Sunday, 15 October 2023

 Naibu waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel leo ametembelea Taasisi ya Saratani Ocean Road na kuzungumza na baadhi ya watumishi, huku akiupongeza uongozi wa Taasisi hiyo kwa kusimamia vizuri pesa zinazotolewa na serikali kwaajili ya miradi mbalimbali.

Dkt. Mollel amesisitiza kuwa ujenzi wa jengo mfano la Cyclotron ukiliangalia kwa nje unaweza Sema limegharimu kiasi kidogo sana cha pesa ila kwa ndani ndio utagundua thamani ya pesa iliyotumika kuwa inaendana na ubora na umadhubuti wa jengo lenyewe.

Dkt. Mollel ameomba uharaka wa umaliziaji wa jengo hilo ufanyike kwani watanzania wanahitaji huduma zake mapema iwezekanavyo huku serikali ikitaka uwekezaji wake uanze kuleta tija kwa wananchi.

Nae mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt Julius Mwaiselage, amemhakikishia Dkt. Mollel kumalizika mapema kwa ujenzi huo kwani kwa upande wa jengo limekamilika kwa Asilimia tisini na nane wakati mashine tayari zimekwishasimikwa kwa asilimia Mia moja huku ukisubiriwa utaratibu wa kuunganisha umeme pekee ili mashine hizo zianze kutumika kama inavyotakiwa.

Jengo hilo limekusanya mashine mbili kubwa ambazo ni PET-CT SCAN pamoja na CYCLOTRON (kiwanda cha kutengeneza mionzi) ambapo kwa sasa kwa Tanzania nzima kitakuwa ni kimoja tu, ambacho kitakuwa kikitengeneza mionzi ambayo itatumika kwa Taasisi huku mingine ikipelekwa kwenye hospitali nyingine kwaajili ya kusaidia wahanga wa huko. Kwa sasa Taasisi inanunua mionzi hiyo kutoka Afrika ya Kusini huku gharama zake zikiwa kubwa mno ukilinganisha na uwezo wa watanzania wenyewe, hivyo kukamilika kwa usimikaji huo kutakuwa msaada mkubwa sana kwa Tanzania na Afrika mashariki na kati kwa ujumla.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka wananchi kufanya uchunguzi wa awali wa kupima Saratani ya Matiti ili kujua hali zao na kupata matibabu mapema kwa wenye changamoto hiyo

Waziri Ummy ameyasema hayo Octoba Mosi, 2023 wakati akimuwakilisha Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kwenye Maadhimisho ya Mwezi wa Saratani ya Matiti yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi ya Saratani Ocean Road Jijini Dar es Salaam.

Waziri Ummy amesema Tanzania inakadiriwa kuwa na wagonjwa wapya wa Saratani takribani Elfu Arobaini na Mbili (42,000) kila Mwaka ndio wanafika katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

Pia, Waziri Ummy amesema taarifa ya mwaka 2022/2023, inaonesha kuwa Taasisi ya Saratani Ocean Road ilihudumia wagonjwa wapya takriban 8,779 na asilimia 13 ya wagonjwa hao sawa na wagonjwa 1,141 walikuwa na Saratani ya Matiti.

Sambamba na hayo, Waziri Ummy amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara ya Afya kufunga mashine za CT-Scan katika Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na mashine za Ultrasound katika Hospitali zote za Halmashauri nchini.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha matibabu kwa kutuletea vifaa tiba vya kutosha kwaajili ya uchunguzi wa Saratani mbalimbali ikiwamo PET-CT huku maahine ya Cyclotron ikiwepo kwaajili ya kuzalisha mionzi tiba itakayo tumika hapa kwenye Taasisi huku bakaa ikipangwa kupelekwa kwenye maeneo mengine kwaajili ya kusaidia watanzania wengine.

Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka ifikapo mwezi wa kumia mabapo watu duniani kote huungana kupingana na ushambulizi wa aina yoyote wa Saratani hii huku ikiwasaidia wananchi waliokwisha athirika na ugonjwa huo kupata matibabu

Friday, 28 July 2023

STELLA REZAULA AELEZEA IMOPHIRIA



Raisi wa imophiria nchini Tanzania Stella Rezaula amesema kati ya watu elfu kumi moja mmoja ana imophiria amesema pia mpaka sasa hospitali saba zinatoa huduma za imophiria tena bure kuanzia vipimo mpaka matibabu ambapo ni hospital ya rufaa ya mbeya KCMC hospitali ya benjamini mkapa Dodoma, Muhimbili, Kigoma mawenzi na zinginezo.

Stella Rezaula amesema asilimia ya 70% ya imophiria ni wakurithi pia amesema kuna utofauti wa kati imophiria na selimundu ametoa wito kwa serikali waendelee kusaidia matibabu ya ugonjwa huu pia ameitaka jamii kujitokeza kwa wingi kupima imophiria.

habari picha na Ally Thabiti

TANESCO YAWAKIKISHIA WATEJA WAO UMEME WA UHAKIKA





Naibu mkurugenzi wa uzalishaji umeme TANESCO mwandisi Pakaya amesema shirika la umeme nchini Tanzania (TANESCO) linafanya kazi kubwa ya kuzalisha umeme wa kutosha kwa wateja wao ambapo asilimia 35% umeme unazalishwa na maji na asimilia 65% umeme unazalishwa na gesi hivyo amesema bwawa la mwalimu nyerere likikamilika uzalishaji wa umeme utakuwa mkubwa sana naye kwa upande wake mkurugenzi wa huduma EXPERIENCE Bw. Martin Mwambene Amesema Tanesco sasa hivi inatatua changamoto za watu kwa haraka zaidi kwa kutumia namba za simu lakini pia imesambaza watendaji kazi wao wa pikipiki, Bajaji kwa maeneo ambayo magari hayafiki amesema haya Serena Hotel wakati wakiwa na wahariri wa vyombo vya habari na waandishi wa habari huku mwenyekiti wa baraza la wahariri ndugu Barire amelipongeza shiurika la Tanesco kwa ufanisi wao mzuri pia kwakuweza kutekeleza miradi yao kwa wakati.

Habari picha na Ally Thabith

TANESCO YAZINDUA MPANGO WA JINSIA (GENDER WORK PROGRAM) WA MIAKA MINNE

 Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kupitia mradi wa kusafirisha umeme mkubwa kutoka Tanzania hadi Zambia (TAZA).

 

Progamu hii imezinduliwa na Mgeni Rasmi na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato ukiwa na lengo la kutatua changamoto wanazokutana nazo wafanyakazi wanawake katika maeneo yao ya kazi na kuongeza uwiano wa utendaji kazi baina ya wanawake na wanaume kati ya mwaka 2023 hadi 2026.

 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo, Mhe. Byabato alisema TANESCO imejizatiti kwa kiasi kikubwa kwenye usawa wa kijinsia na kuitaka menejimenti ya Shirika hilo kuhakikisha inaanzisha kitengo maalumu cha jinsia ili kuwepo na uwanja mpana wa kujadili masuala ya kijinsia.

 

“Naiagiza menejimenti ya TANESCO kupitia mradi wa TAZA kuhakikisha wanawake wanapewa kipaumbele sawa na wanaume na kuongeza fursa zaidi kwa wanafunzi wa vyuo ambao wanajiandaa kuajiriwa kwenye ajira rasmi”.

 

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Maharage Chande alisema, “Sisi kama TANESCO swala la kijinsia lipo juu kabisa katika agenda zetu. Wakati tunaanda mkakati wa Shirika, tuliainisha vipaumbele saba na katika kipaumbele cha kwanza kilikuwa ni kipaumbele cha watu na tuliweka masuala ya usawa wa kijinsia na hususani tuliweka mikakati ya kuhakikisha tunaongeza  viongozi wanawake katika Shirika letu”.

 

Ameyataja maeneo ya kipaumbele kuwa ni pamoja na sera ya Shirika kutoa kipaumbele kwenye masuala ya jinsia, upatikanaji wa taarifa sahihi za masuala ya jinsia kwenye taasisi na kuwepo kwa nafasi za mafunzo ya ukuzaji taaluma kwa wafanyakazi wanawake hasa wanaofanya kazi za kiufundi ili kuwajengea uwezo kupitia mpango wa mafunzo kazini.

 

Akifunga uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Fedha wa TANESCO, CPA Renata Ndege alisema nafasi za wanawake kwenye Shirika zipo nyingi isipokuwa wengi wao wanakosa ujasiri wa kupambanania nafasi husika na wanafanyakazi wanaume.

 

Aidha, amepongeza hatua ya uanzishwaji wa kitengo maalum cha kushughulikia mambo ya jinsia kwani kitendo hiki kitaongeza kasi kwa wafanyakazi wanawake kuwepo kwenye nafasi mbalimbali za uongozi.

 

Mradi wa upanuzi wa njia ya kusafirisha umeme mkubwa wa kilovoti 400 kutoka kituo cha kupokea, kupoza na kusairisha umeme cha Tagamenda Iringa nchini Tanzania kwenda Zambia (TAZA) na nchi nyingine zilizopo Kusini mwa Tanzania kupitia Kisada Iringa, Iganjo Mbeya na Nkangamo Tunduma Songwe unatekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupitia mkopo wa Jumuiya ya  Maendeleo ya Kimataifa (IDA) ya Benki ya Dunia, mkopo wa Mfuko wa Maendeleo wa Ufaransa (AfD), Umoja wa Nchi za Ulaya (EU) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


habari kamili na Ally Thabith

Wednesday, 19 July 2023

WAZIRI WA MADINI AKUTANA NA CHEMBA YA MADINI

Waziri Dr Doto Biteko amesema lengo lakukutana na chema ya madini ili kutatuwa kero zinazo wakabiri wanachama wa chema hii ya madini, kero hizo ni wingi wa kodi, tozo, mwingiliano wa Sheria mfano mizara ya Mali asiri na utalii ambapo wanazuia uchimbaji wa madini kwenye hifadhi na mbuga  hata hivyo Dr Doto Biteko amempongeza na kumshukuru mwenyekiti wa chema ya madini pamoja na wajumbe wake kwa namana wanavyotoa ushirikiano kwenye serikali yao mpaka kupelekea secta hii kukua kwa kiwango kikubwa na kuongezeka kwa mapato.Waziri Dr Doto Biteko ametoa wito kwa jamii na kwa wachimba madini  kulinda na kuhifadhi Maliasiri za Tanzania. pia amewatoa hofu chemba ya wachimba madini kuwa sheria zenye mwingiliano zitafanyiwa kazi.Naye kwa upande wake mwenyekiti wa chemba ya wachimba madini amempongeza serikali na kuishukuru  kwa kutatua kero za wachimba madini kwa kazi kubwa. 


Habari picha na Ally Thabiti. 

Sunday, 16 July 2023

BILL NAS KUPAGAWISHA SIKU YA MWANANCHI

 




Msanii wa kizazi kipya Bilnasi amesema tarehe 22/07/2023 atafanya show ya kibabe katika uwanja wa benjamini mkapa ambako TIMU ya YANGA itacheza na Kaizer Chiefs hivyo amewataka watu wajitokeze kwa wingi.

Habari picha na Ally Thabit