Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya BI Aisha Sururu amesema wataendelea kuwawahifadhisha Quran vijana wote wa kitanzania na wasio watanzania lengo wamtambue mungu na wawe wenye maadili mama.
Tuesday, 11 March 2025
TAASISI YA BI AISHA SURURU YAAHIDI MAKUBWA KWA VIJANA
Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya BI Aisha Sururu amesema wataendelea kuwawahifadhisha Quran vijana wote wa kitanzania na wasio watanzania lengo wamtambue mungu na wawe wenye maadili mama.
Monday, 10 March 2025
AMANA BENK YAAIDI MAZITO
Mkurugenzi wa Amana Benk Abubakari amesema watazidi kudhamini na kufadhiri mashindano ya Quran lengo kuwatia moyo wanaohifadhi na kusoma Quran na kukikuza kitabu cha mungu amesema haya kwenye mashindano ya 25 ya kuifadhi Quran yalioandaliwa na taasisi ya Bi Aisha Sururu foundation ambayo yamefany8ka jijini dar es salaam.
Habari picha na Victoria Stanslaus
BI ASHA DIWANI VITI MAALUM JIJI LA ILALA AIMIZA WAZAZI NA WALEZI KUWAPELEKA WATOTO WAO KUSOMA QURAN
Diwani wa Viti Maalum na Mweka hazina kwenye taasisi ya Aisha Sururu Foundation anawataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kusoma Quran kwani kuna faida zinapatikana zikiwemo kuwa na imani,kuulumia binadamu mwenzako,kuwana ofu na kuwa mwadilifu na weredi katika kazi na jamii kwa ujumla .
Habari picha na Victoria Stanslaus
MJUMBE WA ALMASHAURI KUU YA CCM APONGEZA MASHINDANO YA QURAN
Amoll Abudi Juma Mjumbe wa Almashauri Kuu ya ccm taifa mkoa wa dar es salaam amempongeza bi Aisha Sururu kwa kuendesha mashindano ya quran kwa miaka ishilini na tano pamoja na kuwahifazisha maneno ya mungu watoto yatima,wajane,wasiojiweza,watu wa makundi maalum kwani kufanya hivi kunasaidia kupata watu wenye maadili,wenye ofu ya mungu na hatimae nchi ya tanzania inapata amani ,upendo na utulivu.
SHEIKH PONDA AELEZA UMUHIMU WA FUNGA
Sheikh Issa Ponda amewataka Waislamu wote wale ambao awana matatizo ya kiafya waweze kutekeleza nguzo ya nne ya kiislam kati ya tano wafunge ramadhani ndani ya mwezi huu wa ramadhani kwani watakuwa waja wema pia wasome Quran mara kwa mara.
Habari na Victoria StanslausSHEIKH CHIZENGA AELEZA FAIDA ZA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI
Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Ulamaa Bakwata amewataka waislamu nchini tanzania wafunge ramadhani kwenye mwezi huu mtukufu wa ramadhani kwani miongoni mwa faida watakazozipata ni kuimarika kwa afya zao .Pia mungu atawasamehe makosa yao na zambi zao pia anawasisitiza watanzania wote bila jujali dini,kabila,rangi na jinsia wazidi kumuombea afya njema rais Dr Samia kwani amekalisha miradi yote na anatenda haki kwa kila mmoja hivyo ni vyema kumchagua kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu hakika mama samia mitano tena.
Habari picha na Ally Thabit.





