Tuesday, 16 November 2021

TIRA YAWEKA MIKAKATI MIZITO


 Kaimu Meneja wa Utekelezaji wa Sheria Kutoka TIRA amesema TIRA imeweka mikakati mikubwa Lengo kuinua na kukuza sekta ya Bima  nchini  tanzania amesema haya kwenye viwanja vya mnazi mmoja jijini Dsm.

Habari picha na Ally Thabiti

Monday, 15 November 2021

BOT YATOA TILIONI MOJA KWENYE MABANK


 Mmoja wa Afisa wa BOT amesema Katika Kutekeleza maagizo na maelekezo ya raisi Samia Suluhu Hassan Juu ya mabank kupunguza riba ya mikopo kwenye  mabank BOT imezikopesha Bank nchini Tanzania kiasi cha tilioni moja Lengo zitoe mikopo ya riba nafuu.

Ambako bank zimeanza kushuaha viwango vya riba ambako apo mwanzo Bank zilikuwa zinatoa asilimia 28 na wataasisi zinazotoa mikopo zimeanza kutoa mikopo asilimia 3.5 Kwa mwezi ukilinganisha na kipindi cha nyuma .

Nae Afisa Mwandamizi wa BOT Crispina Nkwa amewataka watu kutozialibu Kwa kuzikanyaga pesa au kuzifanyia Jambo lolote kinyume na Taratibu za nchi kwani hatua Kali dhidi Yao zitachukuliwa kutokana na sheria ya mwaka 206 ya Tanzania BOT Ndio yenye mamlaka ya kuziaribu pesa amesema haya viwanja vya mnazi mmoja jijini Dsm.

Habari picha na Ally Thabiti

MARGARET MNGUMI ATOA NENO KWA TASISI ZA BIMA


Margaret Mngumi Msajili wa Malalamiko Ofisi ya Msuluhishi wa Migogoro ya Bima ,,amesema Kwa mwaka huu wametatuwa Migogoro ya Bima 150 Sawa na mwaka Jana .

Amewataka Wananachi wakiwa na Malalamiko ya Bima waende kwenye Ofisi zao zilizopo Mbeya,Mwanza,Dodoma ,Dsm na Mikoa mingineyo.

Kwamawasiliano zaidi +2552221111117 Nukushi +25522211094 Kwa barua Pepe Ombudsman@tio.go.tz Tovuti Www.tio.og.tz.

Habari picha na Ally Thabiti

 

KUNDI LA KUPINGA NDOA ZA UTOTONI LAWEKA MIKAKATI TGNP MTANDAO


 Kama anavyoonekana Pichani Kiongozi wa Kundi la kupinga Ndoa za utotoni Kerven akieleza mikakati yao ya kwenda kutoa elimu Kwa Jamii,Viongozi wa Kidini na Wadau wengine.

Kerven ameipongeza na kuishukuru TGNP MTANDAO Kwa juhudi na jitihada wanazozifanya na kuzichukuwa za kupinga na kupiga Vita Aina zote za ukatili WA kijinsia, mfano Ndoa za utotoni.

Habari picha na Ally Thabiti

FORUM CC YATOA NENO KWA WANAHARAKATI WA TGNP MTANDAO


 Msololo Onditi Program Officer wa FORUM CC amewataka Wanaharakati wote Kuwajenga uwezo watu WA namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi, Kwa Lengo la kunusulu vizazi vya sasa na vijavyo.

FORUM CC inaipongeza TGNP MTANDAO Kwa juhudi na jitihada wanazofanya Kwa jamii Kwa kuwapa elimu ya utunzaji wa Mazingira. 

 FORUM CC imetoa Rai Kwa serikali washirikiane na Wanaharakati ili waweze kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi . Kwa kuwapa rasilimali watu,Fedha na kuweka mazingira rafiki na wezeshi Kwa wadau wote Kwa maslai mapana Kwa tanzania .

Habari picha na Ally Thabiti

JOYCE WA TGNP MTANDAO AKITANA NA WANAHARAKATI


 Joyce Kutoka TGNP MTANDAO Amewataka Wanaharakati kuweka nguvu za pamoja ili kutokomeza Mimba za utotoni,Ndoa za utotoni na Utoaji wa mimba Kwa watoto wa kike  na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Pia Joyce wa TGNP MTANDAO ameitaka serikali ya Tanzania kutekeleza makubaliano waliyosaini SADC mwaka 2008 namna ya kutokomeza na kupinga maswala ya ukatili wa kijinsia .

Kwani katika makubaliano hayo tanzania imekuwa nchi ya mwisho katika utekelezaji.

Habari picha  na Ally Thabiti

MWANA HARAKATI JENIFA AHAIDI MAZITO


 Jenifa ni Mwanaharakati amesema Mafunzo aliyoyapata TGNP yamemjengea uwezo mkubwa wa namna ya kuweza kutokomeza mimba za utotoni na maswala ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.  

Na mambo yote yanayousu ukatili wa kijinsia yeye atakuwa balozi mzuri,ametoa wito Kwa jamii kuungana na TGNP MTANDAO katika kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Habari picha na Ally Thabiti