 January 2021

WHO YALIA NA UKEKETAJI

kila ifikapo tarehe 6 mwezi pili ni siku ya kupinga ukeketaji ambako maswala makubwa yatokea baada ya mtoto wa kike kukeketwa ikiwemo kutokwa na damu nyingi na kupelekea kifo kwa mkeketwaji pia wakati wakujifungua mzazi hufa au kiumbe kinachozaliwa hufariki ndio maana WHO imekuja na mpango mikakati ya GVV lengo kutokomeza maswala ya ukeketaji Tanzani, Afrika na ulimwenguni kwa ujumla

kwa mwaka zaidi ya mamilioni ya wakeketwaji hufariki na wengine wanabaki na makovu shinyanga na mikoa mingine ni vinara katika maswala ya ukeketaji. WHO imetoa wito kwa watanzania na ulimwengu kwa ujumla kupinga na kutokomeza mila na desturi zilizopitwa na wakati.

Habari picha na Ally Thabith

TAKUKURU YATEMA CHECHE



Mkuu wa Takukuru wa Temeke Ndugu Kessy amesema watu watoe taarifa zinazohusiana na maswala ya kuombwa rushwa au zakutoa rushwa kupia namba 113  lengo katika huduma mbalimbali zitolewe kwa haki bila uonevu wameweza kuokoa kiasi cha Shilingi milioni ishirini na tatu na zaidi wamesimamia kesi nne mbili wameshinda na wanasimamia miradi yenye thamani ya bilioni therathini na saba huku wakianzisha virabu mbalimbali vyakupinga rushwa.

Habari Picha na Ally Thabith

 KAMISHINA MSAIDIZI WA USALAMA BARABARANI AINISHA MIKAKATI MIZITO

Ndugu Mutafungwa Kamishina Msaidizi wa Barabarani amesema wamejipanga katika kuzibiti ajali barabarani kwa kuwachukulia hatua kali wale wote wasiofuata kanuni, Sheria na utaratibu wa sheria barabarani ndugu mtafungwa amepongeza shirika la afya duniani WHO kwakuisaidia serikali ya Tanzania dhidi ya mapambano ya kudhibiti ajali za barabarani kwa kuja na mradi wa kutoa elimu kwa wanahabari jinsi ya kuandika maswala ya barabarani pamoja na kuwapa elimu wanasheria amesema haya kwenye semina iliyowahusisha wanahabari Jijini Dar es Salaam nayo wizara ya Afya wamesema ajali barabarani zikipungua nchini zitasaidia kupunguza vifo kwa wingi na gharama za kuwatibu waga wa ajali zitatumika kwenye maendeleo ya nchi nao WHO wamawataka wanahabari kupaza sauti zao na watumie karamu zao vizuri ili ajali zisitokee nchini Tanzania.

Penina ni mwanahabari kutoka gazeti la majira kwa niaba ya wanahabari wenzake ameipongeza serikali, jeshi la polisi pamoja na WHO kwa kuwapa mafunzo ya kuwajengea uwezo jinsi ya kuandika habari za barabarani.

Habari na Ally Thabith

Monday, 18 January 2021

RAIS AVALIA NJUGA MIGOGORO YA NDOA

 Aliyekuwa Mgombea wa Urais kupitia chama cha Chadema DKT. MAYROSE KAVURA MAJINGE ameamua kuanzisha taasisi ya kushughulikia matatizo ya wanandoa pamoja na wachumba ambayo inaitwa The family is the firts assential cell of human society " tafsiri yake ni kuwa "Familia ni chembe muhimu ya kwanza ya jamii ya binadamu" amesema migogoro ya ndoa inazolotesha uchumi wa mtu na Taifa na ufanisi wa kazi unapotea.

Hivyo taasisi hii itakuja kuwa mwarubaini wa matatizo haya ambako watatoa elimu ya sili pamoja video tarehe 20/01/2021 taasisi hii itazinduliwa msimbazi centre saa 12:00 jioni wote munakaribishwa bila kiingilio.

Habari na Ally Thabiti

Sunday, 17 January 2021

 


JATU PLC YAMUUNGA MKONO RAIS MAGUFURI

meneja wa JATU PLC SIMBA SINGANO amesema kuwa wamekuja na programu ya kuwafikia wanafunzi wa vyuo lengo waweze kujiajili kwenye kilimo ambako asilimia 50 ya ajira zilizopo nchini zinatokana na kilimo program ya UNI TALK ikaibua fursa mbalimbali hapa nchini na lengo ni kumuunga mkono raisi magufuri kwa kutekeleza hilani chama cha mapinduzi kwa kuzalisha ajira mbalimbali ndio maana JATU PLC imeingia mkataba na MISS TANZANIA wa mwaka 2018 ili awe balozi wa JATU PLC kwa mwaka mmoja nae balozi wa Jatu ambae Elizabeth Miss Tanzania 2018 amewatoa mchecheto watanzania kuwa kilimo kinaweza kuwakwamua kiuchumi huku akiahidi kuwa atakuwa balozi mzuri na atatembelea vyuo vyote kumi na watu wenye ulemavu watafikiwa kwa kiwango kikubwa.


Habari na Ally Thabith