Sunday, 30 April 2017

Afisa wa PSPF awataka wafanyakazi wa MOI wajiunge na mfuko wa PSPF

Abdul Njaidi amesema hayo kwenye mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa MOI lililofanyika wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam. Bwana Njaidi ameainisha mikopo inayotolewa na PSPF kuwa ni mikopo ya Nyumba, Viwanja, Elimu na Fao la uzazi kwa akina mama.

Tuesday, 25 April 2017

VIONGOZI WA BARAZA LA BIASHARA WATOA TAARIFA YA KUZINDULIWA KWA BARAZA HILO TAREHE 05/05/2017 NA RAISI MAGUFULI

Katibu wa baraza la biashara la taifa Raymond Mbilinyi akiambatana na katibu mtendaji wa baraza la biashara sekta binafsi James Simbei wakiongea na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa baraza la wafanya biashara lililoundwa tarehe 03/12/2015 na Rais John Pombe Magufuli,( Picha na Mwandishi wetu )
pichani akikaribishwa na mkuu wa mkoa dodoma DANIELI RIGIMBANA rais JOHN POMBE MAGUFULI

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI AWASIRI DODOMA

rais JOHN POMBE MAGUFULI amewasiri mkoani dodoma kwaajiri ya sherehe ya miaka 53 ya muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar . kilele chake kitakuwa tarehe26 mwezi 4 /2017

MUFTI MKUU AWATAKA WATANZANIA WAWE MABALOZI WAKUKEMEA DAWA ZA KULEVYA

Mufti mkuu wa Tanzania Abubakary Zubery akiongea na wadau mbalimbali waliojitokeza kwenye kongamano la kupinga dawa za kulevya na kuwataka watanzania wote wawe mstari wa mbele kupinga matumizi ya dawa hizo pamoja na biashara haramu inayohusu mihadarati huku akiwapongeza viongozi mbalimbali walio mstari wa mbele katika kukemea dawa haramu za kulevya.

TAASISI ZA KIDINI ZATAKIWA KUPINGA DDAWA ZA KULEVYA

Waziri mkuu wa Tanzania akitoa pongezi kwa baraza la waislamu Tanzania BAKWATA kwa kuitisha kongamano lakupinga matumizi na biashara ya dawa za kulevya na akizitaka taasisi nyengine za kidini wafanye makongamano kama haya ili kuweza kuwanusuru vijana na athari zitokanazo na dawa hizo za kulevya huku pia wakitumia mikutano ya hadhara kuonya matumizi ya dawa hizo ambazo ni adui wa nguvu kazi ya Taifa. 

UVCCM WAKANUSHA UVUMI KUHUSU FIGISUFIGISU ZA UTEUZI WA JOKATE

Katibu mtendaji wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka akitolea ufafanuzi kuhusu habari za uzushi kuhusu uteuzi wa Jokate Mwegelo aliyekaa upande wa kushoto kuwa mwenyekiti wa uenezi na uhamasishaji wa vijana wa ccm na pia akielezea mafanikio ya miaka 53 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiwemo suala zima la kuimarika kwa demokrasia na maendeleo ya kiuchumi na kuimarisha idara mbalimbali ndani ya ofisi ya UVCCM.