Sunday, 25 June 2023

MSEMAJI WA SERIKALI ABAINISHA MAMBO MAZURI YA D.P WORLD

Gerson Msigwa amesema mafanikio tutakayopata kutoka kwa D.P world kiwango cha ukusanyaji kodi kitaongezeka kutoka tilioni 7.7 kwa mwaka hatimaye Tanzania tutakusanya tilioni 26 pia hajira za watanzania zitaongezeka kwa kiasi kikubwa vilevile tone za mizigo zitakuwa nyingi kuringanisha na sasa, ambako mizigo hii itabebwa na reli ya SGR vilevile upakuaji wa mizigo kwenye meri utafanyika kwa muda mfupi ukiringanisha na sasa.

Msingwa amesema Bandari yetu inachngia kodi kwa asilimia 37%  D.P World wakiwekeza kwenye bandari yetu utachangia bajeti kwa asimilia 67%. Pia meri zinazopo chelewa kutia nanga kwenye bandari yetu inalipa faini milini 60%

Meli zinakuwa zaidi ya ishirini D.P WORLD wakiwekeza kwenye bandari yetu hakutokuwa na uchelewedshwaji wa meri kuti mamga.

Msingwa ametoa wito kwa watanzania kuwapuuza na kuwabeza wanaopotoshwa uwekezaji wa T.P wor;ld kwenye bandari yetu kwa hawa D.P word wanabandali 190 Duaniani na wapo kwenye nchi 70 duniani, hivyo ni vyeama kumunga mkono Dr. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaleta D.P nchini Tanzania

haabrio kamili na ally Thabit

SHEKH JALALA AELEZA WASIFU WA MUFT TANZANIA

 Shekh Jalala amesema kipindi cha miaka nane cha mufti wa Tanzania amejifunza mambo mema na mazuri.

habari kamili na Ally Thabith

MUSSA HAJI ASHANGAZWA NA WANAOBEZA MAFANIKIO YA MUUNGANO NA MAPINDUZI YA MWAKA 1964

 Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Zanzibar Mussa Haji Mussa, amesema kubeza na kudhihaki mafanikio yaliyopatikana chini ya Muungano na Mapinduzi ya mwaka 1964 haviwezi kuwa tiketi ya kufikia malengo ya kisasa ya Chama Cha ACT-Wazalendo.

Kauli hiyo aliitoa Naibu Katibu Mkuu huyo, wakati akizungumza katika mahojiano maalum huko Afisi Kuu ya UVCCM Zanzibar Gymkhana, alisema mafaniko yaliyopatikana ndani ya miaka 60 ni kielelezo tosha cha wananchi wa Zanzibar kuendelea kuamini,kupenda na kuunga mkono sera na siasa za CCM inayosimamia Serikali zote mbili nchini.

Alisema tabia za viongozi wa ACT-Wazalendo za kubeza na kudharau hatua kubwa za maendeleo zilizofikiwa chini ya tunu za Muungano na Mapinduzi ya mwaka 1964,haziwezi kuwatengenezea uaminifu wa kisiasa kwa wananchi kwani ni porojo zisizokuwa na dhamira ya kuleta maendeleo nchini.

Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo Mussa, alisema baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani wamekuwa wakijisahau kwa kutumia majukwaa ya kisiasa kueleza uongo,upotoshaji na kuchochea ubaguzi dhidi ya taifa badala ya kushauri  Serikali mambo yenye tija kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

“Chama cha ACT-Wazalendo wameishiwa na sera kwani badala ya kuibua hoja zenye mashiko na kuishauri Serikali mambo mema ya kuimarisha masuala mbalimbali katika nyanja za kiuchumi,kisiasa,kijamii na kiutamaduni, wao wanabeza na kuzikashifu Serikali zilizowasomesha na Kuwapa madaraka waliyonayo hivi sasa.

Vyama vya upinzani nchini wanatakiwa wakae miaka zaidi ya 200 kutafakari kwa kina njia bora za kushindana na CCM katika medani za kisiasa katika dhana ya kidemokrasia kwani sisi kazi yetu ni kupanga,kufuatilia,kusimamia kisha kutenda kwa vitendo na hatimaye kutoa matokeo chanya yenye manufaa kwa wananchi wote”, alifafanua Mussa.

Mussa, alisema ACT-Wazalendo imeendelea kutumia vibaya haki ya mikutano ya hadhara kwa kukiuka dhamira ya ruhusa ya uwepo wa mikutano hiyo nchini iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, iliyokuwa na malengo ya kukuza demokrasia na ushindani wa kisasa na sio kauli za hoja za chuki dhidi ya Serikali.

Alisema hakuna mwananchi yeyote visiwani Zanzibar ambaye hakuguswa na dhulma,uonevu na ubaguzi wa utawala wa kigeni  kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964, hivyo wanasiasa wanaojitokeza hivi sasa wakaunga mkono hadharani utawala huo watakuwa na ajenda za siri za kutaka kurejesha utawala huo jambo ambalo haliwezekani kwa zama za sasa.

Pamoja na hayo alieleza kwamba kupitia Serikali zote mbili ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zitaendelea kuwahudumia wananchi kwa uadilifu mkubwa sambamba na kuendelea kufungua milango ya uwekezaji na diplomasia zenye tija na maslahi kwa nchi.

Aidha, alisema UVCCM Zanzibar  itaendelea kulinda,kutetea na kujenga hoja imara juu ya kupinga kauli na vitendo vyote  visivyofaa katika michakato ya siasa za kidemokrasia vinavyofanywa na vyama vya upinzani kupitia majukwaa ya kisiasa visiwani Zanzibar.

Pamoja na hayo Mussa, aliwapongeza Marais wote wawili ambao ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 na kuibua miradi mikubwa ya maendeleo,inayoendelea kutoa fursa za ajira kwa vijana nchini.

habari kamili na Ally Thabit

RAIS SAMIA ANAONGEA KWENYE MAADHIMISHO YA SIKU YA DAWA ZA KULEVYA

KAMISHNA MWAKILEMA ASHIRIKI DORIA YA KUWASAKA SIMBA WALIOZUA TAHARUKI IRINGA

Kamishna wa Uhifadhi TANAPA, William Mwakilema ameungana na timu ya Mkoa wa Iringa kushiriki doria ya kuwasaka wanyama aina ya Simba wanaosemekana wametoka katika maeneo yao ya asili na kuvamia vijiji vilivyoko jirani na Hifadhi ya Taifa Ruaha na kuua mifugo kitu kinachosababisha taharuki katika maeneo wanayozurura.

Nilipata taarifa ya uvamizi wa wanyama hao katika vijiji vilivyoko mbali kabisa na hifadhi zaidi ya kilometa 25 lakini hadi sasa simba hao wameshaenda umbali wa zaidi ya kilometa 70 na wameshavuka barabara ya lami ya kutoka Morogoro, Iringa kwenda Mbeya na wako upande wa pili wa barabara wakiendelea kufanya uharibifu aliongeza Kamishna huyo.

“Baada ya uvamizi wa wanyama hao,timu ya askari 17 kutoka Hifadhi ya Taifa Ruaha na maafisa kutoka Kanda ya Kusini walifika kwa haraka kushirikiana na wenzetu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, TAWA na KDU kuwasaka Simba hao wasilete madhara zaidi” alisema Kamishna Makilema.

Aidha, Kamishna Mwakilema alisema kuwa kutokana na unyeti wa jambo hili tulifanya jitihada za kupata Helikopta na jana wasaidizi wangu wameruka nayo ila kutokana na hali halisi ya milima na makorongo marefu hawakuweza kuwaona. Pia nimeongea na mtu wa AWF pale Manyara Ranch ili kuweza kupata mbwa wa kunusa watusaidie kutambua harufu za Simba hao.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Iringa Veronica Kessy alisema kuwa wilaya imeingiwa na taharuki kubwa baada ya kupata taarifa ya uwepo wa Simba katika Kata ya Magoma na kuua ng’ombe. Kwa haraka niliwasiliana na wenzetu wa TANAPA na TAWA kuja kuwaondoa Simba hao.

Hata hivyo, Simba hao waliendelea kusonga mbele wakiua mifugo na hatimae kufika eneo la Kiponzelya karibia na mji wa Iringa. Hadi kufika tarehe 24.06.2023 Simba hao wameshaua ng’ombe 25, na kujeruhi wawili ambao wanaendelea kupatiwa matibabu, pia wameua mbuzi 5, kondoo 5, nguruwe 3 na kuku1 aliongeza mkuu wa wilaya huyo.

Mkazi wa kijiji cha Tanangozi Grayson Laurent Mtende alisema, “baada ya kupata taarifa za Simba kijijini kwetu tuliogopa kwa sababu Simba hawazoeleki na ni mnyama anayeogopwa hivyo tumesitisha kufanya kazi zetu mashambani kwa muda mpaka pale mamlaka zinazohusika na uhifadhi zitakapotuambia hali ni shwari”.

Simba hao wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 5 bado hawajaonekana na jitihada za kuwasaka zinaendele kwa kutumia magari, helikopta na jitihada za kupata mbwa wa kunusa zinaonyesha kuzaa matunda. Pia wananchi wanaendelea kuelimishwa njia salama za kujilinda na wanyama kwa kutokuwaruhusu watoto na watu wazima kwenda vichakani kuokota kuni, na wanapotoka nje nyakati za usiku watoke na tochi.

DKT. TAX AKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA WA ITALIA JIJINI ROMA

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) amekutana na kuzungumza na Naibu Waziri Mkuu wa Italia na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Antonio Tajani ofisini kwake jijini Rome nchini Italia..

 

Akizungumza na mwenyeji wake Mhe. Dkt. Tax ameelezea kuridhishwa na uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Italia na kuishukuru Serikali ya Italia kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Tanzania katika kuiletea maendeleo kupitia elimu, afya, kilimo, mabadiliko ya hali ya hewa na uchumi wa buluu.

 

Mhe. Dkt. Tax ameihakikishia Italia kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana nayo na kuhakikisha uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Italia unakuwa na kufikia ngazi ya juu.



Dkt. Tax amependekeza kuanzishwa kwa mfumo wa majadiliano ya kisiasa na kidiplomasia kati ya Tanzania na Italia ambao utatumika kama jukwaa la kuimarisha ushirikiano uliopo kati ya nchi mbili kwa maslahi mapana ya pande zote.

 

“Nafahamu kuwa nchi zetu hazina mfumo wa majadiliano wa kisiasa na kidiplomasia licha ya kuwa na uhusiano mzuri wa siku nyingi, napendekeza tuanzishe mfumo wa majadiliano ya kisiasa na kidiplomasia kati ya nchi zetu, mfumo huu utatumika kama jukwaa la kuimarisha zaidi ushirikiano uliopo kati ya nchi zetu kwa maslahi ya pande zote,” alisema Dkt. Tax.

Habari kamili na Ally Thabith

MOFTI AELEZEA MIAKA MINANE NDANI YA BAKWATA

Mufti mkuu wa Tanzania (BAKWATA) ABUBAKARI BIN ZUBERI amesema ndani ya miaka nane anajivunia kuimalisha taasisi za kidini kuanzisha shule na vyuo vya kiislam kuongonisha waislam pamoja nawasio kuwa waislam na ujenzi wa msikiti wa kimataifa pamoja na ofisi za BAKWATA.


Habari kamili na Ally Thabit