Tuesday, 17 June 2025

MWENYEKITI WA CHAMA CHA CHAUMA AZIDIWA MAUTUTI

 Ashim Rungwe  Mwenyekiti wa Chama cha Chauma Maarufu Mzee wa Ubwabwa yupo  Maututi Mkoani Kilimanjaro Mjini Moshi na kupelekea kulazwa kwenye hospitali ya Kisms hali hii ya ugonjwa imemtokea kwenye zoezi la kukieneza na kukitangaza chama cha Chauma haya yamesemwa na mkuu wa Idara ya chama  cha Chauma John Mrema . 

Ambae amesema plesha na sukari vimepanda kwa Ashim Rungwe maarufu Mzee wa Ubwabwa.

Habari na Ally Thabit Mbungo  

WADAU WA KILIMO WAKUTANA

 Dr Mustafa amewasilisha Mada ya Namna ya ubunifu utakavyo wasaidia wakulima  kulima kilimo chenye tija .

Habari na Ally Thabit Mbungo.  

Monday, 16 June 2025

NCHI YA DRC KONGO YAJA NA MIKAKATI KABAMBE KWA TANZANIA


 Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji nchi ya Drc Kongo Roland Kashwakale  amesema watahakikisha kudhibiti kwenye mipaka yao dhidi ya wahamiaji wanaotaka kuingia tanzania . Pia watakuwa wanafanya doria mara kwa mara na pindi watakapo wakamata watu wasifuata taratibu za kuingia tanzania  kupitia Drc Kongo sheria kali watachukuliwa amemuhakikishia Kamishina Mkuu wa Tanzania Dr Ana Makakala kuwa nchi ya Drc Kongo itatoa ushirikiano wao na kuimarisha ulinzi na usalama kwe nye mipaka ya nchi ya Drc Kongo na nchi ya Tanzania  kama wanavyoonekana kwenye picha ya pamoja viongozi hawa.

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

TANZANIA NA DRC KONGO YAKUTANA KUDHIBITI WAHAMIAJI HARAM


 Kamishina Uhamiaji Nchini Tanzania Dr Ana Makakala amesema lengo la nchi ya tanzania kukutana na Mkurugenzi  Mkuu wa Uhamiaji kutoka nchi ya Drc Kongo Roland Kashwakale ni kuhimarisha ulinzi na usalama kati ya Tanzania na Drc Kongo na kukuza uchumi wa nchi zote mbili Pamoja na kuleta maendeleo.

Dr Ana Makakala Kamishina Mkuu wa Uhamiaji  nchini tanzania  amesema katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu jeshi la Uhamiaji la tanzania limeweka nguvu kubwa mipakani kote kwenye nchi zinazozunguka tanzania  kwaajili ya kudhibiti wahamihaji ambao awana vibali vya kuingia tanzania hili kuimarisha ulinzi na usalama wa tanzania kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Dr Ana Makakala amesisitiza kuwa tanzania itaendelea kufanya mikutano yake na nchi za Rwanda, Burundi,Uganda na nchi zinginezo.

Mfano Mkutano wa Drc Kongo na Tanzania ni mwanzo tu wa mikutano mingiyo Dr Ana Makakala ametoa wito kwa watu wanaotaka kuja tanzania wafuate kanuni,miongozo,taratibu na sheria kabla awajaingia tanzania .

Amesema haya jijini dar es salaam 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo. 

Friday, 13 June 2025

TANZANIA YAWASIRISHA BAJETI YA KIMKAKATI

 Waziri wa Fedha Dr Mwigulu Mchemba amesema bajeti alioiwasirisha bungeni jijini dodoma kiasi cha tilioni56.49 bajeti hii itamalizia miradi mbalimbali ya kimkakati na ile itakayoanzishwa . Bajeti hii fedha nyingi za ndani zitaendesha uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 bila kutegemea mataifa ya nje .

Habari na Ally Thabit Mbungo 

ISRAEL K. ILUNDE. AKOSOA MIFUMO YA KODI

 Ndg Israel K. Ilunde Mwenyekiti wa Policy Forum(PF) na Mkurugenzi mtendaji wa YPC kutoka Kibaha mkoa wa pwani amesema mifumo ya kodi iliyopo nchini tanzania si rafiki kwa wajasilia Mali na wafanyabiashara wadogo ndio maana watu awatoi ushirikiano pindi TRA wanapowahitaji wafike kwenye ofisi zao na kwenye mamlaka zingine za kikodi.

Na pindi mtu au taasisi ukihitaji uwe mlipa kodi unapofika kwenye ofisi zao unakutana na mambo mengi ya kukukatisha tamaa . 

Mwenyekiti na Mkurugenzi ametoa wito kwa serikali na mamlaka za kikodi nchini tanzania zifanye marekebisho kwenye mifumo ya kodi na waweke mazingira rafiki na wezeshi kwa wanaohitaji kulipa kodi ambao ni wapya na wale wanaoendelea kulipa kodi hii itasaidia nchi yetu kukusanya kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa walipa kodi na kuachana na bajeti yetu ya tanzania . Kutegemea fedha za misahada na za waisani kutoka nje ya nchi.

Amesema haya makao makuu ya TGNP eneo la mabibo jijini dar es salaam. 

Habari na Ally Thabit Mbungo 

MJUMBE WA TGNP AIMIZA BAJETI YENYE USAWA WA KIJINSIA

 Mwanaharakati na Mjumbe wa TGNP Ana amesema serikali ya tanzania iakikishe bajeti wanazozipanga zizingatie usawa wa kijinsia .Kwani bajeti iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha na Dr Mwigulu Mchemba yenye kiasi cha shilingi za kitanzania tilioni 56.49 ,kwa kiasi kikubwa aijazingatia misamaha ya kikodi kwenye taulo za kike,visaidizi vya watu wenye ulemavu na mengineyo.

Ametoa wito kwa Wanaharakati wa tanzania kuendelea kupaza sauti kwa serikali amesema haya makao makuu ya TGNP eneo la mabibo jijini dar es salaam. 

Habari na Ally Thabit Mbungo

MWANA HARAKATI WA TGNP ALIA NA BAJETI

 Mwanaharakati Mkongwe wa TGNP BI Subira  ameitaka serikali ya tanzania  kabla ya kupanga bajeti ni vyema kuwashirikisha wananchi wote kuanzia ngazi ya kaya ,kitongoji au Mtaa ,Kijiji,Kata,Tarafa,Wilaya,Mkoa na ngazi ya Kitaifa lengo kuwa na bajeti shirikishi .

Hamesema haya Makao Makuu  TGNP  eneo la mabibo jijini dar es salaam. 

Habari na Ally Thabit 

Friday, 9 May 2025

WALIP MPIGA KATIBU MKUU BARAZA LA MAASKOFU WATIWA MBALONI

 Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam  Mulilo Jumanne Mulilo amethibitisha kuwa watu waliompiga na kumjeruhi Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Dkt Charese  Kitima wamekatwa na utaratibu wa kufikishwa Mahakamani unafanyika .

Ambako hivi karibuni eneo la Kurasini Makao Makuu ya Baraza la Maaskofu nchini Tanzania majira ya saa nne ya usiku watu hawa walifika eneo hili na kumshambulia Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania.

Habari na Ally Thabit 

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA AIMIZA UTUNZAJI WA AMANI NA USALAMA WAKATI WA UCHAGUZI


 Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini Tanzania Nyaoza awataka Wanachama,Wapenzi na Viongozi wa Vyama vya Siasa Kutunza na Kuilinda Amani iliyopo kipindi cha Uchaguzi na baada ya uchaguzi. 

Anesema haya kwenye mkutano mkuu wa chama cha NLD ambako chama hiki wanachama wake walipomchagua na kumpitisha Doyo Hassan Doyo  kuwa ndiye atakayepeperusha bendera ya urais ifikako mwezi wa kumi mwaka huu 1025 kwenye uchaguzi mkuu.

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

DOYO KUWA RAISI WA TANZANIA


 Doyo Hassan Doyo amesema Mwaka huu 2025 Katika Uchaguzi Mkuu Utakao Fanyika mwezi wa Kumi yeye ndiye atakayekuwa Rais wa Tanzania. Kupitia Chama cha NLD.

Kitu ambacho kinamfanya awe na uhakika wa kuwa Raisi kutokana na dira ya chama chake cha NLD ambako kusimamia Kilimo kwa kuwapa wakulima mbegu bora na za kisasa pamoja na kuwatafutia masoko ya kitaifa na kimataifa. Ugawaji wa mbolea na pembeje bule kwa wakulima . Kilimo cha kisasa kupitia umwagiliaji,Usimamizi bora kwenye sekta ya madini ambako atahakikisha kila mchimbaji anapata vifaa vya kisasa vya kuchimbia madini na kuweka bei elekezi, Utoaji wa resen kwa wazawa bila mashariti magumu.

Sekta ya Ajira .

Doyo Hassan Doyo Mgombea kiti cha urais kupitia chama cha NLD atahakikisha kila mtanzania anapata ajira ya kudumu,hatakuza sekta ya viwanda na upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na kuimarisha sekta ya Afya na upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa gharama nafuu.

Vile vile atakuza sekta ya Usafirishaji na Uchukuzi kwenye miundombinu ya majini ,nchikavu na Angani amesema haya baada ya kupewa nafasi ya kupeperusha bendera ya uraisi kupitia chama cha NLD . Hivyo amewataka watanzania wamchague Doyo Hassan Doyo  awe rais wa tanzania kupitia chama cha NLD. Kwani ccm walio ahixi hawajatekeleza hata moja .

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

WAZIRI WA AFYA WA ZANZIBAR AWATOA HOFU WATALII


 Nasoro Mazrui Waziri wa Afya wa Zanzibar amesema  wizara yake ya afya  inasimamia kikamilifu maswala ya Afya Zanzibar kwa kina na umakini mkubwa .Hivyo anawataka watalii kutoka nchi mbalimbali duniani wafike Zanzibar kufanya Utalii. Kwani Afya iko salama na imeimarika kwa Zanzibar na wakipata changamoto za kiafya mara nyingi wizara yake inawatibu bule.

Pia miundombinu ya kiafya imezidi kujengwa na kuimarishwa kwa Unguja na Pemba na Madaktali bingwa wapo wa kutosha .

Waziri wa Afya wa Zanzibar anawataka wazanzibar wakate bima za Afya.vilevile ameongeza kwa kusema  katika mwaswala ya watu wenye ulemavu zanzibar yanazingatiwa kwa kiasi kikubwa .Mfano Mashuleni kuna miundombinu rafiki na wezeshi kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa aina zote.

Kwa upande wa wanafunzi wasioona kuna maandishi ya nukta nundu pia kwa watu wenye ulemavu wakienda kupata huduma kwenye vituo vya Afya ,Zahanati, Mahospitalini na maeneo mengine wanapewa kipaumbele.

Habari picha na Victoria Stanslaus. 

BARAZA LA MITIHANI LAJIVUNIA ONGEZEKO LA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA

 Ndugu Wanahabari Mitihani ya Kidato cha sita ( ACSEE) na Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada imeanza tarehe 05 mei 2025 Tanzania Bara na Zanzibar. Mtihani wa Ualimu utakamilika tarehe 19 Mei,2025 na Kidato cha Sita tarehe 26 Mei,2025. Mtihani wa kidato cha sita utafanyika katika jumla ya shule za secondari 982 na vituo vya watahiniwa wa kujitegemea 245. Aidha , Mtihani wa Ualimu  utafanyika katika Vyuo vya Ualimu 68.

USAJILI WA WATAHINIWA

(a) Watahiniwa wa Kidato cha Sita 

Jumla ya watahiniwa 134,390 wamesajiliwa kufanya mtihani wa  Kidato cha Sita 2025 ambapo watahiniwa wa shule ni 126,957 na  Watahiniwa wa Kujitegemea ni 7,433.

Kati ya Watahiniwa wa Shule 126,957 waliosajiliwa, wavulana ni64,581 sawa na asilimia 50.87 na Wasichana  ni 62,376 sawa na asilimia 49.13. Aidha  watahiniwa  wenye mahitaji maalum ni 453 ambapo kati yao weenye Uoni hafifu ni 300, wasioona ni 16, wenye Uziwi 58, wenye ulemavu wa akili ni 04 na wenye ulemavu  wa viungo vya mwili ni 75.

Kati ya  Watahiniwa wa Kujitegemea 7,433 waliosajiliwa,wavulana 4,782 sawa na asilimia 64.33 na wasichana ni 2,651 sawa na asilimia 35.67. Aidha Watahiniwa  wa Kujitegemea wenye mahitaji maalum wako 151 ambapo kati yao wenye uoni hafifu ni142 na wasioona ni 9.

Mwaka 2024 idadi ya watahiniwa wa Shule na Kujitegemea waliosajiliwa walikuwa 113,536. Hivyo, kuna ongezeko la jumla ya watahiniwa 20,854 (18.37) kwa mwaka 2025 ukilinganisha na mwaka 2014.

(b) Mtihani wa Ualimu

Jumla ya watahiniwa 10,895 wamesajiliwa kufanya mtihani wa Ualimu Mei 2025.

Kati ya watahiniwa hawa 3,100 ni wa ngazi ya Stashahada na 7,795 ni wa ngazi ya Cheti.kwa ngazi ya Stashahada, wanaume ni1,751 sawa na asilimia 56.48 na wanawake ni 1,349 sawa na asilimia 43.52. Aidha kwa ngazi ya Cheti watahiniwa 3,987 sawa na asilimia 51.15 ni wanawake .

Watahiniwa  wenye Mahitaji Maalum waliosajiliwa kufanya mtihani wa Ualimu 24.Kati yao 2 ni wenye Uoni hafifu kwa ngazi ya Stashahada; na 16 wenye uoni hafifu ,3 wasioona ,1uziwi,1Ulemavu wa viungo ni wa ngazi ya Cheti.

Mwaka 2024 idadi ya Watahiniwa wa Ualimu waliosajiliwa walikuwa 11,435. Hivyo, kuna upungufu wa jumla ya watahiniwa 540 (4.72) kwa mwaka 2025 ukulinganisha na mwaka 2024.

MAANDALIZI YAMEKAMILIKA PAMOJA NA KUSAMBAZWA KWENYE VITUO USIKA PAMOJA NA VITABU VYA KUJIBIA  NA NYARAKA ZOTE MUHIMU KWENYE MIKOA YOTE  KWA TANZANIA BARA NA ZANZIBAR. 

Mitihani  wa kidato cha sita  ni muhimu kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla kwani upima  maarifa .stadi na umahiri wa wanafunzi katika maeneo yote waliojifunza  kwa kipindi cha miaka miwili ya elimu ya secondari ya juu. Matokeo ya mtihani huu hutumika katika uchaguzi wa wanafunzi wanaojiunga  na Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati katika fani mbalimbali za Utaalaam wa kazi kama vile Afya ,Kilimo,Ualimu,Ufundi na nyinginezo. Hivyo Mtihani huu ni muhimu sana kwa wanafunzi ,Wazazi na Taifa kwa ujumla.kwa upande wa mtihani wa Ualimu,mtihani hufanyika kwa lengo la kupata walimu makini ambao watafundisha  katika ngazi ya Elimu ya Msingi na Secondari.

WITO KWA KAMATI ZA MITIHANI,WASIMAMIZI,WAMILIKI WA SHULE NA JAMII

Wito kwa Kamati za Mitihani

Pamoja na Maandalizi yote muhimu yaliyofanyika  Kamati za Miitihani za Mikoa  na Almashauri ziakikishe kuwa usalama  wa Vituo vya Mitihani vinaimarishwa na kwamba Vituo hivyo vinatumika kwa mujibu wa Mwongozo uliotolewa na Baraza la Mitihani la Tanzania .Aidha , Wahaakikishe wasimamizi wote waliopangwa kusimamaia uendeshaji wa mtihani  katika kituo husika  wanafika kwa wakati katika vituo husika.

WITO KWA WASIMAMIZI

Baraza linatoa wito kwa wasimamizi wote walioteuliwa kusimamia mitihani kufanya kazi yao kwa weledi na uadilifu wa hali ya juu.Wasimamizi wahakikishe kuwa wanazingatia kanuni za mitihani, Tarabu na Miongozo ya Baraza la mitihani waliyopewa ili kila mtahiniwa apate haki yake.

Aidha ,wasimamizi wahakikishe watahiniwa wote wenye mahitajiamaalum wanafanya mitihani yao ipasavyo ili wapate haki zao za  msingi.Haki hizo ni pamoja na  kuwapa mitihani yenye  maandishi ya nukta nundu kwa watahiniwa wasio ona  na Maandishi ya kukuza kwa watahiniwa wenye uoni hafifu. Watahiniwa wote wenye mahitaji maalum waongezewe muda wa dakika 20 kwa kila saa kwa somo la Hisabatina dakika 10 kwa kila saa kwa masomo mengine,kama kanuni za mitihanizinavyoelekeza .Wasimamizi wahakikishe watahiniwa wote wanafanya mitihani kwa muda ulio pangwa na katika hali ya utulivu.

WITO KWA WATAHINIWA

Baraza linaamini kuwa walimu na wanafunzi wamewaandaa vizuri katika kipindi cha miaka miwili ya secondari ya juu na kozu ya mafunzo ya Ualimu. Hivyo ni matarajio ya Baraza la mitihani kuwa kila mtahiniwa atafanya mtihani wake kwa kuzingatia kanuni za mitihani.Aida,Baraza halitarajii kuona mtahiniwa yeyote atakayebainika kufanya udanganyifu. Mtahiniwa yeyote atakayebainiwa kufanya udanganyifu  kwa  Mitihani matokeo yake yatafutwa kwa mujibu wa kanuni za Mitihani.

WITO KWA WAKUU WA SHULE  MA WAMILIKI WA SHULE NA VYUO

Baraza linawaasa Wakuu wa Shule na Wakuu wa Vyuo kutekeleza majukumu yao ya usimamizi kwa kuzingatia  mwongozo wa usimamizi uliotolewa na Baraza la Mitihani  na kuepuka kuingilia usimamizi wa watahiniwa ndani ya vyumba vya mitihani.

Aidha, Baraza linawaasa Wamiliki wa Shule  na Vyuo kutambua kuwa shule zao ni vituo maalum vya mitihani na hivyo hawatakiwi kwa  namna yoyote kuingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani katika kipindi chote cha ufanyikaji wa mitihani hii.  Baraza halitasita kukifuta kituo chochote cha mitihani endapo litajiridhisha pasipo shaka kuwa uwepo wake unahatqrisha usalama wa Mitihani.

WITO KWA JAMII

Baraza linatoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano unaotakiwa katika kuhakikisha Mitihani ya Kidato cha Sita na Ualimu mwaka 2015 inafanyika kwa amani na utulivu. Wananchi wanaombwa kuhakikisha kuwa hakuna mtu yeyote asiyehusika na mitihani anaingia kwenye maeneo ya shule na vyuo katika kipindi chote chamitihani. Kwa kufanya hivyo,tutawawezesha  wanafunzi waliosajiliwa kufanya mitihani ya Kidato cha Sita na Ualimu Mei 2025 kwa amani na utulivu.

Haya yanesemwa na Katibu Mtendaji Dkt .Said A. Mohamed.

Habari na Ally Thabit Mbungo 



Saturday, 22 March 2025

TGNP YAGUSWA NA UONGOZI WA RAIS DR SAMIA

 

Mkurugenzi  Mtendaji  Tgnp Liliani Liundi amesema tarehe 19 ya mwezi 3 mwaka 2025 rais Dr Samia ametimiza miaka minne ya uongozi wake kitendo hiki wanaharakati wanaopigania haki za binadamu kwao ni mafanikio makubwa kwani watu wengi waliamini kuwa mwanamke awezi kuiongoza nchi . Kupitia rais Dr Samia zana hii mbaya na potofu dhidi ya mwanamke imeweza kufutwa na kunjwa.

Pia Tgnp na wadau wanaopigania haki za binadamu wanampongeza rais Dr Samia baada ya kuapishwa alipohutubia bunge alisema atapigania na kuondoa mifumo dume, ataondoa mila na destuli potofu dhidi ya mwanamke na atawapa fursa mbalimbali wanawake  na hili amelitekeleza kwa vitendo kwa kuwapa fursa mbalimbali wanawake kwenye sekta tofauti na amewafungulia milango ya uongozi . Pia amemtua ndoo mama kichwani kwa kuanzisha miradi ya maji, amewapigania maswala ya ardhi, amefanya maboresho ya sera  ya ardhi ambako zamani mwanamke ananyimwa fursa ya kumiliki ardhi, kwenye sekta ya elimu amejenga madarasa, mabweni , matundu ya vyoo na amefanya maboresho dhidi ya mtoto wa kike akipata ujauzito baada ya kujifungua aweze kuludi shule na kuendelea na masomo,   kuwainuwa wanawake kiuchumi  kwa kuanzisha majukwaa mbalimbali na kuwapa mikopo nafuu.

Amesema haya kwenye viwanja vya  Tgnp  mabibo kwenye maadhimisho ya mwanamke duniani na uzinduzi wa ripoti ya miaka 30 ya tamko la Beijing nilipofanya nae mahojiano.

Habari picha na Victoria Stanslaus 

UNDP YAIMIZA MIKAKATI IONGEZWE YA KUWAINUWA WANAWAKE


 Mwakilishi wa  Undp  amesema Wanawake waweze kupewa fursa mbalimbali ili waweze kujikwamuwa kiuchumi hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kuondokana na ukatili wa kijinsia .

Ndani ya miaka 30 ya Beijing wanawake wamejikomboa kiungozi, ardhi na wameweza kujiamini amesema haya viwanja vya  tgnp mabibo katika siku ya mwanamke duniani na uzinduzi wa ripoti ya Beijing. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

BODI YA SUKARI YAJIVUNIA MAFANIKIO YA RAIS DR SAMIA KWA MIAKA MINNE


 Prof Keneth Bengesi Mtendaji Mkuu wa  Bodi ya Sukari  Tanzania amesema tangu tarehe 19 mwezi wa 3 mwaka 2021 baada ya Dr Samia  kuapishwa na kuwa rais wa tanzania  amewezesha sekta ya Sukari  kukuwa na kupiga hatuwa kwa kuwapa ruzuku wakulima wa miwa, kwa kufanya mabadiliko ya sheria ya NFRA kwa kupewa mamlaka ya kuhifadhi Sukari ambako mwanzoni wafanyabiashara wa sukari walikuwa wanaifadhi wenyewe na kupelekea ufichaji wa sukari na kusababisha kupanda kwa bei ya sukari olela olela na kupelekea usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa sukari  nchini tanzania. 

Ujenzi wa viwanda vya sukari na upanuzi wa viwanda vya zamani vya sukari. Prof Keneth Bengesi amesema rais Dr Samia  kwa kipindi cha uongozi wake wa miaka minne amekamilisha miradi yote ilioachwa na mtangulizi wake.mfano ujenzi wa bwawa la mwalimu nyerere, daraja la Kigongo busisi mwanza, ujenzi wa SGR, uwanja wa msarato jijini dodoma , amekuza demokrasia kwa kuwa nafasi viongozi wa vyama vya siasa kufanya mikutano yao kwa uhuru, maridhiano kwa kupitia farsafa yake ya R nne na kuwarejesha watu wote waliokimbia nje ya nchi.

Na mengineyo mengi ameyafanya rais Dr Samia ikiwemo kufunguwa fursa kwa wafabiashara, wasanii kwa kusafiri nao nje ya nchi kwaajili ya kuwatafutia masoko ya kitaifa na kimataifa , ameweka mazingira rafiki na wezeshi kwa wawekezaji kuwekeza kwenye sekta ya sukari na maeneo mengineyo.

Ametoa wito kwa watanzania waendelee  kumuunga mkono na mwaka huu kwenye uchaguzi wampe kura za kutosha rais Dr Samia  ili aendekee kuwa rais wa Tanzania hakika rais Dr Samia  mitano tena. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

PICHANI KAMA INAVYOONEKANA RIPOTI ILIYOZINDULIWA TGNP


 Habari picha  na Ally Thabit 

MGENI RASMI AKIZINDUA RIPOTI YA TGNP


 Mwenyekiti wa Jumuhiya ya Kiislamu na Waziri Msitaafu wa wizara ya viwanda na biashara na wizara ya maendeleo  ya jamii , jinsia na watoto ambae alikuwa   mbunge mwanamke  kwanza kuchaguliwa na wananchi mnamo mwaka 1985 Hajati Shamimu pichani akizindua ripoti ya TGNP inayoeleza na kueleza hatua na changamoto zilizo jitokeza baada ya mkutano wa Beijing uliofanyika mwaka 1995 ambako kwa sasa tunatimiza miaka 30 ya Beijing.

Habari picha na Ally Thabit 

HAJATI SHAMIMU AWAPONGEZA TGNP

Mwenyekiti wa Jumuhiya ya Wanawake  wa Kiislamu Taifa na Mwana harakati mkongwe amewapongeza TGNP kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kupiga vita ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake , wasichana na makundi mengineyo na kupelekea idadi ya wanawake ya kuwa viongozi nchini tanzania imeongezeka. Mfano wabunge wanawake wa ku haguliwa wapo 26 ukilinganisha na miaka ya nyuma haya ndio walio yapigania kwenye mkutano wa Beijing nchini China mwaka 1995 amesema haya kwenye siku ya mwanamke duniani kwenye viwanja vya TGNP  Mabibo jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit 

ST. MATTHEW'S YAGUSWA NA MIAKA MINNE YA RAIS DR SAMIA


 Wakiri Msomi na Mkurugenzi  wa Shule za St. Matthew's Dr Peter Tadeo Mtembei amesema tarehe 19 mwezi wa 3 mwaka 2025 rais Dr Samia  ametimiza miaka minne ya uongozi wake  .Katika miaka hii amekuza na kustawisha maridhiano, miundombinu mfano ujenzi wa SGR,Barabara , Madaraja na Upatikanaji wa Maji safi na salama kwa wananchi wote.

Pia rais Dr Samia ameanzisha miradi mipya na kukamisha miradi ilioachwa na mtangulizi wake. kupitia sekta ya elimu amejenga madarasa mapya, mabweni, ameajili waalimu, ujenzi wa nyumba za walimu na mabadiliko ya sera ya elimu ambako inamuwezesha mwanafunzi akimaliza elimu yake anaweza kujiajili ama kuajiliŵa.

Vilevile Wakiri Msomi na Mkurugenzi wa Shule za St. Matthew's Dr Peter Tadeo Mtembei amewataka wa'azi na walezi kuwaandikisha watoto wao kwenye shule zote nane za St Matthew's  kwani shule zao zinatoa elimu bora nidhamu na usalama ni vitu vya msingi na wanavizingatia na ufahuru wa uhakika na wakiwango cha juu.

Ametoa rai kwa wahitimu 97 wa kidato cha sita kwenye shule ya St. Matthew's iliyopo mkoa wa wa pwani wilaya ya mkuranga kata ya mwandege katika maafari haya ya 20 kwa mwaka 2025 pindi wa wakimaliza mitihani ya taifa wakawe mabalozi wema , waendeleze maadili mema kwa jamii, tabia njema na watumie elimu walioipata kutatuwa changamoto za kijamii.

Pia amewasisitiza wazazi na walezi kwa elimu bora, nidhamu na usalama kwa wanafunzi na gharama nafuu za ada ni vyema wachague shule za St Matthew's  kwani kupitia Maendeleo Bank  wazazi na walezi  watakopeshwa ada kwa riba nafuu ya asilimia moja .

Habari picha na Victoria Stanslaus 

MKUU WA WIRAYA YA KISARAWE AFUNGUWA MILANGO KWA WAZAZI NA WALEZI KWENYE SHULE YA ST MATTHEW'S

 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Dr Tito Magoti anawataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kwenye shule  za St. Matthew's  kwani zinafundisha vizuri mpaka kupelekea mwanafunzi kuweza kujiajili kupitia mafunzo ya ujasilia Mali na kuondokana kuwa tegemezi katika jamii .

Shule za St. Matthew's zinaunga mkono na kutekeleza maono ya rais Dr Samia  kwa kuwapa wanafunzi elimu bora na viwango vikubwa hivyo ni vyema wazazi na walezi wasiache kuwapeleka watoto wao kwenye shule  za St. Matthew's.

Amesema haya kwenye maafari ya 20 ya kidato cha sita ambako wahitimu 97 wanamaliza elimu yao kwenye shule ya St. Matthew's  wilaya ya Mkuranga kata ya mwandege mkoani pwani.

Habari na Ally Thabit 

MAKAMU MWENYEKITI WA BODI YA SHULE YA ST. MATTHEW'S AFICHUWA SIRI NZITO

 Makamu Mwenyekiti  wa Bodi Shule ya St. Matthew's Dr Mwisiga   amesema siri kubwa ya mafanikio kwa shule za St Matthew's  katika wanafunzi kufahuru kwa kiwango kikubwa  ni mazingira ni rafiki na wezeshi ya kufundishia na kujifunza wanafunzi.

Kuwepo kwa mahabara za kutosha na matumizi ya kiteknolojia ya kufundishia na kujisomea .swala la nidhamu, usalama na  malezi ni misingi inayosimamiwa na kuzingatiwa kwenye shule zote za St. Matthew's. 

Makamu Mwenyekiti wa  Shule za St. Matthew's anawataka wazazi na walezi wawpeleke watoto wao kwenye shule za St Matthew's  kwani watapata elimu bora na gharama ni nafuu na inalipika kwa hawamu nne lakini pia kupitia Maendeleo Bank watapata mkopo wa ada wenye riba ya  asili moja .Makamu Mwenyekiti  wa bodi  Dr Mwisiga amesema swala la maadili, mafundisho ya dini , tabia njema ni vitu. Vinavyosimamiwa na kuzingatiwa kwa wanafunzi  ndio maana ufahuru unaongezeka mwaka hadi mwaka  amesema haya kwenye maafari ya 20 ya kidato cha sita kwa wanafunzi wapatao 97 wa shule  ya St. Matthew's. 

Habari na Ally Thabit 

ST. MATTHEW'S INATOA ELIMU KWA GHARAMA NAFUU

Mkuu wa Shule ya St. Matthew's  Josefu Malahila. amewataka Wazazi na walezi kuwahandikisha watoto wao kwenye shule zote nane za St. Matthew's  kuanzia elimu ya Awali , msingi kwa Secondary kuanzia kidato cha kwanza mpaka kidato cha sita. Ambako mzazi analipa hada kwa awamu nne.

Shule za St. Matthew's zina malengo ya kutoa elimu inayozingatia nidhamu, usalama kwa wanafunzi na malezi bora kwa wanafunzi wote  shule ya St Matthew's  inamuwezesha mwanafunzi kujiajili ama kuajiliwa amesema haya kwenye maafari ya kidato cha sita ya wanafunzi wapatao 97 wa shule ya St.Matthew's. 

Mkuu wa Shule ya St. Matthew's  Josefu Malahila ametoa wito kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita elimu na ujuzi walioupata wakatumie katika kutatuwa changamoto za kijamii.

Habari na Ally Thabit 

Wednesday, 19 March 2025

BALOZI RIBERATA MULAMULA AWATAKA WANAWAKE KUCHANGAMKIA FURSA MBALIMBALI

 Balozi Mulamula amewataka Wanawake Kuchangamkia fursa mbalimbali miongoni mwao zikiwemo fursa za kiuchumu ambako wakifanya biashara au ujasilia Mali watafanikiwa kiuchumi .

Pia amewataka wanawake wote wawe na elimu ya fedha amesema haya wakati wa kuwajengea uwezo wanawake na wasichana  walipo kutana na Women Shaping the future (SRS) jijini dar es salaam. 

Habari na Ally Thabit 

SAMIA 4×4 WANAWAKE WAJAWAZITO WAGUSWQ NA SAMIA 4×4


 Salmu Kikeke amesema Tarehe 5 ya Mwezi wa 4 mwaka  2025 amesema kutakuwa na msafara wa magari mia moja yataelekea mkoani Tanga eneo la pangani pia yatapita kwenye ushoroba wa saadani  lengo ni kuonesha mafanikio na maendeleo yaliofanywa narais  Dr Samia  kwa kipindi cha miaka minne ya uongozi wake.

Samia 4×4  itagawa vifaa vya kujifungulia wamama  wajawazito  ambako vifaaa hivyo ni zaidi ya elfu moja ivyo wanawake wote wanatakiwa kujitokeza kwa wingi .

Pia msafara huu utapokelewa na waziri wa maji Awesu Juma Awesu .katika msafara huu kutakuwa na uzinduzi wa miradi mbalimbali iliyotekelezwa na rais Dr samia  na kilele cha msafara huu wa Samia 4×4 utafikia tamati tarehe 8 mwezi wa 4 mwaka 2025.

Habari picha na Ally Thabit 

MAENDELEO BANK YAJA NA CLICK BANK SMILE

 Mwenyekiti wa Bodi ya Maendeleo Bank Plc Prof Ulingeta Mbamba Azindua Huduma ya CLICK BANK SMILE amesema uzinduzi wa Internet Banking .

Amechukua fursa ya kuwapongeza kwa dhati Menejimenti na  wafanyakazi wa Maendeleo bank kwa juhudi kubwa walizofanya kuhakikisha  huduma hii mpya ya  inakamilika na kuzinduliwa kwa mafanikio.jitohada,maarifa,na kujituma kwao kumeifanya Maendeleo bank kuwa kinara wa ubunifu katika sekta ya kifedha amewaponeza sana .

Katika Ulimwenngu wa sasa wa kidigitali,benkiinayoendelea ni ile inayokwenda sambamba na teknolojia- Click Bank Smile ni jibu sahihi kwa mahitaji yawateja wa leo wanaotaka huduma za haraka ,salama na zinazoweza kupatikana mahali popote  na muda wowote .

Hivyo Matarajio ya huduma  hii itaongeza ufanisi wa biashara, hasa kwa wafannyabiashaara wadogo na wa kati na kuokoa muda na gharama za wateja  kwa kila kitu kinapatikana kwa mfuso wa kidole  kwenye simu au kompyuta.

Huu ni ushahidi kwa Maendeleo Bank Plc inatekeleza kwa vitendo mkakati wake wa ukuaji wa kidigitali na kufanikisha azma ya kuwa benki ya kisasa inayoendana na mabadiliko ya kiteknolojia.

Kwa Mujibu wa Fin-Scope Survey ya Mwaka 2023 kiwango cha upatikanaji na matumizi ya huduma rasmi za kifedha kiliongezeka hadi 89% na 76% mwaka 2023 kutoka 86% na 65% mwaka 2017". Hii ilichangiwa sana na uimarikaji wa huduma za kifedha kwa njia ya kidigitali na hasa huduma za kifedha kwa njia ya simu.

Hivyo ni Imani kuwa huduma  hii ya Internet banking  si tu kwamba itawanufaisha wateja wa Maendeleo Bank  tu bali pia itasaidia ukuaji wa uchumi wa wananchi kwa kuongeza ujumuishi wa kifedha nchini. Kwa namna hii, Maendeleo Bank inachangia moja kwa moja katika malengo ya serikali , katika kuimarisha uchumi wa kidigitali na kuhakikisha wananchi wengi wanapata huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.

Pia ametoa wito kwa watanzania wote kutumia  huduma hii ya CLICK BANK SMILE  ili kujionea urahisi wake na manufaa yake .Hii ni huduma iliyoandaliwa kwa ajili yenu hivyo ni jukumu letu kuitumia kwa tija . 

Kwa heshima na taadhima ,sasa ameitangaza rasmi kuwa huduma ya Internet banking  ya Maendeleo Bank Plc -CLICK BANK SMILE- imezinduliwa rasmi, leo tarehe 18 mwezi wa tatu mwaka 2025 .PONGEZI KWA MAENDELEO BANK PLC!.

Habari na Ally Thabit 

Tuesday, 11 March 2025

TAASISI YA BI AISHA SURURU YAAHIDI MAKUBWA KWA VIJANA


 Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya BI Aisha Sururu amesema wataendelea kuwawahifadhisha Quran vijana wote wa kitanzania na wasio watanzania lengo wamtambue mungu na wawe wenye maadili mama. 

BI Aisha Sururu ametoa wito kwa watanzania na wasio watanzania kutoa michango yao ya fedha na Mali ili taasisi yake ijenge madarasa na mabweni eneo la kiparang'anda mkoa wa pwani kiasi kinachoitajika ni zaidi ya bilioni mia nne.
Amesema haya jijini dar es salaam  kwenye mashindano  ya kuhifadhi Quran. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

Monday, 10 March 2025

AMANA BENK YAAIDI MAZITO


 Mkurugenzi wa Amana Benk Abubakari amesema watazidi kudhamini na kufadhiri mashindano ya Quran lengo kuwatia moyo wanaohifadhi na kusoma Quran  na kukikuza kitabu cha mungu amesema haya kwenye mashindano ya 25 ya kuifadhi Quran  yalioandaliwa na taasisi ya Bi Aisha Sururu foundation ambayo yamefany8ka jijini dar es salaam. 

Habari picha na Victoria Stanslaus 

BI ASHA DIWANI VITI MAALUM JIJI LA ILALA AIMIZA WAZAZI NA WALEZI KUWAPELEKA WATOTO WAO KUSOMA QURAN


 Diwani wa Viti Maalum  na Mweka hazina kwenye taasisi ya Aisha Sururu Foundation anawataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kusoma Quran  kwani kuna faida zinapatikana  zikiwemo kuwa na imani,kuulumia binadamu mwenzako,kuwana ofu na kuwa mwadilifu na weredi katika kazi na jamii kwa ujumla .

Habari picha na Victoria Stanslaus

MJUMBE WA ALMASHAURI KUU YA CCM APONGEZA MASHINDANO YA QURAN

 

Amoll Abudi Juma Mjumbe wa Almashauri Kuu ya ccm taifa mkoa wa dar es salaam  amempongeza bi Aisha Sururu kwa kuendesha mashindano ya quran kwa miaka ishilini na tano pamoja na kuwahifazisha maneno ya mungu watoto yatima,wajane,wasiojiweza,watu wa makundi maalum kwani kufanya hivi kunasaidia kupata watu wenye maadili,wenye ofu ya mungu na hatimae nchi ya tanzania inapata amani ,upendo na utulivu.

Habari picha na Victoria Stanslaus 

SHEIKH PONDA AELEZA UMUHIMU WA FUNGA

 Sheikh Issa Ponda  amewataka Waislamu wote wale ambao awana matatizo ya kiafya waweze kutekeleza nguzo ya nne ya kiislam kati ya tano wafunge ramadhani ndani ya mwezi huu wa ramadhani kwani watakuwa waja wema  pia wasome Quran mara kwa mara.

Habari na  Victoria Stanslaus 

SHEIKH CHIZENGA AELEZA FAIDA ZA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

 Katibu Mkuu  wa Baraza Kuu la Ulamaa Bakwata amewataka waislamu nchini tanzania wafunge ramadhani kwenye mwezi huu mtukufu wa ramadhani kwani miongoni mwa faida watakazozipata ni kuimarika kwa afya zao .Pia mungu atawasamehe makosa yao na zambi zao pia anawasisitiza watanzania wote bila jujali dini,kabila,rangi na jinsia wazidi kumuombea afya njema rais Dr Samia  kwani amekalisha miradi yote na anatenda haki kwa kila mmoja hivyo ni vyema kumchagua kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu hakika mama samia mitano tena.

Habari picha na Ally Thabit. 

KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI AWATOA OFU WATANZANIA















Eng. Felchesmi J.Mramba  Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati amewatoa ofu watanzania  kuhusu uhamuzi uliofanywa na serikali yetu ya tanzania kwa kununua umeme megawati mia moja kutika nchi ya Ethiopia .

Kwani Umeme huu unanunuliwa kwa gharama ndogo  kwani umeme utasaidia mikoa ya kaskazini kupata umeme wa uhakika  kwenye viwanda na  maeneo wanayoishi wananchi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Eng Felchesmi J. Mramba amesema tanzania itapata umeme huu kupitia kutoka Ethiopia kwa kutumia miundombinu ya Kenya kwani Kenya na Ethiopia zipo karibu . Serikali ya tanzania imefanya uhamuzi huu kwa sababu tunapoteza megawati kumi na saba za umeme kwa kutumia kupitisha umeme kwa njia za ndani ya nchi yetu Pia sera zetu zinaruhusu kununua umeme nchi za nje .

Mfano Mkoa wa Rukwa umeme unaotumika ni kutoka nchi ya Zambia ,Umeme unaotumika  mkoa wa Kagera unatoka nchi ya Uganda hata nchi ya Ethiopia amnayo inatuuzia tanzania  umeme licha ina megawati elfu sita lakini bado inanunua umeme nchi zinginezo na mpaka sasa nchi zipatazo tatu zimeleta maombi za kuuziwa umeme na tanzania  na wamekubaliana na wapo hatua za mwisho nchi hizi ni Burundi,Rwanda na Zambia .

Na sasa Tanzania kwa Kushirikiana na Zambia wanatekeleza mradi wa Taza ambao megawati sita za umeme zitauzwa nchini Zambia na mradi umefikia asilimia hamsini .Nakampu  ya Mifodi ya Zambia itanunua megawati mia moja tanzania  nchi zinginezo  zitazonunu umeme tanzania Msumbiji,Marawi,Dr kongo

Katibu Mkuu amesisitiza kuwa bei tunayouziwa umeme na nchi ya Ethiopia  ni bei na fuu na rafiki kwani ni dora saba nukta saba sent .

Swala la Bwawa la Mwalimu Nyerere limeleta ukombozi katika kupatikana umeme wa kutosha nchini tanzania hivyo watanzania tuunge mkono uwamuzi uliofanywa na serikali yetu ya tanzania na tuendelee kumpongeza rais Dr Samia kwa kukamilisha bwawa la mwalimu nyerere na miradi mingineyo mpaka kuwezesha nchi kuondokana na tatizo la kukatikakatika umeme mara kwa mara.

Habari picha na Victoria Stanslaus 

Wednesday, 26 February 2025

MKURUGENZI AIMIZA MIFUMO YA MITAJI YA MASOKO YA ISA HIIMARISHWE


 Mitaji ya Masoko ya Isa Ikihimarishwa Idadi ya Wawekezaji itaongezeka ambako kwa sasa  watu laki6 wamewekeza kwenye masoko ya isa Cipiey Nikolaus ameipongeza kampuni ya VERTEX INTERNATIONAL SECURITIES LTD kwa kusimamia fedha za wawekezaji.

Habari picha na Ally Thabit 

Saturday, 22 February 2025

MSANII JEYB AWATAKA WASANII KUMUUNGA MKONO RAIS DR SAMIA


 Barozi wa Chama cha Ccm Msanii Jeyb anawata wasanii nchini tanzania kujiunga na chama cha ccm na kumuunga mkono rais Dr Samia kwani ameweza kutekeleza kwa vitendo miradi yote ya kimkakati mfano ujenzi wa SGR  ,amewapa wasanii mikopo ya fedha ambayo aina riba bila kujali chama dini wala rangi na jinsia .

Barozi Jeyb amesema watafanya kampeni nchi nzima ya kuakikisha watu wanajiunga na chama cha ccm na rais Dr Samia  anashinda kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Habari picha na Ally Thabit 

KATIBU MKUU NA MSEMAJI WA SERIKALI ABAINISHA MIKAKATI YA WAKULIMA WA KAHAWA


 Greyson Msigwa Katibu Mkuu na Msemaji wa Serikali amesema kuwa serikali ya tanzania imeweka mazingira rafiki na wezeshi kwenye zao la kahawa kwa kuwapa wakulima wa kahawa pembejeo zenye ubora na za kisasa ,Mbegu zenye ubora,Mafunzo kwa wakulima wa kahawa,Teknolojia za kisasa na zenye ubora na kufanya tafiti pamoja na kuwatafutia masoko wakulima wa kahawa ndani ya nchi na nje ya nchi.

Lengo la kufanya haya yote ni kuwainuwa wakulima wa kahawa kiuchumi na kuongeza uzalishaji wenye tija katika kahawa . Baada ya serikali kuyafanya haya yote chini ya rais Dr samia hatimae kahawa ya tanzania imepanda thamani kubwa na kupelekea kahaya ya tanzania kuuzika katika masoko ya kitaifa na kimataifa .

Katibu Mkuu na Msemaji wa Serikali amesisitiza kuwa watu wenye ulemavu katika zao la kahawa wanashirikishwa kikamilifu Pia kupitia mradi wa BBT watu wenye ulemavu  wapo na kupitia mikopo ya halmashauri watu wenye ulemavu wanapewa pesa kwaajili ya kufanya biashara mbalimbali amesema haya kwenye mkutano 3RD G25 AFRICAN SUMMIT 2025 uliofanyika jijini dar es salaam. 

Habari picha na Ally Thabit Mbungo 


Friday, 21 February 2025

WAZIRI WA KILIMO AZITAKA NCHI ZA AFRIKA KULETA MAGEUZI KWENYE ZAO LA KAHAWA

 Husen Bashe Waziri wa Kilimo anazitaka Nchi zote za bara la Afrika kuweka mkazo mkubwa kwenye zao la kahawa kwa kutenga bajeti za kutosha kwaajili ya kununua pembejeo,Kuweka program kwa wakulima wa kahawa ,Kuwatafutia masoko ya kimataifa na kuwawezesha teknolojia za kilimo amesema haya kwenye mkutano wa  3RD G25 African Coffee Summit 2025 unaofanyika jijini Dar es salaam. 

Habari na Ally Thabit 

ANT EZEKIEL AJIUNGA NA CHAMA CHA CCM

 

Msanii Ant Ezekiel ameamuwa Kutoka chama cha Chadema na kujiunga na chama cha ccm kwani rais Dr samia anawaunga mkono wasanii kwa kiasi kikubwa kwa kuwapa mikopo na kuweka mazingira rafiki kwa wasanii na ameahidi atakuwa balozi wa chama cha ccm.

Habari picha na Ally Thabit 

STAMINA KUMLUDISHA ROMA TANZANIA


 Msanii wa Kizazi Kipya Stamina na balozi wa chama cha ccm amesema atamshawishi msanii Roma aliopo mafichoni nchini marekani aweze kurudi nchini tanzania na kujiunga na chama cha ccm.

Habari picha na Ally Thabit 

TANTRADE YAJIVUNIA NA TUZO


 Ratifa Mohamed Mkurugenzi  wa TANTRADE  amesema tuzo zitasaidia kuwakuza wafanyabiashara wadogo na wakati kwani biashara zao watazalisha bidhaa zenye ubora na watazingatia alama zote.

Habari na Ally Thabit 


MWENYEKITI WA CHAMA CHA KAHAWA WA AFRIKA APONGEZA MKUTANO WA WADAU WA KAHAWA


 Mwenyekiti wa Chama cha Kahaha bara la Afrika  amesema mkutano wa wadau wa kahawa utasaidia kuweka sera na sheria katika kukuwa kwa zao la kahawa na kutatuwa changamoto la zao la kahawa.

Habari picha na Ally Thabit 

Saturday, 8 February 2025

MKURUGENZI MKUU MTENDAJI WA HOSPITALI YA OCEANROAD CENCER INSTITUTE AMSHUKURU RAIS DR SAMIA

 Diwani Othman Msem Mkurunzi Mkuu Mtendaji wa Hospitali ya OCEAN ROAD CANCER INSTITUTE  anamshukuru rais Dr Samia  kwa kuweza kununua mashine mfano MRI na zinginezo kwaajili ya kufanya uchunguzi na tiba kwa nagonjwa ya saratani za aina zote . Pia anashuru kwa kuweza kutoa pesa nyingi kwaajili ya kununua dawa kwa wagonjwa wa saratani .

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji  Diwani Othman Msem anawataka watu kufanya uchunguzi wa miili yao lengo wakugundulika na saratani waanze matibabu mapema  kwani saratani inatibika . Ameishukuru Gsm Foundation kwa jitihada kubwa wanazozifanya  za kuzibiti na kupambana ili kutokomeza saratani za aina zote kwa  kutoa michango ya pesa,mawazo,elimu na vitu mbalimbali kwa kushirikiana na hospitali ya Ocean road cancer Institute. 

Amesema haya siku ya saratani duniani kwenye hospitali  ya Ocean road cancer Institute ambapo uazimishwa kila ifikapo tarehe 4 ya mwezi wa 2 duniani kote . 

Habari na Ally Thabit 


Friday, 7 February 2025

MASHUJAA WA SARATANI PAMOJA NA WADAU WANAOPIGA VITA SARATANI ZA AINA ZOTE WAPO KWENYE MATEMBEZI

 
Kama Inavyo Onekana Pichani  hawa ni Wadau wanaopiga vita ugonjwa wa saratani wapo katika matembezi Lengo la matembezi haya kuhiasa jamii kujitokeza kufanya uchunguzi kwenye miili yao kama wana magonjwa ya saratani au dalili ili waanze tiba mapema kwani saratani inatibika ukiiwai .


Habari picha na Ally Thabit Mbungo 

FAITH GUGU MKUU WA GSM FOUNDATION AAHIDI MAKUBWA KWENYE HOSPITALI YA OCEANROAD CENCER INSTITUTE

 Mkurugenzi Mkuu wa GSM FOUNDATION Faith Gugu amesema wataendelea kushirikiana na hospital ya Ocean road Cancer Institute katika mapambano ya saratani za aina zote lengo kutokomeza au kupunguza uogonjwa wa saratani na vifo vinavyotokana na saratani za aina zote kwani GSM FOUNDATION inatoa elimu kwa jamii ya kujilinda dhidi ya magonjwa ya saratani. Elimu hii inawafikia watu wenye ulemavu wa aina zote.

Amesema haya kwenye kilele cha maazimisho ya saratani yalio fanyika kwenye Hospitali ya Ocean road cancer Institute ambako uazimishwa kila tarehe 4 ya mwezi wa 2 duniani kote kila mwaka . 

Habari na Ally Thabit 

GLORIA KIDA MKURUGENZI WA ASASI YA SHUJAA WA SARATANI AIMIZA WATU KUPIMA SARATANI

 Mkurugenzi  wa Asasi ya Shujaa wa Saratani Gloria Kida anawataka watu kujitokeza kwa wingi  kupima saratani za aina zote Pia anawahimiza wanajamii kuchanja chanjo ya HPV wao na watoto wao kwani  ni kinga dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi .

Asasi yao Imetoa Elimu ya Saratani Katika  Mkoa wa Mwanza na Wilaya zote za Dar es salaam  amesema haya kwenye kilele cha week ya saratani iliyo fanyika kwenye Hospitali ya Oceanroad   Cancer Institute ambako kila mwaka uazimishwa tarehe 4 ya mwezi 2 duniani kote .

Habari  na Ally Thabit. 

ASCP MULIRO J. AELEZEA WATOTO WALIOJITEKA

 Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam  Limewapata na Kuwahoji wasichana wawili ambao ambapo mmoja wa miaka16  Mwanafunzi wa kidato cha pili na mwingine  wa miaka 12 Mwanafunzi wa Darasa la saba  wakazi wa vijibweni kigamboni kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo baada ya kutengeneza mazingira kuwa wametekwa  na watekwaji wanataka pesa.

Ufuatiliaji ulifanywa na kufanikiwa kubainiwatoto hawa walipokuwa na baada ya mahojiano ya kina  walikiri kutengeneza tukio hili la uongo ili waweze kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu toka kwa wazazi wao baada ya kutoweka  tarehe 26/01/2025 na kuelekea  Longoni Beach ambapo walikesha hapo hadi tarehe 27/01/2025 asubuhi na  baadae kuelekea maeneo ya Tungi hadi walipo kamatwa  wakiwa wanazunguka. Jeshi linalaani vitendo vya hivi vya watu wenye lengo la kujipatia  pesa kwa njia za udanganyifu.

Aidha, Jeshi la Polisi Kanda ya  Maalum Dar es salaam  katika kipindi cha Desemba hadi Januari 2025 katika kusimamia mifumo ya haki jinai mahakamani baadhi ya watuhumiwa mbalimbali walipatikana na hatia  ikiwa ni pamoja na Idrisa  Rasshid miaka [35]  Mkazi wa Kwembe  Kimara alihukumiwa  miaka 30 jela kwa kosa la kubaka kwenye Mahakama ya Wilaya ya  Kinondoni.  Paul Elisha miaka (37) mkazi wa Mbezi  Beach kwe nye Mahakama ya Kinondoni alihukumiwa kifungo cha maisha  jela kwa kosa la kubaka na Jackson Mgeta (34) mkazi wa Kawe alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kubaka.

Jeshi la Polisi lina wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana ili kuimarisha mifumo ya ulinzi shirikishi ikiwa ni pamoja na kutekeleza falsafa ya ulinzi shirikishi ili kuzuia  vitendo vya kihalifu. Imetolewa na Kamanda  Kanda Maalum ya Polisi Dar es salaam. 

Habari na Ally Thabit Mbungo.