Wednesday, 7 August 2024

KAIMU MKURUGENZI MKUU WA DAWASA ABAINISHA MIKAKATI KABAMBE


 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dawasa Mkama Bwile amesema moja ya mipango mikakati yao ni kudhibiti uvujqji wa maji kutoka asilimia 40% mpaka ifike asilimia 30% ingawaje inatakiwa upoteaji wa maji iwe asilimia 20%.

Mkama Bwile amesma dawasa inadai kiasi cha fedha bilioni 40 kutoka kwenye taasisi mbalimbali na watu binausi ivyo kwa kushirikiana na viongozi wenzake wanampango wa kukusanya kiasi kikubwa cha madeni haya ili dawasa iweze kujitegemea na kutatuwa changamoto zilizopo ndani ya dawasa.

Mkama Bwile ameongeza kwa kusema dawasa itafunga dira za maji pamoja na mita za kisasa amewaakikishia waariri wa vyombo vya habari na wanahabari dawasa itakuza na kuhimarisha ushirikiano kati yao ,kwani dawasa inaamini kuwa wanahabari pamoja na waariri wa vyombo vya habari ni daraja kubwa na kiungo muhimu kati ya dawasa na wananchi katika kufikisha taarifa kwa wananchi wote.

Amesema haya kwenye semina kati ya dawasa pamoja na wanahabari na waariri wa vyombo vya habari semina hii imefanyika jijini dar es salaam  ukumbi wa mwalimu nyerere.

Habari picha na Ally Thabit 

WANAHABARI WAWAPONGEZA DAWASA


 Mwanahabari Mkongwe wa Tbc Anuali Mkama amesema kitendo cha Dawasa kukutana na wanahabari pamoja na waariri wa habari ni muhimu kwani itasaidia kwa kiasi kikubwa katika kutatua changamoto za ujujaji wa maji ambako zaidi ya asilimia 40% maji ya dawasa yanapotea kwa kuvuja .

Hivyo kupitia wanahabari na waariri wa vyombo vya  habari watatumia vyombo vyao vya habari katika kuelimisha jamii  kutoa taarifa ya uvujaji wa maji ya dawasa na changamoto zingine zinazowakabili wateja wa dawasa.

Mwanahabari Anuali Mkama amesema semina hii imekuwa kiunganishi kati ya dawasa ,waariri wa vyombo vya habari na wanahabari amesema haya kwenye semina kati ya dawasa ,waariri wa vyombo vya habari na wanahabari jijini dar es salaam  ukumbi wa mwalimu nyerere.

Habari picha na Ally Thabit 

Tuesday, 6 August 2024

RAISI WA WAKANDARASI WANAWAKE WAIPONGEZA BANKI YA NMB


 Raisi wa Wakandarasi  Wannawake Mwandisi Judith Odongo amesema Nmb kuwaongezea kiwango cha fedha imewasaidia katika swala la mtaji kwani wataweza kufanya miradi mikubwa nchini tanzania .

Raisi wa wakandarasi wazawa mwandisi Judith Odongo amesema faida wanazozipata kuongezeka kwa uchumi kwa mtu mmojammoja na nchi kwa jumla 'kuongezeka kwa kodi,kukuwa kwa ajira ambako vijana wengi watapata ajira ya vibaruwa au za kudumu.

Judith Odongo amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kuwa wakandarasi ambako kwa sasa wanawake 350 ni wakandarasi na wenye ulemavu wawili 2akiwemo mwandisi mkongwe mama Esta amesema haya wakandarasi wakiwa na nmb banki  jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 

NMB YAWATAKA WAKANDARASI WAZAWA KUCHANGAMKIA FURSA

Kiongozi wa Benki ya Nmb amesema lengo lao kuwakuza wakandarasi wa tanzania ili waweze kufanya miradi mikubwa ambako itawezesha kukuwa kwa ajira tanzania ,kukuwa kwa uchumi na kuwezesha pesa ya tanzania kubakia hapa nchini .

Nmb benki imeongeza kiwango cha mkopo kwa wakandarasi wazawa kutoka bilioni mbili nukta tano 2.5 mpaka bilioni tatu na kuweka kiwango kidogo cha riba  .amesisitiza kuwa nmb benki itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi kwa wakandarasi wa kitanzania amesema haya nmb benki walipokutana na wakandarasi wazawa.

Habari picha na Ally Thabit  

NAIBU WAZIRI WA UJENZI AMEWAPONGEZA NMB BENKI


 Naibu Waziri wa Ujenzi Mwandisi Godfrey Kasekenya aipongeza Banki  ya NMB kwa kuwapa fursa Wakandarasi wa ndani kwa kuwaongezea kiwango cha fedha ambako akina riba kubwa  hii itawawezesha na kusaidia wakandarasi wazawa kufanya miradi mikubwa na kukamilisha kwa wakati .

Ambako mwanzo wakandarasi wazawa walikuwa wanakabiliwa na changamoto ya mitaji,Naibu Waziri wa Ujenzi amesema raisi dkt Samia kafanya maboresho ya sheria kwa wakandarasi wazawa kufanya miradi ya bilioni hamsini 50 ambako hapo mwanzo walikuwa wakifanya miradi ya bilioni kumi 10

Amesema haya jijini dar es salaam  kwenye mkutano wa wakandarasi na benki ya nmb.

Habari picha na Ally Thabit 

SHULE YA ST.MARKS INATOA ELIMU YA VIWANGO VYA JUU

 Mwenyekiti wa Ccm Wilaya ya Mkuranga Juma Saidi Maghahira anawata wazazi na walezi wawapeleke watoto wao kwe ye shule ya St. Marks kwani elimu wanayotoa inaubora na viwango vya kimataifa  pia inazingatia elimu bora ,maadili, Ulinzi na usalama amesema haya kwenye mahafari ya tatu kwa wanafunzi wa Awali na mahafari ya pili kwa darasa la saba shule ya St Marks. 

Habari na Ally Thabit. 

Monday, 5 August 2024

ASKOFU FROLIANI KATINZI AWAPA NENO WAZAZI


 Askofu Froliani Katunzi Mwenyekiti wa Bodi wa Shule za St Marks,St Methinks,Ujenzi,Victoria na Magnet anawataka wazazi na walezi watanzania na wasio watanzania wawapeleke watoto wao kwenye shule hizi  kwani bei ni nafuu ,ulinzi na usalama unazingatiwa kwa kiasi kikubwa kwa watoto .

Mabweni kwaajili ya kulala watoto yapo ya kutosha, katika elimu inayotolewa kwenye shule hizi ni kiwango cha kimataifa ambako mtoto akiitimu anauwezo wa kujiali na kuajiliwa .Askofu Katunzi amesema shule zao zina miundombinu rafiki na wezeshi kwaajili ya wanafunzi wenye ulemavu  pia ina wataalam wa rugha za alama kwa wenye uziwi na uono afifu.

Mwenyekiti wa bodi Askofu Katunzi amesema katika kumuunga mkono rais dkt Samia elimu wanazozitoa kwenye shule zao kuanzia elimu ya Awali,Msingi na Secondary wanamafunzo ya vitendo na wana kompyuta zipatazo Mia nne kwaajili ya kufundishia wanafunzi kwa njia ya kidigitali .

Swala la Elimu Bora ,Maadili ,Malezi na Usalama na Ulinzi kwa Watoto pamoja na nidhamu katika shule zao ndio falsafa yao kwa siku zote.ametoa wito kwa nawafunzi watakao maliza darasa la ssaba wawe na nidhamu njema pindi watakapoenda makwao na amewataka wazazi na walezi ifikapo tarehe 19/9/2024 wawalete kwenye shule hizi ili wapate kusoma preform one wapate elimu bora kwa gharama nafuu.

Amesema haya kwenye mahafari ya tatu kwa wanafunzi wa elimu ya awali shule ya St Marks na mahafari ya pili kwa darasa la saba shule ya St Marks wilayani mkuranga mkoa pwani eneo la mwandege.

Habari picha na Victoria Stanslaus.