Monday, 10 March 2025

KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI AWATOA OFU WATANZANIA















Eng. Felchesmi J.Mramba  Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati amewatoa ofu watanzania  kuhusu uhamuzi uliofanywa na serikali yetu ya tanzania kwa kununua umeme megawati mia moja kutika nchi ya Ethiopia .

Kwani Umeme huu unanunuliwa kwa gharama ndogo  kwani umeme utasaidia mikoa ya kaskazini kupata umeme wa uhakika  kwenye viwanda na  maeneo wanayoishi wananchi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Eng Felchesmi J. Mramba amesema tanzania itapata umeme huu kupitia kutoka Ethiopia kwa kutumia miundombinu ya Kenya kwani Kenya na Ethiopia zipo karibu . Serikali ya tanzania imefanya uhamuzi huu kwa sababu tunapoteza megawati kumi na saba za umeme kwa kutumia kupitisha umeme kwa njia za ndani ya nchi yetu Pia sera zetu zinaruhusu kununua umeme nchi za nje .

Mfano Mkoa wa Rukwa umeme unaotumika ni kutoka nchi ya Zambia ,Umeme unaotumika  mkoa wa Kagera unatoka nchi ya Uganda hata nchi ya Ethiopia amnayo inatuuzia tanzania  umeme licha ina megawati elfu sita lakini bado inanunua umeme nchi zinginezo na mpaka sasa nchi zipatazo tatu zimeleta maombi za kuuziwa umeme na tanzania  na wamekubaliana na wapo hatua za mwisho nchi hizi ni Burundi,Rwanda na Zambia .

Na sasa Tanzania kwa Kushirikiana na Zambia wanatekeleza mradi wa Taza ambao megawati sita za umeme zitauzwa nchini Zambia na mradi umefikia asilimia hamsini .Nakampu  ya Mifodi ya Zambia itanunua megawati mia moja tanzania  nchi zinginezo  zitazonunu umeme tanzania Msumbiji,Marawi,Dr kongo

Katibu Mkuu amesisitiza kuwa bei tunayouziwa umeme na nchi ya Ethiopia  ni bei na fuu na rafiki kwani ni dora saba nukta saba sent .

Swala la Bwawa la Mwalimu Nyerere limeleta ukombozi katika kupatikana umeme wa kutosha nchini tanzania hivyo watanzania tuunge mkono uwamuzi uliofanywa na serikali yetu ya tanzania na tuendelee kumpongeza rais Dr Samia kwa kukamilisha bwawa la mwalimu nyerere na miradi mingineyo mpaka kuwezesha nchi kuondokana na tatizo la kukatikakatika umeme mara kwa mara.

Habari picha na Victoria Stanslaus 

No comments:

Post a Comment