Friday, 7 February 2025

MASHUJAA WA SARATANI PAMOJA NA WADAU WANAOPIGA VITA SARATANI ZA AINA ZOTE WAPO KWENYE MATEMBEZI

 
Kama Inavyo Onekana Pichani  hawa ni Wadau wanaopiga vita ugonjwa wa saratani wapo katika matembezi Lengo la matembezi haya kuhiasa jamii kujitokeza kufanya uchunguzi kwenye miili yao kama wana magonjwa ya saratani au dalili ili waanze tiba mapema kwani saratani inatibika ukiiwai .


Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

FAITH GUGU MKUU WA GSM FOUNDATION AAHIDI MAKUBWA KWENYE HOSPITALI YA OCEANROAD CENCER INSTITUTE

 Mkurugenzi Mkuu wa GSM FOUNDATION Faith Gugu amesema wataendelea kushirikiana na hospital ya Ocean road Cancer Institute katika mapambano ya saratani za aina zote lengo kutokomeza au kupunguza uogonjwa wa saratani na vifo vinavyotokana na saratani za aina zote kwani GSM FOUNDATION inatoa elimu kwa jamii ya kujilinda dhidi ya magonjwa ya saratani. Elimu hii inawafikia watu wenye ulemavu wa aina zote.

Amesema haya kwenye kilele cha maazimisho ya saratani yalio fanyika kwenye Hospitali ya Ocean road cancer Institute ambako uazimishwa kila tarehe 4 ya mwezi wa 2 duniani kote kila mwaka . 

Habari na Ally Thabit 

GLORIA KIDA MKURUGENZI WA ASASI YA SHUJAA WA SARATANI AIMIZA WATU KUPIMA SARATANI

 Mkurugenzi  wa Asasi ya Shujaa wa Saratani Gloria Kida anawataka watu kujitokeza kwa wingi  kupima saratani za aina zote Pia anawahimiza wanajamii kuchanja chanjo ya HPV wao na watoto wao kwani  ni kinga dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi .

Asasi yao Imetoa Elimu ya Saratani Katika  Mkoa wa Mwanza na Wilaya zote za Dar es salaam  amesema haya kwenye kilele cha week ya saratani iliyo fanyika kwenye Hospitali ya Oceanroad   Cancer Institute ambako kila mwaka uazimishwa tarehe 4 ya mwezi 2 duniani kote .

Habari  na Ally Thabit. 

ASCP MULIRO J. AELEZEA WATOTO WALIOJITEKA

 Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam  Limewapata na Kuwahoji wasichana wawili ambao ambapo mmoja wa miaka16  Mwanafunzi wa kidato cha pili na mwingine  wa miaka 12 Mwanafunzi wa Darasa la saba  wakazi wa vijibweni kigamboni kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo baada ya kutengeneza mazingira kuwa wametekwa  na watekwaji wanataka pesa.

Ufuatiliaji ulifanywa na kufanikiwa kubainiwatoto hawa walipokuwa na baada ya mahojiano ya kina  walikiri kutengeneza tukio hili la uongo ili waweze kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu toka kwa wazazi wao baada ya kutoweka  tarehe 26/01/2025 na kuelekea  Longoni Beach ambapo walikesha hapo hadi tarehe 27/01/2025 asubuhi na  baadae kuelekea maeneo ya Tungi hadi walipo kamatwa  wakiwa wanazunguka. Jeshi linalaani vitendo vya hivi vya watu wenye lengo la kujipatia  pesa kwa njia za udanganyifu.

Aidha, Jeshi la Polisi Kanda ya  Maalum Dar es salaam  katika kipindi cha Desemba hadi Januari 2025 katika kusimamia mifumo ya haki jinai mahakamani baadhi ya watuhumiwa mbalimbali walipatikana na hatia  ikiwa ni pamoja na Idrisa  Rasshid miaka [35]  Mkazi wa Kwembe  Kimara alihukumiwa  miaka 30 jela kwa kosa la kubaka kwenye Mahakama ya Wilaya ya  Kinondoni.  Paul Elisha miaka (37) mkazi wa Mbezi  Beach kwe nye Mahakama ya Kinondoni alihukumiwa kifungo cha maisha  jela kwa kosa la kubaka na Jackson Mgeta (34) mkazi wa Kawe alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kubaka.

Jeshi la Polisi lina wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana ili kuimarisha mifumo ya ulinzi shirikishi ikiwa ni pamoja na kutekeleza falsafa ya ulinzi shirikishi ili kuzuia  vitendo vya kihalifu. Imetolewa na Kamanda  Kanda Maalum ya Polisi Dar es salaam. 

Habari na Ally Thabit Mbungo. 


Monday, 25 November 2024

NMB BANK NA TAASISI YA TSA WASHILIKIANA KUWAFUNZA WAJISIRIAMALI

 


KWAME mkuu wa Idara ya TEHAMA na UBUNIFU Bank ya NMB amesema wameingia makubaliano na TSA lengo kuwakuza na kuwatafutia masoko wajasilimali wa nchini Tanzania kwani wajasiriamali wengin wanashindwa kuuza kimataifa bidhaa zao kwa kukosa elimu ya namna ya kutumia Tehama kwa ajili ya kutafuta masoko ndani ya nchi na nje ya nchi, KWAME amesema makubaliano waliongia na taasisis ya TSA itasaidia kusimamia ubunifu mbalimbali kwa muda wa mika mitatu.

Kwaupande wake mtndaji mkuu wa Taasisi ya TSA ZAHORO PAULO  MAKANGA amesema wameamua kuingia makubaliano na Bank ya NMB kwa ajili ya kuboresha na kukuza mifumo ya wabunifu na wajasilia mali kwani wajasiriamali watatengenezewa mazingira lafiki ya kuu na kutangaza bidhaa zao, 

Taasii ya TSA na Bank ya NMB watawapa wajasiriamali na wabunifu elimu ya utunzaji fedha na usimamizi wa mitaji yao ya biashara TSA na NMB bank wataandaa program mbalimbali kwa wajasiriamali na wabunifu namna ya kukuza na kuimalisha biashara na uchumi wao, 

ZAHORO PAULO  amesema pia kutakuwa na mashindano kwani  kutaleta chachu kwa wajasiriamali na wabunifu katika matumizi ya mtandao huku akiipongeza serikali kwa kuandaa sera ambayo itasaidia kukuza na kulasimisha wajasiriamali na wabunifu, Nchi zingine zinapata kiasi kikubwa cha fedha. amesema haya makao makuu ya NMB wakatika wakiingia makubaliano na Bank hiyo.


Habari Picha na Ally Thabiti.

CHADEMA WAISUTA SERIKALI

Mwenyekiti wa chama cha CHAEMA Mbowe na katibu mkuu John Mnyika wamekanusha na kukana waziwazi kuwa awajawahi kukubaliana na serikali juu ya TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa serikali za mitaa, Vitongoji na Vijiji na badala yake walitaka tume huruma ya uchaguzi ndiyo isimamie.

Habari na Ally Thabiti

MKUU WA CHUO KIKUU HURIA HAMIZA NDOTO ZA MWALIMU NYERERE KUKAMILIKA

Waziri Mkuu Mstaafu mizengo pinda na mkuu wa chuo huria amesema katika kuhazimisha miaka 30 ya chuo kikuu huria waweza kukamilisha na kufanikisha ndoto za mwalimu Nyerere kwa kutoa elimu yenye ujuzi. 

Habari na Ally Thabiti